Thursday, February 28, 2013

Warsha ya wadau wa kilimo katika picha...

 Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bw Sazi Salula akifungua Warsha ya Wadau ya Kupitia na Kujidili Muongozo wa Kitaifa wa Mabadiliko ya Tabianchi juu ya Wakulima na Wafugaji Nchini Kulia Mkurugenzi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais Dk Julias Nihgu Warsha imefanyika kwenye Hotel ya Palmtree Village Bagamoyo.
 
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bw Sazi Salula akimsikiliza jambo Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Mazingira Ofisi ya Makamu wa Raisi Bw Richad Muyungi mara Baada ya Ufunguzi wa Warsha hiyo jana.y



 Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bw Sazi Salula akiwa katika Picha ya Pamoja na Washiriki wa Warsha ya Kupitia na Kujadili Muongozo wa Kitaifa wa Mabadiliko ya tabianchi juu ya Wakulima na Wafugaji Nchini.



Mkurugenzi Msaidizi Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais Bw Richad Muyungi akimwambia jambo Afisa Mazingira Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bw Daniel Nkondola Mara baada ya Ufunguzi wa Warsha hiyo jana.



 [Picha zote na Ali Meja Ofisi ya makamu wa Rais]


Monica Sapanjo- Ofisi ya Makamu wa Rais

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bwana Sazi Salula amewataka wadau wa sekta ya kilimo  nchini hasa wakulima wadogo wadogo  kujitahidi  kufahamu athari  na  changamoto mbalilmbali zinazoikabili sekta hii kutokana na athari za  mabadiliko ya tabianchi. Alitoa rai hiyo wakati akifungua warsha ya siku mbili  ya kitaifa ikihusisha wadau mbalimbali kuandaa  mwongozo wa taarifa za kuhimili mabadiliko ya tabianchi kwa  jamii za wakulima na wafugaji nchini.

Aliwaomba wajumbe wa warsha hiyo kutoa maoni yao ya kitaalamu ili kuhakikisha   mwongozo unakuwa tayari kwa matumizi ya jamii za wakulima na wafugaji nchini mapema iwezekanavyo hasa ikinzingatiwa kuwa athari sasa zimeanza kuwa kubwa sana. Alisema  mwongozo huu  ni muendelezo wa juhudi za serikali katika kushughulikia masuala ya mabadiliko ya tabianchi. "Juhudi hizi zitaiwezesha nchi kuhimili atahari za mabadiliko haya na kuchangia juhudi za kimataifa za kupunguza gesijoto" alisema Bwana Salula.

Warsha hiyo ya siku mbili imeandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais kwa ufadhili wa Serikali ya Japana kupitia UNDP,  kwa ajili ya kujadili mwomgozo huu wa kusaidia wakulima na wafugaji wadogo wadogo kuhimili  mabadiliko ya tabianchi. Washirki wa warsha hiyo  ni kutoka kwenye taasisi  mbalimbali  ikiwa ni pamoja na  Ofisi ya Waziri mkuu, Wizara ya maji, Wizara ya habari na michezo, Wizara ya kilimo na baraza la Mazingira la Taifa(NEMC, Jumuia ya Wakulima Tanzanaia na asasi mbalimbali zisizo za kiserikali.

Madhumuni ya mwongozo huu ni kuwasaidia wakulima na wafugaji  kuendeleza shughuli zao za ufugaji na ukulima katika maeneora ambayo yamebadilika kutokana na mabadiliko ya tabianchi.



Soma hoja ya John Mnyika kuhusu umeme...




Nchi imeingia tena katika mgawo wa umeme kinyume na ahadi iliyotolewa na Waziri wa Nishati na Madini Prof Sospeter Muhongo bungeni tarehe 28 Julai 2012. Hali hiyo ni matokeo ya Serikali kutozingatia tahadhari niliyoitoa bungeni tarehe 27 Julai 2012 kwa niaba ya Kambi Rasmi ya Upinzani na kwa nyakati mbalimbali kwa nafasi yangu ya Waziri Kivuli wa Nishati na Madini juu ya hali tete iliyotarajiwa kuwepo na hatua zinazopaswa kuchukuliwa katika utekelezaji wa mpango wa dharura wa umeme.


Ikiwa ni sehemu ya wajibu wa kibunge wa kuisimamia Serikali nawataka viongozi na watendaji wa Wizara ya Nishati na Madini na Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) kuacha kuficha hali ya mambo na kuwaeleza ukweli wananchi kuhusu mgawo wa umeme uliojitokeza na hatua za haraka zinazochukuliwa kurekebisha hali hiyo. 

Iwapo Wizara na TANESCO hawatatoa matangazo ya ukweli kwa wananchi, kwa nafasi yangu ya Waziri Kivuli wa Nishati na Madini nitaeleza vyanzo vya mgawo wa umeme uliojitokeza ili hatua ziweze kuchukuliwa wakati huu ambapo wajumbe wa kamati ya nishati na madini wenye wajibu wa kuisimamia Serikali kwa niaba ya Bunge katika sekta hizo nyeti hawajateuliwa.


