Saturday, September 29, 2012

Chelsea mhhh... tupo juu jamani.


Chelsea imekuwa timu ya kwanza kuichapa Arsenal katika mechi za ligi kuu ya Uingereza msimu huu baada ya kuwachapa 1-2 katika uwanja wao wa nyumbani,Emirates siku ya Jumamosi.
Vijana wa Roberto Di Matteo ndio walikuwa wa kwanza kufunga katika dakika ya 20 kupitia mshambulizi Fernando Torres baada ya mkwaju wa adhabu kupigwa na Juan Mata.
Lakini katika dakika ya 42 mshambulizi Gervinho alifunga bao safi hivyo kuzifanya timu hizo mbili ziende mapumzikoni zikiwa sare ya 1-1.
Na katika dakika ya 52 ya kipindi cha pili, Mata alipiga mkwaju mwengine wa adhabu ambapo ulimshinda mlinzi Laurent Koscielny na badala yake kumgonga mguu na kuingia ndani huku ikimuacha Kiper wa Arsenal Vito Mannone hoi.
Wenger amekua akilalamika kwamba safu yake ya nyuma imekuwa ikizembea katika mipira ya adhabu.
Licha ya kufungwa huko, Arsenal walitawala ngoma hiyo nzima ya Jumamosi lakini safu ya mbele ya vijana hao wa Arsene Wenger iliyonekana kukosa makali na kuwa na kukosa umakini.
Chanzo: BBC Swahili

Yanga saaafiii...


Kocha mpya wa Yanga Ernstus Brands akisaini mkataba wa mwaka mmoja kwa ajili ya kuiona klabu ya Yanga,kushoto ni makamu Mwenyekiti wa Yanga Clement Sanga akimpa maelekezo.Kabla ya kujiunga na Yanga, kocha huyo alikuwa akiifundisha APR ya Rwanda.

Picha kwa hisani ya mjengwa blog.

Friday, September 28, 2012

What about this, and ask yourself if you once happened to be her judge for a minute...


Bertha Charles doing the dew at BSS audition.


FILIKUNJOMBE ADAI YEYE, MKONO, LUGOLA WALIPONZWA NA PINDA, NAPE ATAKA WASIORIDHIKA WAKATE RUFAA, WASOMI WAPONGEZA



SIKU moja baada ya Halmashauri Kuu ya CCM (Nec), kutangaza majina ya wagombea, baadhi ya vigogo walioachwa kwenye uteuzi huo wameeleza ya moyoni, huku Mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe akisema anaamini ametoswa kwa sababu alitia saini ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Katika Bunge la 10 lililoketi Aprili mwaka huu, baadhi ya Wabunge wa CCM akiwamo Filikunjombe, Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono na Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugola, waliunga mkono hoja ya kutokuwa na imani na Pinda iliyokuwa imeanzishwa bungeni na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe wa Chadema. 

Wabunge hao wa chama tawala, waliungana na wenzao wa upinzani kutaka kupiga kura za kutokuwa na imani na Pinda kutokana na kile kilichoelezwa kuwa ameshindwa kuisimamia Serikali kwa kuwawajibisha mawaziri wazembe. Hata hivyo, mpango huo haukufanikiwa baada ya Spika wa Bunge Anne Makinda kueleza kuwa haukufuata taratibu zinazotakiwa.
 

 Filikunjombe alipotakiwa jana kuzungumzia kuenguliwa kwake kwenye kinyang'anyiro cha uchaguzi wa ndani ya chama, alisema anaamini yeye na wenzake hao wa CCM, wametoswa kwa sababu ya kushiriki mpango wa kumng'oa Waziri Mkuu Pinda. Hata hivyo, alisema amelazimika kukubali hali hiyo na kupokea matokeo, kwa kuwa hatua yake ya kusaini kitabu hicho ilitokana na nia njema kutaka Waziri Mkuu ajiuzulu ili mambo fulani muhimu katika jamii yafanyike. 

Filikunjombe alibainisha kuwa alisaini kitabu hicho cha kutokuwa na imani na Pinda akiwa na akili timamu na alikuwa anajua kinachoweza kutokea kutokana na hatua yake hiyo. "Nimesaini kitabu kile kwa nia njema, nikiwa na akili timamu na sijutii uamuzi wangu huo, ila siwezi kuwasemea Kigwangalla (Khamis mbunge wa Nzega) na Bashe (Hussein). Lakini sisi watatu (yeye, Lugola, Mkono) tumeenguliwa kwa sababu hiyo (ya kutokuwa na imani na Pinda)." Aliendelea: "Nashangaa leo naonekana adui wa chama wakati nilikuwa nakinusuru na kusema kweli adui wa CCM ni Wabunge wa chama hicho ambao hawakusaini kitabu hicho cha kutokuwa na imani na Waziri Mkuu, " alisema Filikunjombe. 

Mkono Mbunge wa Musomo Vijijini, Nimrod Mkono alisema kutoswa kwake ni uamuzi wa watu aliowaita wenye chama. "Walikata jina langu nikakata rufaa, likarudishwa Dodoma, lakini walipokutana wakaona sifai. Wakaamua kunifukuza sasa hapo mimi nifanye nini?" alihoji Mkono. Mkono alisema huu ni utaratibu wa chama chao cha CCM ambao umewapa baadhi ya watu haki ya kuwafukuza wengine bila kuwapa fursa ya kujitetea. "Kama ilivyotokea kwangu wamekaa na kuona Mkono hafai, fukuza basi wakafanya hivyo na hiyo haijalishi kama nilisaini kutokuwa na imani na Waziri Mkuu au la.

 Suala la msingi ni kuwa Mkono amefukuzwa na atarudi kama ilivyokuwa kwa mwana mpotevu." alisema bila kufafanua. Kigwangalla Mbunge wa Nzega, Dk Hamis Kigwangalla alisema anaheshimu uamuzi wa vikao vilivyokaa na kufikia uamuzi uliochukuliwa na kwamba, ataendelea kuwa mwanachama na kukitumikia chama pamoja na wananchi kwa nguvu zote bila kinyongo. “Nitaendelea kuheshimu vikao vya chama changu na kuwa mwanachama hai ingawa sijajua wametumia vigezo gani kuteua majina hayo,” alisema Dk Kigwangalla. Bashe Kwa upande wake Bashe alisema kilichotokea ni uamuzi wa chama na vikao halali vilivyokaa na kuchukua uamuazi huo. 

“Sijui kwa nini jina langu halikupitishwa, lakini nitaendela kuwa mwanachama na kuwatumikia wananchi wenzangu wa Nzega,” alisema Bashe. Katika kuhakikisha hilo, Bashe alisema leo anakwenda Nzega kupeleka mifuko ya saruji tani 18 kwa ajili ya ujenzi wa ofisi za kata za chama hicho wilayani humo. 

Nape ajibu Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alitaka makada waliotoswa na wenye kinyongo wawasilishe malalamiko yao CCM kwa maandishi badala ya kulalamika nje ya utaratibu."Wathibitishe kwa maandishi nasi chama tutajua la kufanya, kwani wabunge hao hawakuingia katika vikao vilivyotoa maamuzi sasa nashangaa kusikia katika vikao tuliwajadili na hoja iliyowaondoa ni hiyo," alisema Nape. Maoni ya wasomi Wakizungumzia uteuzi huo wasomi na wanasiasa walitoa maoni tofauti huku baadhi wakisema chama kinatakiwa kuwa na sera na mtizamo wa kuliletea maendeleo taifa bila kujali kama chama kinaongozwa na wazee au vijana.

 Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Benson Bana alisema uamuzi huo wa CCM umeonyesha kuwa, ndani ya chama hicho hakuna aliye juu kuliko mwenzake. “Wapo waliosema wakitoswa patachimbika, lakini wametoswa na hapajachimbika, uamuzi wa kuwatosa watu wa aina hii utarejesha nidhamu ndani ya chama hicho licha ya kuwa kazi bado ni kubwa,” alisema Dk Bana. Profesa Gaudence Mpangala alisema vijana kupewa nafasi kubwa ya kugombea nafasi mbalimbali ndani ya CCM, hakuna maana kuwa sera na mtizamo wa chama hicho utabadilika. 

 “Kuwa na wanachama au wagombea wenye umri wa wastani(vijana) sio kigezo cha chama kufanya vyema kwa sababu hawawezi kubadili sera na mtizamo wa chama husika,” alisema Mpangala. Dk Kitila Mkumbo alisema kuingiza vijana wengi katika mpambano huo ni hatua ya ukomavu wa kisiasa kwa kuwa chama hicho awali hakikuwa na utaratibu mzuri wa kuwapa nafasi ya uongozi vijana. “Awali Chadema ndio kilionekana chama kinachowapa nafasi zaidi vijana, lakini kwa hatua hii ya CCM ni nzuri, sasa tunasubiri utendaji wao kama utakuwa na manufaa kwa taifa,” alisema Mkumbo. 

 Bashiru Ally alisema kama kigezo cha kuweka vijana wengi kitazingatia msimamo, fikra na ufanisi katika utendaji kazi wao basi taifa lina kila sababu ya kuunga mkono hatua hiyo.Alisema kwa kuwa vijana ndio chachu ya maendeleo kwa mataifa mbalimbali duniani, hatua ya CCM kuwapa nafasi vijana ni nzuri kama wakiifanya kazi hiyo kwa manufaa ya taifa kwanza. 

Habari hii imeandikwa na Ibrahim Yamola, Fidelis Butahe, Elizabeth Edward na Joseph Zablon,Mwananchi .

Kocha mpya wa Club ya Yanga awasili leo...

 Brandts wa pili kutoka kulia, akiwa na viongozi wa Yanga. Kulia ni Seif Magari. Kushoto kwake ni Bin Kleb na Majjid.




Na Mahmoud Zubeiry
KOCHA mpya wa Yanga, Ernstus ‘Ernie’ Wilhelmus Johannes Brandts, beki wa zamani wa kimataifa wa Uholanzi na klabu ya PSV Eindhoven ya Holanzi, amewasili usiku huu (saa 3:45) katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere na ndege ya KLM tayari kusaini mkataba na kuanza kazi katika klabu hiyo.
Brandts amepokewa na Katibu Mkuu wa Yanga, Lawrence Mwalusako na viongozi wengine, Abdallah Ahmad Bin Kleb, Seif Ahmad ‘Magari’ na Majjid Suleiman na amesema anaijua Yanga ni timu nzuri, kubwa hana shaka ataiwezesha kufanya vizuri katika medani ya soka Afrika.
Yanga, imetimiza malengo yake ya kuwa kocha mpya, kabla ya kucheza na wapinzani wao wa jadi, Simba SC, Oktoba 3, mwaka huu baada ya kumfukuza Mbelgiji, Tom Saintfiet, kutokana na kuwasili makubaliano na Brandts, ambaye ataanza kazi mara moja kesho.
Mholanzi huyo aliyefukuzwa APR ya Rwanda baada ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame, Agosti mwaka huu amepewa ukocha wa Yanga, baada ya Mbrazil Marcio Maximo kukataa nafasi hiyo kwa mara ya pili.
Mtaalamu huyo, alizaliwa Februari 3, mwaka 1956 mjini Nieuw-Dijk, Gelderland, mbali na PSV Eindhoven, alichezea pia Roda JC Kerkrade, MVV Maastricht na De Graafschap.
Brandts aliichezea mechi 28 timu ya taifa ya Uholanzi na kuifungia mabao matano na pia alicheza Fainali za Kombe la Dunia mwaka 1978.
Katika fainali hizo, Raundi ya pili kwenye mechi na Italia, aliweka rekodi ya kuwa mchezaji pekee aliyezifungia mabao timu zote katika mechi moja kwenye fainali za Kombe la Dunia.
Alianza kujifunga dakika ya 18, kisha akaisawazishia Uholanzi dakika ya 50 katika mechi ambayo, mchezaji mwenzake Arie Haan baadaye aliifungia timu yake bao la ushindi na kutoka kifua mbele kwa mabao 2–1.
Alipostaafu soka akawa kocha na katikati ya msimu wa 2007–2008, Brandts aliambiwa hataongezewa mkataba NAC-Breda, licha ya matokeo mazuri ya kushika nafasi ya tatu katika Ligi Kuu Uholanzi (Eredivisie), ingawa uamuzi huo haukuwafurahisha mashabiki wa timu hiyo na nafasi yake akapewa Robert Maaskant kuanzia msimu wa 2008–2009.
Akateuliwa kuwa Kocha wa Rah Ahan mwaka 2009, kabla ya kufukuzwa Desemba 2009 na kuibukia APR ya Rwanda mwaka 2010, ambako ‘riziki’ yake imeisha miezi miwili iliyopita na sasa amepata maisha mapya Yanga.
Akiwa APR, Brandts alifungwa mechi zote mbili na Yanga iliyokuwa ikifundishwa na Mbelgiji Tom Saintfiet katika Kombe la Kagame, moja ya makundi 2-0 na nyingine ya Nusu Fainali 1-0. Yanga iliibuka bingwa, ikiifunga Azam FC 2-0 kwenye fainali.
Brandts atakutana na wachezaji wake wa zamani wawili Yanga, beki Mbuyu Twite anayeanza msimu wa kwanza katika klabu hiyo na kiungo Haruna Niyonzima anayeingia katika msimu wa pili, ambao alifanya nao kazi APR. 

Habari na picha kwa hisani ya Bin Zubeir bongostaz.blogspot

Jamani eeehe jembe nawashauri watanzania mliojiandikisha vitambulisho vya uraia nendeni mkahakiki majina yenu...

 Jamaa hakutaka kusubiri asubuhi, alianza kuhakiki jina lake kwa kutumia mwanga wa simu. Asubuhi kazini.

 Jembe na mimi sikutaka kujichosha, nilihakiki jina langu kwa kutumia simu ya tochi. Lakini sikuambulia kitu macho yameshakuwa ya kitu kizima tena. Kayaoni jamanii...

                                                Watu wa Tanga wenyewe wanaita jitangazo.

Zitto Kabwe asema hakuteleza kusema anagombe Urais mwaka 2015...


Narudia, mwaka 2015 sitagombea Ubunge. Nitafanya kampeni ya Urais, ama mimi kama mgombea wa chama changu CHADEMA au kama mpiga debe wa mgombea wa chama changu. Miaka 10 ya Ubunge inatosha na kwa ngazi hiyo ni vema niwaachie wengine wasukume mbele gurudumu la maendeleo ya Jimbo na mkoa wetu. Huu ndio uamuzi wangu wa mwisho na nimeshawaeleza wananchi wa Jimbo langu na mkoa wa Kigoma toka mwaka 2005. 

NB: Hii imetoka kwenye ukurasa wake wa facebook.... tembelea na wewe ujionee..

CUF yaisaidia CCM kushinda Umeya Mwanza...


