Tuesday, January 1, 2013

Seneta yapitisha mswada wa Rais Obama...


Rais wa Marekani Barrack Obama, amewataka wabunge wa bunge la wawakilishi kupitisha maazimio yaliopitishwa na bunge la Senate kuhusu sera mpya ya uchumi bila kusita.
Bwana Obama, amesema kuwa makubaliano hayo yanawaokoa asili mia sabini ya Wamarekani dhidi kupandishiwa ushuru na pia yataimarisha uchumi uchumi waa taifa hilo.
Rais Obama, amesema kuwa kwa mara ya kwanza wanaomiliki mabilioni na mamilioni ya fedha watalazimika kulipa ushuru unaohitajika kwa mara ya kwanza kwa zaidi ya miaka ishirini iliyopita.
Wabunge wa chama cha Republican, wamesema kuwa watahitaji muda zaidi kusoma mapendekezo hayo.
Hata hivyo wantarajiwa kupiga kura baadaye hivi leo.
Chanzo: BBC Swahili

No comments:

Post a Comment