Aidha, pamoja na kutoa maelezo kuhusu mgawo wa umeme, Wizara ya Nishati na Madini na TANESCO watumie nafasi hiyo pia kueleza hatua zilizochukuliwa kuhusu ukaguzi wa awamu ya pili kuhusu tuhuma za ufisadi katika ununuzi wa vifaa na uzalishaji wa umeme wa dharura ikiwemo kuhusu mafuta mazito ya kuendeshea mitambo ya kufua umeme. 

Ikumbukwe kwamba mwanzoni mwezi Agosti 2012 Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (NAOT) iliunda timu ya wakaguzi kufanya ukaguzi maalum wa hesabu za Shirika la Umeme (TANESCO) kufuatia tuhuma za ubadhirifu wa fedha za umma zilitajwa bungeni na Waziri Kivuli wa Nishati na Madini katika maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani tarehe 27 Julai 2012 na Waziri wa Nishati na Madini wakati wa majumuisho ya hoja ya Serikali tarehe 28 Julai 2012. 

Wizara ya Nishati na Madini na TANESCO waeleze pia hatua iliyofikiwa kuhusu uchunguzi mwingine uliofanywa na Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) kuanzia mwezi Agosti 2012 wa mchakato wa ununuzi wa mafuta mazito ya kuendeshea mitambo ya kufua umeme wa dharura kutokana na tuhuma mbalimbali zilizotolewa bungeni kuhusu ununuzi huo suala ambalo Kambi Rasmi ya Upinzani ilitaka pia tarehe 27 Julai 2012 liundiwe kamati teule ya Bunge ili uchunguzi wa kina uweze kufanyika. 


Wenu katika uwakilishi wa wananchi, 

John Mnyika (Mb)
Waziri Kivuli wa Nishati na Madini 

27 Februari 2013

Rwanda yateua Mtanzania, kuwa Waziri wa miundombinu wa nchi hiyo.


RAIS Paul Kagame wa Rwanda amemteua Mtanzania, Profesa Silas Rwakabamba kuwa Waziri wa Miundombinu wa nchi hiyo katika mabadiliko ya Baraza la Mawaziri yaliyofanyika Jumatatu iliyopita.

Kabla ya uteuzi huo, Profesa Rwakabamba alikuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Rwanda. Ni mmoja wa mawaziri wanaoingiza sura mpya katika Baraza la Rais Kagame ambalo amelifanyia mabadiliko kwa kuunda wizara nyingine mpya.

Sura nyingine mpya katika Baraza hilo ambalo liliapishwa juzi Ikulu ya Rwanda ni pamoja na Seraphine Mukantabana (Wakimbizi na Menejimenti ya Maafa) na Oda Gasinzigwa (Ofisi ya Waziri Mkuu- Familia na Jinsia).

Akizungumza kwa simu na mwandishi wetu jana, mdogo wa Profesa Rwakabamba, Timothy Rwamushaija anayeishi Dar es Salaam, alisema ndugu yake alizaliwa katika Kijiji cha Bushagara, Wilaya ya Muleba mkoani Kagera.

Alisema Profesa Rwakabamba alikuwa Mtanzania aliyeamua kuchukua uraia wa Rwanda na wote baba yao ni Mzee Titus Rwamushaija... “Huyu ni kaka yangu wa tumbo moja na kwa kweli tumefurahi sana kwa mafanikio yake sisi kama wanafamilia.”

Naibu Makamu Mkuu - Taaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM), Profesa Makenya Maboko alisema Profesa Rwakabamba alifanya kazi katika chuo hicho na aliondoka akiwa Mkuu wa Kitivo cha Uhandisi.

“Aliondoka wakati Kagame alipoingia madarakani na alikwenda kuongoza Taasisi ya Teknolojia ya Kigali (KIST) kabla ya kwenda katika Chuo Kikuu cha Kigali,” alisema Profesa Maboko.

Msomi huyo alikwenda Rwanda mwaka 1997, baada ya kuombwa na Rais Kagame ambaye alikwenda UDSM kuwaomba baadhi ya wahadhiri kwenda Kigali kufungua chuo kikuu katika taifa lake baada ya kumalizika vita ya wenyewe kwa wenyewe mwaka 1994.

Profesa Rwakabamba alikuwa Mkuu wa kwanza wa KIST na kukifanya kuwa miongoni mwa vyuo bora barani Afrika kwa masuala ya teknolojia jambo lililomfurahisha Rais Kagame.

Baada ya mafanikio hayo, Rais Kagame alimteua kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Rwanda, Butare ambako pia alijizolea sifa baada ya kusimamia vyema ujenzi wa mabweni kwa wingi na kiongozi huyo alimtunukia uraia wa nchi hiyo kama zawadi.

Hata hivyo, Profesa Rwakabamba atakuwa amelazimika kuukana uraia wa Tanzania kwa kuwa katiba ya nchi hairuhusu uraia wa nchi mbili.
Profesa Rwakabamba alipata elimu ya msingi huko Muleba na akajiunga na Shule ya Sekondari ya Ihungo.

Baada ya hapo, alijiunga na Chuo Kikuu cha Leeds, Uingereza na kupata Shahada ya Uhandisi mwaka 1971 na 1975 alipata Shahada ya Uzamivu katika fani hiyohiyo.
Alirejea Tanzania na kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika Kitivo cha Uhandisi ambacho kilikuwa kimeanza mwaka huo.
Alipata nafasi mbalimbali katika muda mfupi aliokuwa hapo hadi alipotunukiwa kuwa Profesa mwaka 1981.