Mgombea wa kiti cha umeya katika Halmashauri ya jiji la Mwanza kupitia CCM na diwani wa kata ya Mkolani Ndg Stanslaus Mabula, ameshinda kiti cha umeya kwa jumla ya kura 11 dhidi ya mgombea wa CHADEMA diwani wa kata ya Mahina Ndg Charles Chinchibera aliyepata kura 8.

chadema ilikuwa na madiwani 8, CCM madiwani 7 na CUF madiwani 2.

TAMKO LA CHAMA KUKANUSHA SHUTUMA ZA CHAMA CHA CUF KUFANYIWA VURUGU NA CHADEMA.



Ndugu wananchi na wanahabari, Siku ya terehe 27 Alhamisi Septemba 2012 chama cha wananchi CUF walitoa taarifa ya malalamiko kwa vyombo vya habari na mitandao kuwa wanachama wa CHADEMA wamewafanyia vurugu kwa kuwapiga mawe na kuwa jambo hilo limehamasishwa na viongozi wa chama katika mkoa wa Arusha pamoja na Mhe Godbless Lema. Wote tunafahamu kuwa siku hiyo hiyo katika viwanja vya soko la Kilombero wafanyabiashara ndogo ndogo walikuwa wamevamia na walikuwa wakijigawia maeneo, baada ya eneo la awali walilopewa la viwanja vya NMC kushindwa kuwachukua wafanyabiashara wote na halmashauri kushindwa kutoa majibu kwa wafanyabiashara hawa ambao waliwaambia wote waende NMC. Kwanza tunapenda kutoa pole kwa viongozi wa CUF kwa jambo hili lililowapata. 

Wao kama watu na Watanzania wenzetu tunawapa pole sana. Pili, CHADEMA inakanusha kuhusika na jambo hili. Hii si tabia ya CHADEMA na kamwe haiwezi kuwa tabia ya CHADEMA kufanya siasa chafu za namna hiyo. CHADEMA tunajali sana amani na upendo, na hii ndiyo tabia na makuzi yetu Watanzania. Katika mazingira haya, CHADEMA tunachukua fursa hii kuvikaribisha vyama vyote mathalani CUF, Arusha ni yetu sote na tutumie demokrasia vizuri kufanya kazi nzuri ya siasa kwa ajili ya kusababisha na kuleta matumaini kwa Watanzania hawa ambao serikali ya chama cha mapinduzi imeshindwa kuwaletea. 

CHADEMA hatuna shida na ushindani wa kisiasa katika mazingira ya kidemokrasia kwa maana ndio wakati pia wa wananchi kupima na kujua nani mkweli na ama nani anafanya kwa dhati ya kweli. Hivyo tunawakaribisha CUF karibuni Arusha na wala wasitafute kisingizio cha kuegemea ili CUF ianze kutajwa tajwa kwa kutumia mgongo wetu. Sambamba na hili, CHADEMA mkoa wa Arusha tumesikitishwa sana na tamko la CUF lilitolewa na Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na haki za BInadamu Mhe Abdul Kambaya, tamko lenye matisho na lugha isiyofaa. Moja na maneno ya tamko hilo wamesema, nukuu “Uwezo wa kuwafanya tutakavyo tunao na kwa sababu wameanza tunaweza kumaliza”. 

Wakazi wa Arusha na Watanzania wapime na waone, haya si maneno yanayoweza kutoka kwenye kichwa cha mtu anayefikiri vizuri, mtu anayeipenda nchi yake na kuheshimu utawala wa sheria. Zaidi ya hapo tamko hilo limesema pia, “Ile ngangari kwa polisi tunaweza kuwahamishia wao wakose pa kukaa”. Katika yote haya, niwaombe wakazi wa Arusha, Wanachadema na hata wanachama wa vyama vingine tuwapende na tuwakaribishe CUF Arusha na sote tufanye kazi ya siasa kwa nguvu za hoja. 

CUF wanaweza kufanya hicho wanachotaka kufanya lakini CHADEMA kamwe hatupo tayari kwa vurugu ya aina yoyote, aidha tunawakaribisha kwa moyo mmoja na kama wapo tayari basi tufanye siasa zenye tija na manufaa kwa wakazi wa Arusha. Aidha nitoe onyo kali sana kwa mamluki ambao wamekuwa wakijifanya kondoo kumbe ndani ni mbwa mwitu. Mara kadhaa watu hawa wamekuwa wakisababisha fujo ili kukifanya CHADEMA kionekane kuwa ni chama cha vurugu. 

MAMLUKI ni sumu, tukimgundua na kumthibitisha mtu wa aina hiyo katikati yetu tutamtangaza mbele ya jamii kuwa yeye ni sumu na kuomba wananchi wamtenge maana anapingana kwa kuleta hila na unafiki kwenye kazi ya kuwakomboa Watanzania. 

Niwatangazie mamluki hamtatuweza na tutawagundua tu. Mwisho, tunapoelekea kwenye marudio ya uchaguzi mdogo kwenye kata za Daraja II kwa Arusha mjini na Bangata kwa wilaya ya Arumeru Magharibi, nirudie kusema maneno ya Mhe Lema kuwa iwapo viongozi na watumishi wa umma watajihusisha na kushiriki kwa kufanya kampeni za kisiasa wakiwa wanatumia magari na vifaa vingine vya serikali watu hawa tutawakamata na tutawapeleka huko wanakostahili kupelekwa wezi na vibaka wengine. Hii ni tahadhari tunamaanisha kweli na wananchi wote wawe makini “wakamate mwizi” lengo likiwa ni kuweka adabu kwa watumishi na viongozi umma wanaovunja sheria ya utumishi wao kwa umma na matumizi ya rasilimali kwa namna isivyotakiwa kisheria.

 CHADEMA tutashiriki chaguzi hizi na tunawaomba wakazi wote wa maeneo haya tushiriki kwa utulivu na amani. WANACHADEMA wote tuendelee kuwa majasiri, tusiwe waoga na tusimamie kweli na haki. 
“Hakuna kulala Mpaka Kieleweke” Amani Sam Golugwa KATIBU WA CHADEMA MKOA WA ARUSHA: golugwa@gmail.com Source JF

Mshindi wangu Dada Bertha Charles leo alikuja kunitembelea jembe lenu nyumbani Tandale kwa mtogole mtaa wa mkunduge kwa mfuga mbwa aka kwa mafundi simu.

                                  Hapa akionekana kufurahia kufika kwa kaka yake jembeeeee...

Akiwa ametoklezea na jembe baada ya kufanyiwa interview bila ya kujijua. Si unajua tumepikwa katika fani hii ya uandishi?

Kuanzia sasa nimepunguza ama kuacha kushabikia shindano la kusaka vipaji Tanzania la BSS, sina ugomvi na shindano hilo wala waandaaji. Sababu ya msingi ni kuwa mshindi wangu ametangulia kutolewa.

Leo dada Bertha ambae alikuwa ni mshiriki akiwakilisha jiji la maraha la Dar es Salaam aliamua kunitafuta kaka yake, nikamuelekeza nyumbani na nashukuru hakupotea. Nilizungumza nae mambo mengi sana, lakini nilijitahidi kumuonyesha kuwa kila kitu kipo sawa ingawa moyoni kwangu haikuwa hivyo.

Aliposhuka kwenye 'bajaj' ama tuktuk, kama kawaida yake alianza kuniita jina langu kwa kwikwi kama mtu aliekuwa akitaka kulia. Lakini nikamkumbatia na kumminya mwili wake ishara ya kumuonyesha upendo na kumwambia 'every thing is okey, there is life even outside the BSS' Nashukuru alielewa na kuyarudisha nyuma machozi yake. Namjua kwa kupenda kulia.

