Saturday, January 19, 2013

Unamjua Gabriel De Santos Mario Barbosa?


Mshambuliaji mwenye mashuti makali kutoka nchini Brazil Gabriel Barbosa leo ataonyesha makali yake na kuwadhihirishia wapenzi wa soka Tanzania kuwa hajakuja Tanzania kuonyesha mavazi. Barbosa atakuwa Mbrazil wa kwanza kucheza soka katika ligi kuu ya Tanzania tangu nchi hii kupata uhuru. Na Coastal Union itaandika historia hiyo siku ya tarehe 26 katika uwanja wa Mkwakwani Tanga wakati itakapofungua dimba la mzunguko wa pili wa ligi kuu dhidi ya Mgambo FC ya Handeni Tanga.

No comments:

Post a Comment