Mwaka 1985, Profesa Rwakabamba aliteuliwa kuwa Mkurugenzi Mwanzilishi wa Mafunzo katika Kituo cha Afrika cha Uhandisi Ubunifu na Uzalishaji (ARCEDEM), kinachodhaminiwa na Umoja wa Mataifa (UN) kilichopo Nigeria. Baada ya kazi hiyo, ndipo alipokwenda Kigali.

Tangu 1975, Profesa Rwakabamba amekuwa mjumbe wa bodi mbalimbali kitaifa na kimataifa ikiwa ni pamoja na kuwa Bodi ya Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (Unesco) na pia Kiongozi Mwandamizi wa Muungano wa Vyuo vya Kimataifa (IAUP).
 Chanzo: Mwananchi.

Soma hotuba ya mwisho ya Papa Benedict 16



Venerable Brothers in the Episcopate and in the Priesthood!
Distinguished Authorities!
Dear brothers and sisters!
Thank you for coming in such large numbers to this last General Audience of my pontificate.
Like the Apostle Paul in the biblical text that we have heard, I feel in my heart the paramount duty to thank God, who guides the Church and makes her grow: who sows His Word and thus nourishes the faith in His people. At this moment my spirit reaches out to embrace the whole Church throughout the world, and I thank God for the “news” that in these years of Petrine ministry I have been able to receive regarding the faith in the Lord Jesus Christ, and the charity that circulates in the body of the Church – charity that makes the Church to live in love – and of the hope that opens for us the way towards the fullness of life, and directs us towards the heavenly homeland.


I feel I [ought to] carry everyone in prayer, in a present that is God’s, where I recall every meeting, every voyage, every pastoral visit. I gather everyone and every thing in prayerful recollection, in order to entrust them to the Lord: in order that we might have full knowledge of His will, with every wisdom and spiritual understanding, and in order that we might comport ourselves in a manner that is worthy of Him, of His, bearing fruit in every good work (cf. Col 1:9-10).

At this time, I have within myself a great trust [in God], because I know – all of us know – that the Gospel’s word of truth is the strength of the Church: it is her life. The Gospel purifies and renews: it bears fruit wherever the community of believers hears and welcomes the grace of God in truth and lives in charity. This is my faith, this is my joy.

When, almost eight years ago, on April 19th, [2005], I agreed to take on the Petrine ministry, I held steadfast in this certainty, which has always accompanied me. In that moment, as I have already stated several times, the words that resounded in my heart were: “Lord, what do you ask of me? It a great weight that You place on my shoulders, but, if You ask me, at your word I will throw out the nets, sure that you will guide me” – and the Lord really has guided me. He has been close to me: daily could I feel His presence. [These years] have been a stretch of the Church’s pilgrim way, which has seen moments joy and light, but also difficult moments. I have felt like St. Peter with the Apostles in the boat on the Sea of Galilee: the Lord has given us many days of sunshine and gentle breeze, days in which the catch has been abundant; [then] there have been times when the seas were rough and the wind against us, as in the whole history of the Church it has ever been - and the Lord seemed to sleep. Nevertheless, I always knew that the Lord is in the barque, that the barque of the Church is not mine, not ours, but His - and He shall not let her sink. It is He, who steers her: to be sure, he does so also through men of His choosing, for He desired that it be so. This was and is a certainty that nothing can tarnish. It is for this reason, that today my heart is filled with gratitude to God, for never did He leave me or the Church without His consolation, His light, His love.

We are in the Year of Faith, which I desired in order to strengthen our own faith in God in a context that seems to push faith more and more toward the margins of life. I would like to invite everyone to renew firm trust in the Lord. I would like that we all, entrust ourselves as children to the arms of God, and rest assured that those arms support us and us to walk every day, even in times of struggle. I would like everyone to feel loved by the God who gave His Son for us and showed us His boundless love. I want everyone to feel the joy of being Christian. In a beautiful prayer to be recited daily in the morning says, “I adore you, my God, I love you with all my heart. I thank You for having created me, for having made me a Christian.” Yes, we are happy for the gift of faith: it is the most precious good, that no one can take from us! Let us thank God for this every day, with prayer and with a coherent Christian life. God loves us, but He also expects that we love Him!

At this time, however, it is not only God, whom I desire to thank. A Pope is not alone in guiding St. Peter’s barque, even if it is his first responsibility – and I have not ever felt myself alone in bearing either the joys or the weight of the Petrine ministry. The Lord has placed next to me many people, who, with generosity and love for God and the Church, have helped me and been close to me. First of all you, dear Brother Cardinals: your wisdom, your counsels, your friendship, were all precious to me. My collaborators, starting with my Secretary of State, who accompanied me faithfully over the years, the Secretariat of State and the whole Roman Curia, as well as all those who, in various areas, give their service to the Holy See: the many faces which never emerge, but remain in the background, in silence, in their daily commitment, with a spirit of faith and humility. They have been for me a sure and reliable support. A special thought [goes] to the Church of Rome, my diocese! I can not forget the Brothers in the Episcopate and in the Priesthood, the consecrated persons and the entire People of God: in pastoral visits, in public encounters, at Audiences, in traveling, I have always received great care and deep affection; I also loved each and every one, without exception, with that pastoral charity which is the heart of every shepherd, especially the Bishop of Rome, the Successor of the Apostle Peter. Every day I carried each of you in my prayers, with the father's heart.