Nilipanga nikionana nae nimuhoji baadhi ya maswali halafu niandike chochote ndani ya kidojembe, ila sikutaka ajue chochote kinachoendelea. Najua kwa sasa hapendi vyombo vya habari ila amesahau kama kaka yake ni miongoni mwao. (So this is a surprise to you Bertha)

Alinambia wale washiriki wote walikuwa ni wa kawaida sana na kilichomfanya atoke mapema mpaka sasa hajui ni kitu gani. Hata baadhi ya wakufunzi na washiriki wenzie hawajui ni kitu gani kilitokea siku ile alipotajwa jina lake.

Cha ajabu nilipomdadisi zaidi ili kujua kama anahuzunika kwa kutolewa kwake, alinijibu "Kimsingi kido mimi sijutii kutoka, najihisi kama kuna kitu kimepungua ndani ya mwili wangu baada ya kutoka, hata 'crue' (watu waliokuwa wakichukua picha) ilishangaa sikulia wala sikucheka. Hakika nilikuwa katika wakati mgumu sana, si kwa ubaya but i feel like i'm free," alisema Bertha.

Baada ya BSS maisha yanakwendaje mtaani: "Nimeamua nikafanye ngoma katika moja ya nchi hizi tatu za Afrika Mashariki, Bongo, Kenya ama Uganda. Na aliendelea kufafanua kuwa akiitwa katika tamasha la top 20 mwisho wa shindano la BSS atakuwa na ngoma yake ambayo kwa wakati huo itakuwa hit mbayaaa... lakini nataka nikafanye ngoma kali ambayo itawaonyesha mashabiki wangu kuwa naweza na kushiriki BSS ilikuwa ni kutaka kupata njia na nashukuru sana BSS imenisaidia kunikutanisha na watu wengi.

"Nimeweza kufunzwa mambo mengi juu ya muziki ambayo sikuwa nikiyajua na sasa ninatambua aina za uimbaji na hata Chief Judge Madam Rita ametuambia washiriki wote tukiwa na shida ya aina yoyote tumuone atatusaidia," alisisitiza Bertha.

Swali la kizushi kwake ilikuwa ni uhusiano wake na judge matata wa BSS Salama Jabir, "Huwezi amini yule dada ananikubali sana tofauti na watu wanavyoona kwenye TV. Mwanzo niliona kama ananichukia lakini ni mshikaji ile mbaya."

baada ya kuzungumza nae sana niliamua kumsindikiza mpaka kwao na jembe kurudi uswahilini kwetu.

Bertha Charles wewe ndie uliekuwa ukinifanya nitazame BSS na sasa sioni hiyo sababu. Kwa hakika tulikuwa na mipango mingi sana kwa dada huyu, nilimweleza namna wanafunzi Uganda walivyokuwa wakimpenda mpaka kwenye facebook Page ya Epic BSS yeye ndie aliekuwa akiongoza kwa 'likes' wengine mhh.....

Na hata uamuzi wa kutengeneza facebook page yake ambayo tayari nishaanza kuiandaa na picha nishakusanya tangu za shindano la KIU Star Search lililofanyika mwaka 2008 chuoni KIU Kampala. Aliposikia hivyo macho yake yalianza kung'aa nikajua anataka kulia. Nikaanza kumchekesha ili kumsahaulisha. Ila najua anaumia na alikuwa akirudia neno hili la kizungu ambalo lilikuwa likinikera sana 'i'm sorry i know i have disappointed you guys'.

HAFIDH KIDO
DAR ES SALAAM, TANZANIA
kidojembe@gmail.com
0713 593894/ 0752 593894
28/09/2012

Nyeregete Mbeya hii.......


                                 Umkhomboti unajipimia mwenyewe, usinichoshe nisikuchoshe.

Picha zote kwa hisani ya Mjengwa blog.

One day tour in Kampala-Uganda on my way back to Dar es Salaam.

                                          The beautiful yard of Uganda parliament in Kampala.


 This monument was installed in 2007  to mark the Common Wealth Heads of Government Meeting 'CHOGM' held in Kampala and chaired  by Her Majesty Queen Elizabeth II.

 This is Mabira forest, the famous forest in Uganda which rose a lot of confusion in last year where the rumor spread that the forest has been sold to one of the giant sugar industry in Mukono-Uganda.

 Vendors display their goods to travelers at Mabira forest. There is delicious chicken here big and cheap...

                         People removing unwanted materials from River Nile at Owen's falls Jinja.

Owen Falls Jinja Town where River Nile crossed to Egypt. This bridge connect Kampala and Other parts of Uganda and Kenya. During Kagera war between Tanzania and Uganda TPDF (Tanzania People Deffence Force) aimed to blow this bridge but Mwalimu Nyerere refused the idea because he professed that one day we will be good friends with Uganda and in-need to one another, by the way this bridge connect even Tanzania if we use Arusha route and it is very expensive to construct.


                             The above statement elaborate more about the monument above my head...

                                            Don't play with Kampala they even have sub way.


           Bayimba festival, i always like this festival conducted every year at National Theater in Kampala.



                                                           Kampala is a nice place to be.

Thursday, September 27, 2012

Tanzania nzuri jamani

 Eldoret hii jamani, Niliingia usiku lakini kwakuwa huu mji ninaupenda nikaamua kubaki na kumbukumbu japo si nzuri.



Hii ni Longido wadau, milima ya Oldonyo Sambu, inapendea kwelikweli jamani Tanzania nzuri kweli.....

Uchungu wangu kwa watoto wa mitaani bado ipo palepale kila ninapokwenda Duniani.




Hawa watoto wapo mpaka wa Busia, Kenya na Uganda. Wanakaa hapo kuanzia asubuhi mpaka usiku kazi yao kubwa ni kuwaomba wasafiri wanaokwenda Kenya ama Uganda. Wengine wanaiba ama kuwalaghai wasafiri hasa wanawake nyakati za usiku.

Kwa maana unapofika mpakani ni lazima ushuke kwenye gari ukaguliwe na kugongewa muhuri katika pasi ya kusafiria 'visa', hivyo wanatumia mwanya huo kuwalaghai abiria wageni kwa kujidai wanawaomba lakini wakiona kitu kimekaa vibaya wanapora na kukimbia.

Katika kila mipaka ya nchi kuna eneo ambalo halimilikiwi na nchi yoyote katika nchi mbili zilizopakana, wazungu wanaita 'no man's land' Hivyo eneo hilo halikai askari kwa maana halina mtu. Wengi hutumia mwanya huo kukaa katika eneo hilo na kufanya uhalifu.

Wapo watoto ambao nilianza kuwaona tangu mwaka 2008 mpaka sasa wamekuwa wakubwa, wanakunywa ulevi na kuvuta gundi. Wachafu na wakorofi sana.

Lazima serikali za nchi mbili hizi zikae pamoja kujadili watoto hawa maana lazima watakuwa wanahusika katika moja ya nchi hizo mbili Kenya ama Uganda.

HAFIDH KIDO
DAR  ES SALAAM, TANZANIA
0713 593894/0752 593894
kidojembe@gmail.com
28/09/2012

Bukoba nitarudi tena....

 Hivi mzee kama huyu ukimwambia atoe maoni ya katiba mpya atazungumza nini unadhani?

                     The beautiful view of Rwamishenye suburb in Bukoba District Kagera Region in Tanzania.

                                                      Bukoba town, city center.

Ubunge sasa basi: Zitto Kabwe..


Na: Frank Sanga na Anthony Kayanda, Kigoma, MWANANCHI.