I wish my greetings and my thanks to reach everyone: the heart of a Pope expands to [embrace] the whole world. I would like to express my gratitude to the Diplomatic Corps accredited to the Holy See, which makes present the great family of nations. Here I also think of all those who work for good communication, whom I thank for their important service.

At this point I would like to offer heartfelt thanks to all the many people throughout the whole world, who, in recent weeks have sent me moving tokens of concern, friendship and prayer. Yes, the Pope is never alone: now I experience this [truth] again in a way so great as to touch my very heart. The Pope belongs to everyone, and so many people feel very close to him. It’s true that I receive letters from the world's greatest figures - from the Heads of State, religious leaders, representatives of the world of culture and so on. I also receive many letters from ordinary people who write to me simply from their heart and let me feel their affection, which is born of our being together in Christ Jesus, in the Church. These people do not write me as one might write, for example, to a prince or a great figure one does not know. They write as brothers and sisters, sons and daughters, with the sense of very affectionate family ties. Here, one can touch what the Church is – not an organization, not an association for religious or humanitarian purposes, but a living body, a community of brothers and sisters in the Body of Jesus Christ, who unites us all. To experience the Church in this way and almost be able to touch with one’s hands the power of His truth and His love, is a source of joy, in a time in which many speak of its decline.

In recent months, I felt that my strength had decreased, and I asked God with insistence in prayer to enlighten me with His light to make me take the right decision – not for my sake, but for the good of the Church. I have taken this step in full awareness of its severity and also its novelty, but with a deep peace of mind. Loving the Church also means having the courage to make difficult, trying choices, having ever before oneself the good of the Church and not one’s own.

Here allow me to return once again to April 19, 2005. The gravity of the decision was precisely in the fact that from that moment on I was committed always and forever by the Lord. Always – he, who assumes the Petrine ministry no longer has any privacy. He belongs always and totally to everyone, to the whole Church. His life is, so to speak, totally deprived of the private sphere. I have felt, and I feel even in this very moment, that one receives one’s life precisely when he offers it as a gift. I said before that many people who love the Lord also love the Successor of Saint Peter and are fond of him, that the Pope has truly brothers and sisters, sons and daughters all over the world, and that he feels safe in the embrace of their communion, because he no longer belongs to himself, but he belongs to all and all are truly his own.

The “always” is also a “forever” - there is no returning to private life. My decision to forgo the exercise of active ministry, does not revoke this. I do not return to private life, to a life of travel, meetings, receptions, conferences and so on. I do not abandon the cross, but remain in a new way near to the Crucified Lord. I no longer wield the power of the office for the government of the Church, but in the service of prayer I remain, so to speak, within St. Peter’s bounds. St. Benedict, whose name I bear as Pope, shall be a great example in this for me. He showed us the way to a life which, active or passive, belongs wholly to the work of God.

I thank each and every one of you for the respect and understanding with which you have welcomed this important decision. I continue to accompany the Church on her way through prayer and reflection, with the dedication to the Lord and to His Bride, which I have hitherto tried to live daily and that I would live forever. I ask you to remember me before God, and above all to pray for the Cardinals, who are called to so important a task, and for the new Successor of Peter, that the Lord might accompany him with the light and the power of His Spirit.

Let us invoke the maternal intercession of Mary, Mother of God and of the Church, that she might accompany each of us and the whole ecclesial community: to her we entrust ourselves, with deep trust.
Dear friends! God guides His Church, maintains her always, and especially in difficult times. Let us never lose this vision of faith, which is the only true vision of the way of the Church and the world. In our heart, in the heart of each of you, let there be always the joyous certainty that the Lord is near, that He does not abandon us, that He is near to us and that He surrounds us with His love. 

Thank you!

Tuesday, February 26, 2013

Hizi ndizo sababu za kufungiwa Radio Imani na Radio Kwa Neema...


KAMATI ya Maadili ya Utangazaji nchini imevifungia vituo viwili vya radio pamoja na kukipiga faini ya Sh mil 5, kituo cha Clouds FM kutokana na kukiuka maadili ya utangazaji.

Vituo hivyo viwili vya redio ambavyo vyote kwa pamoja vimefungiwa kutorusha matangazo yake kuanzia leo kwa miezi sita ni pamoja na Imani FM cha Morogoro na  Kwa-Neema FM kilichopo mkoani Mwanza.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Walter Bgoya alisema Kituo cha Clouds FM kimetakiwa kufuta kipindi chake cha Jicho la Ng'ombe mara moja pamoja na kulipa faini ya sh. milioni 5.
Akifafanua zaidi Makamu Mwenyekiti huyo alisema vituo vya Imani FM na Kwa-Neema vimefungiwa kwa kosa la kufanya kazi zao kwa uchochezi jambo ambalo ni kinyume cha maadili ya tasnia ya utangazaji. Kituo cha Clouds FM kimetakiwa kutoanzisha kipengele (segment) nyingine inayofanana na Jicho la Ng'ombe iliyo katika kipindi chao cha asubuhi cha ‘Power breakfast’.

Kituo cha Imani FM kinadaiwa kufanya uchochezi kwa wananchi juu ya suala la sensa ya watu na makazi huku kile cha Kwa-Neema kufanya uchochezi juu ya mgogoro wa uchinjaji wanyama kwa Waislamu na Wakristu mkoani Geita.

Hata hivyo Kamati ya Maadili imeweka mlango wazi kwa vituo hivyo kukata rufaa endapo havikuridhika na adhabu vilivyo pewa kutokana na makosa vinao daiwa 
kufanya.
Kamati Imevitaka vyombo vyote vya habari kufanya kazi kwa kuzingatia Kanuni Sheria na maadili ya tasnia hiyo ili kuepuka kuzua migogoro kwa wananchi ambao wamekuwa wakiviamini vituo hivyo.
Hata hivyo mara baada ya ujumbe wa kamati hiyo kumaliza kusoma adhabu hizo kwa waandishi wa habari haukuruhusu maswali kwa waandishi wa habari, hivyo waandishi kubaki wameduwaa.
Akizungumza kwa njia ya simu mkurugenzi wa Clouds FM Ruge Mutahaba alisema haoni tatizo kwa viongozi hao kufikia hatua hiyo kwani wanafanya kazi yao, lakini kwakuwa wamepewa nafasi ya kukata rufaa watajipanga na kuenda kuwaelewesha maana na umuhimu wa waliyokuwa wakiyarusha katika sehemu (segment) ya jicho la ngombe iliyo katika kipindi chao cha asubuhi.
Sababu za kufungiwa:
- Kwa Neema FM Mwanza: Sababu ni kushabikia maswala ya uchinjaji Mwanza
- Radio Iman FM Morogoro: Kushabikia watu kutoshiriki Sensa 2012
- Clouds FM: Kushabikia ushoga & kuendesha kipindi kisichofuata maadili (Jicho la Ng’ombe)
kidojembe@gmail.com
26 Feb,2013
Dar es Salaam, Tanzania.


Monday, February 25, 2013

Soma nafasi ya tatu ya makala ya mwanajeshi aliemuua Osama Bin Laden.