MBUNGE wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe amesema hana mpango wa kugombea ubunge mwaka 2015 badala yake anajipanga kuwania urais. Zitto alisema hayo jana alipozungumza na wananchi katika mjadala ulioandaliwa na asasi ya kiraia ya Meza ya Duara uliokuwa unafanyika maeneo ya Soko la Mwanga, mjini Kigoma. Zaidi ya watu 200, ambao walihudhuria katika mjadala huo wa wazi walimuuliza maswali mbalimbali mbunge huyo, huku mmoja akigusia kuhusu tetesi za mara kwamba Zitto anataka kugombea urais katika uchaguzi ujao.


 “Nimefanya kazi kubwa katika kazi yangu ya ubunge, nimeleta mabadiliko mengi kuanzia bungeni mpaka jimboni. Nadhani inatosha na hata nikiongezewa miaka mingine sitaweza kufanya yale yaliyonishinda katika kipindi cha miaka kumi. “Kama Mungu ataniweka mpaka mwaka 2015, sitagombea ubunge tena kwa sababu kazi niliyofanya inatosha. Natangaza rasmi kuwa nitagombea urais kupitia chama changu cha Chadema, bila kusababisha msuguano wowote na sitaki kuingia katika historia ya kurudisha nyuma harakati za upinzani kushika dola,” alisema Zitto.

 “Nataka kuleta changamoto mpya, nitawaeleza watu wa chama changu nia hiyo na nitatoa hoja za msingi. Hata kama sitapata ridhaa yao, lakini huo ndio msimamo wangu. “Iwapo chama kikiona sistahili au sifai, nitakubaliana na uamuzi huo. Watu wengi wanadhani urais ni cheo, hawajui kuwa ni nafasi ambayo inakufanya ufanye vitu ambavyo ni vikubwa na vya maendeleo kwa wananchi.” Atangaza kugombea urais Katika hatua nyingine Zitto alisema ana mpango wa kuwania urais kupitia Chadema katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015. “Kwanza nataka niwahakikishia watu wa Kigoma msiwe wanyonge…mna uwezo wa kutoa rais wa nchi hii,” Zitto alianza kujibu swali hilo na kuendelea. 

Hata hivyo Zitto alipoulizwa baadaye na Mwananchi kuwa mwaka 2015 atakuwa na miaka 39, hivyo kukosa sifa ya kugombea urais kwa mujibu wa katiba alijibu; “Nadhani nina uwezo wa kuwa rais, sidhani kama Katiba inaweza kumzuia mtu mwenye uwezo asigombee na ndio maana ninaamini kuwa kipengele cha kuwa na miaka 40 kitabadilishwa katika katiba mpya.”

 “Nchi za Kidemokrasia lazima vyama vibadilishane utawala wa kuongoza nchi kama ilivyo katika nchi za Ghana na Zambia. Tanzania inatakiwa kuiga mfano wa nchi hizo,” alisema Zitto Katika kukazia hilo, Zitto alisema anashangazwa na umaskini uliopo Tanzania wakati mwaka 1976 uchumi wake ulikuwa sawa na nchi ya Malaysia, lakini mpaka kufikia mwaka 2001, Malaysia ilipunguza idadi ya watu wanaoishi chini ya dola moja kutoka asilimia 56 mpaka kufikia asilimia tatu huku Tanzania ikipunguza kutoka 51 mpaka 46. Katika hatua nyingine, Zitto alikana kuwa, Chadema ni chama cha udini, ukanda, ukabila ila akasisitiza kuwa ni chama cha kitaifa. 

 “Ndugu zangu naomba mnielewe, Chadema si chama cha ukabila, ukanda wala udini bali ni chama cha kitaifa. Hizo ni propaganda za wapinzani wetu,” alisema Zitto baada ya kuulizwa na mmoja wa washiriki kuhusu tuhuma za chama hicho kuwa cha Kikanda.

 “CCM imewahi kudai CUF ni chama cha Waislamu, na sasa wanasema Chadema ni chama cha Wakristo, sasa wao CCM ni chama cha wapagani au cha watu gani?” Alihoji Zitto. Alisema ili kuthibitisha kuwa Chadema si chama cha Kikanda, matokeo ya urais wa mwaka 2010, Dk Wilbroad Slaa aliongoza dhidi ya wagombea urais wengine kwa kupata kura nyingi katika Jimbo la Manyovu mkoani Kigoma na hivyo kufanya kupata asilimia nyingi kuliko sehemu yoyote Tanzania

 Chanzo: http://www.mwananchi.co.tz/habari

AMEEN KASHMIRI, MWANAJESHI MZALENDO WA TANZANIA ALIYEPITIA MENGI.




"MZIGO MZITO APEWE MNYAMWEZI".

Historia ya Tanzania ina mengi na ina wengi ambao hawajazungumzwa, kiasi ambacho kuna mambo yakizungumzwa basi yanaweza kukusisimua na kukufanya ujisikie fahari sana kuwa Mtanzania.

Leo tunamzungumza Mzee wetu Mashuhuri Ameen Kashmiri. Askari Mstaafu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) ambaye historia ya maisha yake inatupa mafunzo na kutufamamisha mengi sana ambayo hatukuwa tukiyajua.

Ameen Kashmiri alizaliwa tarehe 31 mwezi Oktoba mwaka 1935 huko Mjini Tabora wakati huo kukijulikana kama Jimbo la Magharibi, sehemu kubwa ya maisha yake ya utottoni ameyatumia huko wakati Baba yake ambaye alikuwa Mfanyakazi wa Shirika la Reli la Tanganyika alipokuwa kwenye Tawi hilo la Tabora.

Maisha ya Wafanyakazi wa wakati huo yalikuwa ya kuhamahama sana jambo ambalo lilimfanya Mzee Kashmiri asikae sana Tabora. Alihamishiwa Mkoani Dodoma, kisha Dar es salaam ambako nako hakukaa sana kabla ya kuhamishiwa Jimboni Tanga ambako ndipo sehemu alitumia sehemu kubwa ya maisha yake na ndipo Elimu na Mafunzo ya Mwanawe Ameen yalipopatikana.

WITO WA KUTUMIKIA UMMA, UBAGUZI KWA WATANGANYIKA.

Mwaka 1956 Bwana Ameen Kashmiri alihitimu Elimu yake ya Upili (Sekondari) katika Skuli Maarufu Jijini Tanga iliyojulikana kwa jina la Shule ya Karimjee (Sasa hivi ikijulikana kama Shule ya Sekondari Usagara), ambapo kwa wakati wake alikuwa mmoja ya wanafunzi wenye uelewa mkubwa sana.

Tokea Shuleni yeye na baadhi ya Wenzake walivutiwa sana na habari na masimulizi ya Ushujaa, Ujasiri na kusisimua ya wazee wengi wa Tanga ambao walikuwa Sehemu ya Jeshi la Wakoloni wa Kiingereza lililokwenda Burma na Somalia wakati ule wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia, na hivyo kuwafanya wavutiwe sana na wawe na wito wa kuwa Maaskari Jeshi.

Mara tu alipomaliza Shule alifanya jitihada mbalimbali za kuomba kujiunga na Jeshi lakini mara zote alikataliwa. Pamoja na kuwa alionekana mweupe kwa rangi tofauti na Watanganyika wengine lakini bado alibaguliwa na Maofisa wa Kikoloni kwa kuwa Rangi yake haikuondoa Utanganyika wake au kubadili lafudhi yake ya Kiswahili safi, kwa wakati husika Askari wa Jeshi la Kikoloni la Tanganyika (Kings African Rifles) hawakuwa wakipenda sana kuwaingiza vijana wa Kitanganyika Jeshini kwa sababu mbalimbali.