MAREKANI inaamini kuwa vita vya kukabiliana na ugaidi vimepata mafanikio baada ya kuuawa kwa kiongozi wa kundi la Al-Qaeda, Osama bin Laden aliyeuawa Mosi, 2011 nchini Pakistan.
Hivi karibuni askari aliyefyatua risasi na kumuua kiongozi huyo alifanya mahojiano na mwandishi mmoja wa habari kuelezea namna operesheni hiyo ilivyofanikiwa.
Katika mfululizo wa simulizi hiyo leo mwandishi George Njogopa anapitia sehemu ya mwisho ambayo inamulika upande wa maisha yake binafsi.
Kulikuwa na furaha na shangwe kila kona ya Marekani na duniani kote. Mhalifu wa kimataifa alikuwa ameondoshwa kwenye uso wa dunia.
Askari aliyefyatua risasi na kumaliza uhai wa Osama alikuwa tayari amerejea nyumbani.
Rais Barack Obama aliingia kwenye rekodi mpya kwa kuwa kiongozi aliyefanikisha kuangusha ngome muhimu ya mtandao wa Al-Qaeda.
Baadhi ya askari wa Marekani waliopiga kambi katika mji wa Jalalabad nchini Pakistan waliambatana na askari mlenga shabaha kurejea nyumbani.
Askari huyo anasema kuwa, “Tulivyomaliza operesheni yetu tukarejea nyumbani kuendelea na majukumu mengine. Nakumbuka nilivyoondoka Jalalabad nilirejea moja kwa moja kwenye kituo cha vikosi vya majini na kuendelea na shughuli nilizopangiwa.”
Askari huyu ambaye ndiye aliyekuwa mtu wa mwisho kumwona Osama wakati akiwa hai kabla hajammiminia risasi mbili za usoni amesema sasa anaishi maisha ya upweke tofauti na miaka ya nyuma.
Anasema kuwa wakati akiwa katika operesheni nchini Pakistan mkewe pamoja na watoto wake waliishi maisha ya mahangaiko na  wakati mwingine walilazimika kuhama mji mmoja hadi mwingine wakihofia pengine wangevamiwa na makundi yenye uhusiano na vikundi vya kigaidi.
“Wakati nikiwa Jalalabad niliwaambia watoto wangu kutosema chochote kwa marafiki zao kuhusiana na kazi yangu hasa baada ya kujulikana kuwa mimi ndiye niliyemuua Osama.
Nakumbuka wakati fulani mke wangu aliwafuata maofisa wa CIA akitaka kubadilisha jina na apelekwe katika mji mwingine kwa hofu kuwa pengine angevamiwa na watu wasiojulikana.
Hata hivyo jaribio lake hilo halikufaulu na baadaye akaamua kuondoka na kwenda kuishi katika mji mwingine akiwa na watoto.  Askari huyo anasema kuwa muda mwingi aliotumia jeshini ulimfanya apoteze upendo wa karibu na familia yake jambo lililosababisha kuvunjika kwa ndoa yake.
Wakati akizungumza katika mahojiano maalumu na mwandishi mmoja wa habari, mke wa askari huyo alieleza sababu za kuachana na mumewe ambaye alikuwa ameishi naye kwa zaidi miaka 10.
“Sikupenda kuendelea kuishi maisha ya hofu… halafu isitoshe muda mwingi nilikuwa mpweke na mwenzangu mara zote alikuwa kwenye safari za mbali.
“Hata hivyo, siwezi kusema simpendi hapana, bado tunawasiliana na jambo kubwa ni hawa watoto wetu tungependa kuona wanaendelea kupata uangalizi wa karibu kutoka pande zote mbili. Nimefurahi kuona sasa niko peke yangu lakini bado tunawasiliana kwa karibu na mwenzangu,” alisema mama huyo.
Mama huyo ambaye hata hivyo hakutaka  jina lake kuchapishwa hadharani, hivi sasa anaishi Milwaukee ambako anajishughulisha na  kazi za hapa na pale kwa ajili ya kuendesha maisha yake.
Akizungumzia maisha yake baada ya kurejea toka kwenye operesheni nchini Pakistan, askari huyo anasema kuwa, aliendelea kuishi maisha ya furaha na amani huku akipata pongezi toka kwa ndugu na marafiki zake kutokana na kitendo  cha kishujaa cha kuondosha maisha ya Osama.
Lakini hata hivyo bado anakumbuka jinsi operesheni ya kusambaratisha ngome ya Osama ilivyoendeshwa.
“Unajua mie ndiye niliyekuwa wa mtu wa mwisho kumwona Osama wakati akiwa bado hai. Baada ya hapo askari wote waliokuja baada yangu walikuta mwili umelala sakafuni ndiyo maana walipiga risasi za ovyo ovyo tu.
“Nakwambia ile operesheni ilifanikiwa kwa mazingira ya ajabu sana, kwani wakati tunakwenda kuvamia nyumba yake tulikuwa bado tuna mashaka mengi kama kweli hesabu zetu zilikuwa sahihi au la.
“Wakati fulani nakumbuka tukiwa bado angani lakini tumekaribia eneo la tukio tuliulizana je, tulipue kwa bomu ama twende kwa kutumia uvamizi wa ardhini.Tulishauriana kwa muda kidogo lakini baadaye tukafikia uamuzi wa pamoja kwenda kwa kutumia mashambulizi ya ardhini kwani tulikuwa tayari tumejifua vya kutosha.
“Nakumbuka pia wakati  tunatoka Washington kuelekea Pakistan tulikuwa tumegawanywa kwa makundi. Kuna wale waliokuwa kitengo cha CIA, makomandoo, walenga shabaha na wengine katika idara za kawaida. Pia nakumbuka tulikuwa tumeambatana na mbwa wawili ambao walitusaidia kwa kiwango kikubwa wakati tulipoendesha upekuzi katika nyumba ya Osama baada ya kufanikiwa kumzingira na kumuua.
Akirejelea kwenye maisha yake baada ya kurejea nyumbani askari huyo anasema kuwa aliendelea kulitumikia jeshi hilo kwa miaka mingine 12 na baadaye ilipofika mwaka 2011 alistaafu na kurejea kwenye maisha ya uraiani.
“ Nimelitumikia jeshi kwa miaka mingi lakini ilipofika mwaka 2012 nikaamua kustaafu na kurejea kwenye maisha ya uraiani. Maisha ya jeshi kwa kweli yalikuwa na mikikimikiki mingi sana, lakini hata hivyo namshukuru Mungu niliingia salama na nimetoka salama pia.”
Anasema kuwa jambo linaloendelea kusalia kichwani mwake ni kuwa mazingira yaliyomsukuma kuingia jeshini ndiyo hayohayo yaliyomponza wakati akiwa jeshini.
Pamoja na ufahari mkubwa alionao wa kuondosha uhai wa aliyekuwa adui mkubwa wa Marekani, Osama bin Laden lakini anasema kuwa alijikuta akitengana na mkeo kutokana kile alichokieleza kuwa uhusiano wa mbali uliosababishwa na asili ya kazi yake.
Kwa upande mwingine anasema kuwa, “Jambo jingine linaloendelea kunivunja moyo ni kupuuzwa na Serikali. Unajua wakati mwingine hizi kazi hazina shukrani kabisa. Hebu fikiria mie ndiye niliyekuwa mstari wa mbele na kufanikisha kumuua yule gaidi nambari moja, lakini sijawahi kupewa nishani yoyote ama barua ya shukrani… nadhani hilo ndilo ninaloniumiza sana moyo.”
Anasema kuwa pamoja na kwamba sheria na taratibu za uajiri zinazuia kutoa hadharani baadhi ya taarifa zinazohusu utendaji wa jeshi lakini hata hivyo amedhamiria kutunga kitabu kitachoelezea jumla ya mambo ili dunia ipate kujua .
“Nafahamu kuna baadhi ya taarifa ni classified (maalumu) hazipaswi kutolewa hadharani mpaka itakapoamuliwa ifanywe hivyo, lakini mimi na rafiki yangu tupo kwenye mpango wa kuandika kitabu ambacho nadhani kitatoa picha nzima itakayoelezea uzoefu wangu jeshini na kwa kiasi operesheni ya kusambaratisha ngome ya Osama,” alieleza.
Chanzo: Mwananchi, gazeti.

Take your time and read this, it is very interesting and funny....


Na Edna Bondo
WAKATI watanzania wengi hawajasahau machungu ya kulizwa na kampuni ya kupanda na kuvuna mbegu ya DECI, kumeibuka taasisi mpya ya fedha inayojitapa kutoa mikopo kwa njia ya mtandao, huku ikitumia vibaya majina ya Rais Jakaya Kikwete na Barack Obama wa Marekani.
Mbali ya taasisi hiyo ya Tanzania Loans Society kutumia majina ya marais hao, imewahusisha pia Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Ridhiwani Kikwete, ambapo inahofiwa kutapeli mamilioni ya walalahoi.
Taarifa za taasisi hiyo zinaonesha kuwa ilianza shughuli zake mwaka 2012, na kupata ufadhili wa fedha kutoka kwa Rais Obama, ambapo inasimamiwa na Rais Kikwete, Waziri Mkuu Pinda na mratibu mkuu ni Ridhiwani.
Watendaji wengine ni Michael John ambaye namba yake ya simu ya mkononi ndiyo inayotumika kutuma pesa za usajili.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili, umebaini kuwa taasisi hiyo, imekuwa ikijitangaza kutoa huduma ya mikopo na mawasiliano ya jinsi ya kupata mikopo hiyo, hufanyika kwa njia ya mtandao ili kuwawezesha wateja wa mikoani kupata mikopo hiyo kirahisi bila usumbufu wa kuja makao makuu yao jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wananchi walioomba kupata mikopo hiyo, waliliambia gazeti hili kuwa, fomu za mikopo ya taasisi hiyo hutolewa kwa sh 15,000 ambazo nazo hulipiwa kwa njia ya mtandao.
Mmoja wa wateja wa taasisi hiyo aliyedai kutapeliwa, Maywood Maganga alisema alionja machungu baada ya kuingia kwenye tovuti yake na kukutana na maelekezo ya kumtaka ajaze fomu na taarifa zake binafsi na kisha kutakiwa kutuma sh 15,000 kwenda kwenye namba 0656 73 64 16, iliyosajiliwa kwa jina la Michael John.
Maganga alisema kuwa alifanya hivyo, na kusubiri majibu.
Kwa mujibu wa mkopo huo wenye masharti nafuu, tena usio na riba, mteja hutakiwa kurejesha na kuanza kukatwa baada ya miezi miwili tangu siku ya kupokea pesa hizo za mkopo.
“Maelezo ya mkopo huo yanaonesha kuwa una masharti nafuu sana na marejesho yake ni sh 60,000 kila mwezi bila kujali kiasi ambacho mteja amekopa.
“Maelezo ya fomu niliyojaza yalinionesha kwamba nitapata sh 300,000 kama zawadi kwa kukubali kukopa na baada ya dakika 30, ningeingiziwa kiasi cha fedha za mkopo nilizoomba,” alisema.
Kwa mujibu wa Maganga, fomu alizozikuta kwenye tovuti ya taasisi hiyo, zilionesha mahala ofisi ilipo, lakini alipofuatilia na kuuliza, alibaini kuwa taasisi hiyo haina ofisi katika jengo la serikali la Utumishi wa Umma.
“Mwanzoni sikuwaza kama taasisi hii itakuwa ya kitapeli, lakini baada ya siku mbili ya kutokutumiwa pesa hiyo ndipo nilipogundua kwamba nimetapeliwa,” aliksema.
Maganga aliziomba mamlaka husika kuingilia kati kwa kudhibiti utapeli huo, kwani Watanzania wengi wameshalizwa kupitia taasisi hiyo inayotumia majina ya watu maarufu kutapeli.
Aidha, maelezo ya tovuti hiyo yanaeleza zaidi kuwa kwa kutambua ugumu wa maisha uliopo kwa Watanzania na kukua kwa teknolojia kama nchi zingine zifanyavyo, taasisi hiyo inatoa mikopo kwa njia hiyo ya mtandaao ili kuepuka usumbufu wa kuwafikia watu walioko mikoani ili nao wanufaike.
Mbali ya hayo, pia taarifa ya maelezo ya taasisi hiyo hiyo ilieleza kuwa kiwango cha chini cha kupata mkopo ni sh 100,000 na ofisi zake zipo katika jengo la utumishi wa umma, ghorofa ya tano chumba namba 30.
Ridhiwani hakuweza kupatikana kuzungumzia taasisi hiyo, lakini katika taarifa aliyoituma hivi karibuni kwenye ukurasa wake wa facebook, alikanusha yeye na viongozi wa serikali akiwemo Rais Kikwete kuhusika na taasisi hiyo.
“Maisha ni kuhangaika na kwamba inataka mtu anayefahamu njia sahihi kuweza kujua kuwa nikitumia njia hii hali itakuwa sawa na pengine mambo yangu yatanyooka.
“Hii inaweza kuwa ndiyo maana halisi ya kuhangaika ufanikiwe, lakini tafsiri hii haiwezi kuwa kutumia njia za kudhulumu, kukaba, kuiba au kufanya utapeli ili ufanikishe malengo yako mabaya dhidi ya mtu au kikundi fulani cha watu," aliandika Ridhiwani kwenye ukurasa wake wa facebook.
Kwa mujibu wa Ridhiwani, hivi karibuni alipokea ujumbe mfupi wa maandishi kupitia simu yake ya mkononi na barua pepe, ikihoji kuhusika kwake na kampuni hiyo.
Alisema mradi huo unadaiwa kuanzia katika mikono ya Rais Obama kuja Tanzania kupitia Kikwete na sasa yeye akishirikiana na Waziri Mkuu Pinda wanauendesha.
“Jambo hili si la ukweli hata kidogo, na naomba kutumia nafasi hii kulikanusha kabisa mbele ya umma wa Watanzania na wale wote ambao kwa namna moja au nyingine wanafuatilia,” ilisema taarifa hiyo ya Ridhiwani.
Vilevile taarifa ya Ridhiwani ilitahadharisha umma wa Watanzania kuwa makini na mambo ya mitandao ambayo hutumia jina lake kwa utapeli kwa lengo la kumchafua, lakini yeye na viongozi wengine hawahusiki na Tanzania Loans Society.
Viongozi wa taasisi hiyo hawakuweza kupatikana kwa njia yoyote ile kwani simu zao hazipokelewi na hata katika ofisi wanazodai kuwapo, hawaonekani.Tanzania Daima.