Akiwa kakatishwa tamaa kwa kukataliwa kwake kuingia Jeshini, Ameen alikataa kuomba nafasi mbalimbali za kazi ambazo zilikuwepo kwa watu wa kiwango chake cha elimu kwa wakati huo. Baada ya Ushauri na kubembelezwa sana na baba yake aliamua kukubali ajira ya Uhasibu katika Kampuni ya Tom Co. Ltd kazi ambayo pamoja na kuwa hakuipenda lakini aliifanya kwa ufanisi sana kiasi kwamba baada ya muda tu alipandishwa cheo na kuwa Mhasibu Mkuu wa Kampuni.

MCHAKAMCHAKA, ASKARI MKAKAMAVU AMEEN KASHMIRI.

Mwishoni mwa Mwaka 1957 Jeshi la Wakoloni lilifungua Milango kwa Vijana wa Kitanganyika kujiunga nalo. Wakati huo wito na kampeni ilifanywa nchi nzima ili kuwahamasisha na kuwasajili vijana mbalimbali ambao walitaka kujiunga na Jeshi hilo nafasi ambayo Mzee Ameen hakuiacha impite hivi hivi, hivyo akawa miongoni mwa vijana wachache wenye Elimu wa Kitanganyika wa wakati huo kukubali kujiunga na Jeshi hilo.

Baada ya Maombi na Usaili mwezi Januari mwaka 1958 Mzee Ameen Kashmiri, Mrisho Sarakikya na Alex Nyirenda walichaguliwa kujiunga na Mafunzo ya Juu ya Kijeshi katika Chuo cha Royal Military Academy, Sandhurst, Nchini Uingereza ambapo baadaye Mzee Mrisho Sarakikya aliachwa katika Orodha ya Wanafunzi waliotakiwa kwenda Uingereza kwa sababu ya Ufaulu wake mdogo kwenye Somo la lugha ya Kiingereza. kabla ya kwenda huko Nchini Uingereza kwa ajili ya Mafunzo yao ya Juu ya Kijeshi kwanza walipelekwa Nairobi Nchini Kenya na kisha Jinja Nchini Uganda kwaajili ya Mafunzo ya kawaida ya Kijeshi.

Mafunzo ya Kijeshi yaliyokuwa yakifanyika Nairobi na kisha Jinja Nchini Uganda yalihusisha pia Vijana kutoka Kenya na Uganda, ambapo wakati wakimalizia mafunzo kule Jinja ni watu nane (8) tu katika kundi zima ambao walichaguliwa kujiunga na masomo ya Juu ya Kijeshi ambapo watatu walitoka Kenya na Tanganyika alikuwa ni yeye na Nyirenda tu baada ya kuondolewa kwa Sarakikya.

MAFUNZONI, JASIRI AMEEN KASHMIRI ALIYEWEKA MSINGI.

Mzee Ameen na vijana wenziwe walipokelewa vizuri tu Nchini Uingereza, lakini Bodi ya Uchaguzi wa Jeshi la Uingereza iliwachagua yeye na kijana wa Kizungu kutoka Kenya moja kwa moja kwenda Chuoni Sandhusrt na wale wenzao waliobakia (akiwemo na Nyirenda) walipelekwa katika Chuo cha Mafunzo cha Makuruta cha Mons kabla ya kurudisha kujiunga na kina Ameen miezi sita (6) baadaye.

Mwezi Juni mwaka 1960 alimaliza mafunzo na kufaulu kuwa Askari Jeshi Luteni mwenye Nyota Mbili (Second Lieutenant) ambapo alikuwa mtu wa kwanza kufaulu chuoni hapo kutoka katika Nchi za Afrika Mashariki na Kati.

Mara baada ya kumaliza Mafunzo yake Ameen Kashmiri alirudi Tanganyika na kujiunga na kikosi Namba sita cha King's African Rifles katika Kambi ya Calito (sasa Lugalo).

KIKOSI CHA BENDERA, MZALENDO AMEEN KASHMIRI.

Mwaka 1961 Tanganyika ilipata Uhuru wake kutoka kwa Wakoloni wa Kiingereza, Usiku wa kuamkia tarehe 9 Desemba mwaka 1961 kulikuwa na Shamra shamra nyingi sana ikiwemo kitendo cha Mzee Nyirenda kuupandisha Mwenge wa Uhuru kwenda katika kilele cha Mlima Kilimanjaro na matukio mengine mengi sana ya kusisimua.

Mzee Ameen Kashmiri alikuwa katika Kikosi cha Bendera kwenye Sherehe za Uhuru zilizofanyika katika Uwanja wa Taifa (sasa Uwanja wa Uhuru) Jijini Dar es salaam asubuhi ya siku hiyo ya Uhuru. Ameen alibeba Bendera ya Uhuru ya Tanganyika (kama anavyoonekana pichani) ambayo ilipandishwa Juu siku hiyo huku askari mwenzie akiwa amebeba Bendera ya Wakoloni wa Kiingereza ambayo ilishushwa rasmi siku hiyo na Kiongozi wa Harakati za Uhuru wa Tanganyika Mwalimu Julius K Nyerere kuashiria Uhuru kamili wa Tanganyika.

MASHUHURI AMEEN KASHMIRI, MBEBA BENDERA YA MATUMAINI YETU.

Jukumu kubwa na zito la kubeba Bendera ya Tanganyika katika siku ile ya kukumbukwa linaonyesha weledi, kuaminiwa, ujemedari na uzalendo wake ambao haukuwa na mashaka kwa Taifa hili, tukio hilo ni kiashiria na kielelezo cha umuhimu na mchango wake katika Historia njema ya Tanganyika.

Yeye binafsi siku zote anasema hawezi kulisahau kabisa tukio hilo mpaka kufa kwake, kwake ni tukio lenye kubeba ufahari wa kitanzania, umashuhuri wa kizalendo na ujemedari wa uaminifu wa kitumishi kwa umma wa Watanzania. Heshima ambayo alipewa na wanawema wenziwe haina mithali kwake.

Tukio la Mzee Ameen Kashmiri kubeba bendera ile ya Matumaini ni jambo lenye kusisimua sana nyonyoni mwetu watanzania wote mpaka leo hii, kumbukumbu njema za tukio hilo kwa wale waliokuwepo siku hiyo ni jambo la kifahari na linarithisha Uzalendo na kuipenda Nchi kwa sisi Vijana wadogo wa Kitanzania ambao hatukuwepo wakati ule, ni tukio adimu lenye kumfanya Mzee Ameen Kashmiri kuwa Mtu Mashuhuri sana nyoyoni mwetu.

MAASI YA KIJESHI, USULI WA "AFRICANIZATION". 

Usiku wa kuamkia Januari 21, 1964, Jeshi la Tanganyika liliasi na kushikilia serikali kwa muda, tukio ambalo Baba wa taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, alilielezea kuwa ni “siku ya aibu sana kwa Taifa”. Wakati jeshi hilo likiasi siku hiyo hiyo, na saa hiyo hiyo, majeshi ya Kenya na Uganda nayo yaliasi kwa staili hiyo hiyo. Maasi yote ya nchi tatu hizo yalizimwa na majeshi ya Uingereza siku moja na wakati huo huo. Kwa Tanganyika, maasi haya yalitokea wiki moja tu baada ya mapinduzi ya umwagaji damu ya Zanzibar, Januari 12, 1964; na usiku huo wa maasi hayo, Kiongozi wa Mapinduzi ya Zanzibar “Field Marshal” John Gidion Okello, alikuwa na mazungumzo na Mwalimu Nyerere Ikulu, Dar es Salaam, katika hali ya kubadilishana mawazo juu ya hali ya Zanzibar ambapo Mwalimu, alimshauri Okello afanye kazi kwa imani na Rais Abeid Amani Karume. 

Mara baada ya Uhuru Tanganyika (sasa Tanzania bara) ilirithi Jeshi kutoka kwa Wakoloni wa Kiingereza lililokuwa likijulikana kama “Kings African Rifles” – (K. A. R) na baadaye kuitwa “Tanganyika Rifles” (TR). Katika kipindi kufuatia uhuru, ili kukidhi matarajio ya Watanganyika, zilitakiwa hatua za haraka kuhakikisha nafasi zote za juu serikalini na taasisi zake (likiwemo jeshi), zinashikwa na Wazalendo. Huu ni utamaduni uliokuwa umejengeka kwa nchi zote za Kiafrika zilizokuwa zikipata uhuru

Nyerere hakuwa na ujasiri wa kuchukua hatua haraka hivyo, kama pia ambavyo Waziri wake wa Mambo ya Ndani wa wakati huo, Clement George Kahama, hakuwa na ujasiri wa kuwatimua Waingereza katika nafasi za juu ndani ya Jeshi la Polisi. Yakaanza malumbano ndani ya Halmashauri Kuu (NEC) ya Chama Tawala, Tanganyika African National Union (TANU), kwamba Nyerere alikuwa anairudisha Tanganyika katika enzi za Ukoloni, na hivyo kwamba “uhuru” haukuwa na maana kwa Watanganyika kwa kushindwa kwake kuwapa vyeo Waafrika.

Ili kuepusha shari, na ili Chama kisifarakane, Mwalimu akaachia ngazi Januari 16, 1962 na kurejea kijijini kuimarisha Chama kama Mwenyekiti wa Taifa wa TANU na Rashid Kawawa akachukua Uwaziri Mkuu. Naye Oscar Kambona, ambaye wakati huo alikuwa Waziri wa Elimu, akawa Waziri wa Mambo ya Ndani badala ya George Kahama. Wote wawili hao wakaachiwa kazi ya kuwaondoa Wazungu katika vyeo walivyokuwa bado wanashikilia haraka bila visingizio.

Kazi ya kwanza ya Kambona ilikuwa ni kumtimua Kamishna wa Polisi Mwingereza, na kumteua Bwana Elangwa Shaidi kuchukua nafasi hiyo, lakini hakufanya mabadiliko kwa Jeshi (Tanganyika Rifles).

Zoezi hili la “Africanisation” lilifanywa kwa kasi ya kutisha kiasi cha kuishitua jamii ya Kimataifa. Desemba 1962, ulifanyika Uchaguzi Mkuu ambapo Mwalimu Nyerere alichaguliwa kuwa Rais Mtendaji wa kwanza. Kwa hiyo, Januari 1963, Mwalimu alirejea madarakani kama Rais wa kwanza wa Tanganyika na kusitisha mara moja zoezi la “Africanisation” na kuchochea hasira ya viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi nchini, ambao waliapa kutolala usingizi, wala kuupa nafasi uamuzi wa Mwalimu wa kusisitiza zoezi la kuwapa madaraka Watanganyika.

AMEEN KASHMIRI CHINI YA ULINZI, ASKARI WA KWANZA WA CHEO CHA JUU KUKAMATWA. 

Matata yalianza usiku wa Januari 20, kuamkia 21 usiku huo, siku ambayo Okello alikuwa na mazungumzo na Mwalimu, Ikulu usiku. Mzee Ameen Kashmir anaikumbuka sana siku hii kwa kuwa yeye ndiye Aliyekuwa Ofisa wa zamu wa wiki ile.

Saa 11 jioni alianza utaratibu wa kichunguza (routine inspection) kwa kuanzia Eneo la Ikulu na kisha kupita katika maeneo yote nyeti ya Nchi ambapo kila kitu kilionekana kuwa shwari na hakukuwa na vishiria vyovyote vya uwepo wa tukio la Jeshi kuasi.

Mara baada ya ukaguzi huo kwenye maeneo nyeti ya Nchi aliamua kurudi katika kambi kuu ya Colito ambapo alishangazwa sana na hali ya kukuta taa zote za kambi zikiwa zimezimwa jambo ambalo halikuwa la kawaida lakini aliondoa hisia mbaya na kuhisi labda kulikuwa na matatizo ya umeme kambini hapo.

Wakati alipokuwa amevalia Sare zake maridadi za Jeshi alijitambulisha kama Askari wa Zamu wa Jeshi wa wiki, ambapo mara baada ya Geti kuu kufunguliwa na yeye kuingia alishangaa anawekwa Chini ya Ulinzi na Askari wenzie jambo ambalo halikumshangaza kwa kuhisi ni utani tu.

Baada ya muda aligundua kuwa kilichokuwa kinatokea si utani tena na ni uasi kamili wa Jeshi ambapo yeye alikuwa Afisa Mkuu wa Kwanza kuwekwa ndani, kisha king'ora kilipigwa kambini hapo kuashiria kutakiwa kwa askari wote kukusanyika katika uwanja, ambapo wasaa huo ndiyo ulitumika kuwaweka chini ya ulinzi Askari wengine wa kizungu waliokuwa na vyeo vya juu.

Lakini ilipofika saa 7:50 alfajiri, Januari 21, Mkuu wa Kikosi cha kwanza cha TR, Brigedia Patrick Sholto Douglas, aliamshwa nyumbani kwake na sauti ya baruji (buggle) na ving’ora, karibu na kambi ya Jeshi ya Colito (sasa Lugalo Barracks).

Alipotoka nje, aliona askari wake 12 wakikamatwa na wenzao wenye silaha na kutiwa mahabusu. Ndipo alipofahamu kwamba, nusu ya askari 800 wa Kikosi hicho walikuwa wameasi. Aliweza kutoroka yeye na familia yake hadi katikati ya jiji, akaiacha familia kwa Balozi wa Australia, kisha akakakimbilia kwa Afisa mwenzake, eneo la Oyster Bay na kutumia wasaa huo kumjulisha kwa Simu Waziri Kawawa juu ya kinachoendelea. Mzee Ameen anawataja askari wengine wa cheo cha juu waliofanikiwa kutoroka kuwa ni Meja Maricadi pamoja na Mkuu mwengine mmoja ambaye amemsahau jina ambaye alijificha kwenye mapori ya Kunduchi.

KASHMIRI UGHAIBUNI, HUZUNI YA KUKUMBUKA NYUMBANI.

Akiwa amefungiwa katika Mahabusu ya Jeshi katika kambi ya Colito, Mzee Kashmiri anakumbuka sana kumuona Waziri Kambona akifanya juhudi mbalimbali za kupoza na kutuliza maasi yale, Kama moja ya matakwa ya Askari wale waasi ilimbidi Kambona akubali kuwasafirisha mpaka Nairobi Viongozi wote wa Jeshi ambao walitiwa ndani (akiwemo Kashmiri) na wale walioasi bila kipingamizi ambapo baadaye walisafirishwa kwenda Uingereza.

Anakumbuka vyema wakati akiwa ndani ya Gari wakitaka kusafirishwa namna mwenzie Nyirenda alivyoulizwa "Wewe Mswahili nawe unakwenda wapi?", jambo ambalo lilimhuzunisha sana yeye kwa kuona ameachwa kwa kuwa yeye hakuwa Mswahili kama Nyirenda kwa kudhaniwa naye ni mzungu tu kwa sababu ya rangi yake.

Maasi yale baadaye yalizimwa kwa msaada mkubwa wa Majeshi ya Kikoloni ya Kiingereza na baadaye Kikosi cha Ulinzi cha Jeshi la Nigeria chini ya Generali Ochukwu kilikuja kuchukua nafasi ya Jeshi la Uingereza, wakati huo Kashmiri alikuwa tayari yuko Uingereza ambapo aliishi kwa muda wa miezi minne ya Upweke na kutokupata mawasiliano yoyote na Serikali ya Taifa lake. Waingereza walijaribu kumpa Ajira Mzee Kashmiri lakini aliwakatalia na kuwaambia kuwa yeye ni Mwanajeshi wa Tanganyika na hivyo hawezi kufanya kazi nyengine yoyote.

Mwezi April mwaka huo (1964) alipata simu ya maandishi (Telefax) kutoka kwa Waziri Mkuu wa Tanganyika, Mzee Rashid Mfaume Kawawa ikimtaka arudi nyumbani jambo ambalo lilimpa faraja kubwa sana. Kabla ya Maasi yale ya Jeshi alikuwa ameomba ruhusa Jeshini ya kwenda kusoma Kozi Fupi ya Utawala wa Jeshi hivyo aliomba kutumia muda ule ambao yuko kule Uingereza kusoma kozi hiyo ambayo aliimaliza Mwezi Julai mwaka huo huo kisha akarudi nyumbani ambapo wakati huo haikuwa Tanganyika tena bali Tanzania.

JWTZ, FAHARI YA WATANZANIA.

Mara baada kurudi Nchini Mzee Ameen Kashmiri alipewa Cheo cha Ukuu wa Utawala na Uhandisi ambapo alifanya kazi nzito na ya kizalendo ya kujenga Jeshi Imara la Wananchi wa Tanzania kwa muda wa miaka minane.

Ilipofika Mwaka 1974 Mzee Kashmiri alikuwa amemaliza kazi yake ya kujenga Jeshi lenye Askari Imara na wakakamavu zaidi ya 30,000 kutoka kati ya wale 400 waliobakishwa mara baada ya kuvunjwa kwa Tanganyika Rifles, ambapo anaelezea namna ambavyo waliweza kusajili askari zaidi ya 2,000 kwa kila mwaka mpaka kufikia kiwango hicho, ambapo alichangia kulijenga Jeshi hilo kuwa imara, lenye nidhamu na lililo madhubuti zaidi katika Ukanda wote wa Afrika Mashariki.

MTUMISHI WA UMMA ASIYECHOKA.

Mwezi Januari mwaka 1974 Mzee Kashmiri alistaafu kwa heshima zote kutoka Jeshini na kuwaachia nafasi vijana wapya ambao alishiriki kuwaunda washike nafasi yake ili kuliendeleza na kuliimarisha zaidi Jeshi kutoka pale yeye alipoishia.

Kama vile walivyo wazalendo wengine wote kustaafu hakuna maana kuwa hawezi tena kulitumika Taifa lake, alirudi tena kwenye utumishi wa umma mara baada ya kuombwa na Rais Nyerere kuwa Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Sukari (SUDECO), kazi ambayo aliifanya kwa muda wa Miezi Miwili mpaka alipoondoka kwenye Ukuu huo mwaka 1976 ambapo alirudi tena Jeshini wakati wa Vita vya Kagera. 

RAFIKI WA KWELI NA MZALENDO ANAYELIPENDA TAIFA LAKE.

Mzee Ameen Kashmiri yu hai, japo siku hizi amekuwa mtu mzima sana na akijishughulisha zaidi na shughuli zake binafsi katika sekta ya uchimbaji wa madini pamoja na kuwa karibu na Familia yake.

Wakati wa Kilele cha Sherehe za Mbio za Mwenge wa Uhuru katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam mwaka 2011 Mzee Kashmiri alikuwa mmoja wa wahudhuriaji uwanjani hapo. Rais Jakaya Mrisho Kikwete alipata nafasi ya kuzungumza naye na alimpongeza na kummwagia sifa kwa kuwa mmoja wa mashujaa wachache wa Uhuru walio hai na kuvutiwa naye kwa kulipenda Taifa lake siku zote.

Wakati wa Maadhimisho ya Miaka Hamsini (50) ya Uhuru wa Tanzania Bara (Tanganyika) Familia ya Marehemu Brigedia Alex Gwebe Nyirenda (ambayo Mzee Kashmiri ndiye Baba Mlezi wa Familia hiyo) iliandaa tukio lililoitwa GWEMBE NYIRENDA MEMORIAL KILIMANJARO EXPEDITION ambalo limepangwa kufanyika kila Mwaka, tukio hilo likihusisha Upandaji wa Kuchochea Utalii na kuutangaza Mlima wa Kilimanjaro kwa kukumbuka Tukio la Kuupandisha Mwenge wa Uhuru Mlimani hapo lililofanywa na Nyirenda.

Mzee Ameen Kashmiri, Kaka na Dada Alex Foti Gwebe Nyirenda na Tima Gwebe Nyirenda (WATOTO WA MZEE NYIRENDA), Mobeen Kashmiri (MTOTO WA MZEE KASHMIRI) waliwaongoza ndugu jamaa na marafiki katika tukio hilo adhimu la kumkumbuka rafikiye Nyirenda.

Mzee Kasmiri ni mtu mwenye Utu, Upendo na kujali kulikopita mipaka, miaka yote amekuwa baba na mlezi mwema wa watoto hao wa Rafikiye wa kweli Nyirenda, kiasi amewafariji na kuwafanya wajihisi kama vile baba yao yu hai bado. Yote hayo yakionyesha sura halisi ya wema na umashuhuri wa Mzee wetu Ameen Kashmiri.

Chanzo: ukurasa wa facebook ‘watanzania mashuhuri’

John Terry kukosa mechi nne na kulimwa fidia ya Pauni 220,000 za Uingereza kwa kosa la utovu wa nidhani uliofananishwa na ubaguzi wa rangi dhidi ya wtu weusi katika soka.


John Terry ameadhibiwa na chama cha kandanda cha England, FA, asicheze mechi nne, na vile vile alipe faini ya pauni 220,000, kutokana na matamshi ya ubaguzi wa rangi dhidi ya mchezaji wa QPR, Anton Ferdinand. 

Chama cha FA kilithibitisha Terry alifanya makosa hayo, baada ya kusikiliza kesi dhidi yake kwa kipindi cha siku nne. 

Msemaji wa John Terry alisema mchezaji huyo "alisikitishwa" na hatua ya FA, kwa kuamua tofauti, kinyume na mahakama, ambayo awali ilisema hana makosa. 

Mwezi Julai, mahakama ya Westminster mjini London ilipitisha uamuzi kwamba mchezaji huyo, mwenye umri wa miaka 31, hakufanya kosa hilo, la kutumia matamshi ya ubaguzi wa rangi dhidi ya Ferdinand. 

Hata hivyo wengi watajiuliza kwa nini adhabu dhidi ya Terry ni nyepesi mno, ikilinganishwa na ile iliyopitishwa dhdi ya mchezaji wa Liverpool, Luis Suarez mwaka jana. 

Terry ana muda wa siku 14 kukata rufaa dhidi ya uamuzi huo, mara tu atakapopokea maelezo ya adhabu hiyo kupitia maandishi. 

Adhabu hiyo haitatekelezwa hadi Terry atakapopata nafasi ya kuamua atafanya nini. 

Taarifa kutoka klabu yake ya Chelsea iliongezea: "Klabu ya Chelsea inafahamu vyema uamuzi uliopitishwa, na inaheshimu uamuzi huo uliotolewa leo na chama cha FA kumhusu John Terry."

Chanzo: BBC Swahili.