UFUMBUZI WA MADAI YA FIDIA MILIONI 278 KWENYE UJENZI WA BARABARA NA DARAJA GOLANI SUCA


SUNDAY, FEBRUARY 24, 2013


Tarehe 19 Februari 2013 Mbunge wa Ubungo, John Mnyika alifanya ziara ya kikazi katika kata za Kimara na Saranga kufuatilia kuhusu matengenezo ya barabara na daraja la Golani. 

Mnyika alifanya hivyo siku mbili tangu afanye mkutano wa kikazi na viongozi wa Serikali ya Mtaa wa Kanuni na wananchi katika kata ya Mabibo tarehe 16 Februari 2013 kulitolewa malalamiko kuhusu Kampuni ya Maji Safi na Maji Taka (DAWASCO) kutoshughulikia maombi ya wananchi yaliyowasilishwa kwa kampuni hiyo kwa nyakati mbalimbali kati ya mwaka 2010 mpaka 2012. 

Ikiwa ni sehemu ya ufuatiliaji huo kuhusu barabara, Mnyika alikutana na wananchi ambapo walipaswa kulipwa fidia inayokadiriwa kufikia shilingi milioni 278 ili kuruhusu njia mbadala kupatikana kufuatia ujenzi wa daraja katika eneo hilo. 

Aidha, Mbunge amekagua matumizi ya daraja hilo yaliyoanza kupitia njia ya zamani na athari zake katika mfumo mzima wa usafiri katika eneo husika; na kubaini kwamba daraja husika haliwezi kuzinduliwa pamoja na kuwa limeanza kukamilika mpaka ujenzi wa kingo za mito ukamilike pamoja na kupatikana kwa barabara mbadala baada ya wananchi kulipwa fidia. 

Mara baada ya ziara hiyo Mbunge alikutana na uongozi wa Manispaa ya Kinondoni na kuwasilisha madai hayo ya wananchi ambao miezi zaidi ya sita imepita toka nyumba zao ziwekewe X bila hata ya kufanyiwa tathmini. Baada ya Mnyika kuwawakilisha wananchi hao uongozi wa Manispaa umeamua kutuma timu ya uthamini na mara baada ya uthamini huo, kutuma uongozi kukamilisha majadiliano na wananchi husika kabla ya tarehe 25 Februari 2013

Itakumbukwa kwamba tarehe 6 Mei 2011 Mbunge Mnyika alitembelea kata za Saranga na Kimara kufuatilia utekelezaji wa mipango ya maendeleo na kuwajulisha wananchi wa maeneo husika kwamba jumla ya shilingi milioni zaidi ya mia tano (501,973,470) zilitengwa kwenye bajeti ya Halmashauri ya Kinondoni kwa mwaka wa Fedha 2011/2012 kwa ajili ya kujenga Daraja Kubwa la Burura/Golani katika Mto Ubungo.

Baada ya ujenzi wa daraja hilo kuchelewa mbunge alichukua hatua za kufuatilia kwa mara nyingine mwezi Aprili 2012 na hatimaye mkataba wa ujenzi wa daraja husika umesainiwa kati ya Manispaa ya Kinondoni na Mkandarasi Kika Co. Ltd kwa gharama za shilingi milioni 447. Gharama za ujenzi huo zimeongezwa kwa nyakati mbalimbali mpaka kufikia milioni 672.

Ifahamike kwamba kutokuwepo kwa daraja katika eneo hilo miaka mingi kulifanya mawasiliano katika maeneo hayo kuwa magumu nyakati za mvua na kusababisha madhara ya kibinadamu na mali wananchi wanapovuka mto katika eneo hilo wakati wa mafuriko.

Baada ya mbunge kuwawakilisha wananchi kwa kushirikiana na madiwani kutaka ujenzi wa daraja hilo, liliingizwa kwenye bajeti ya Manispaa ya Kinondoni kwa mwaka wa fedha 2011/2012 kwa vyanzo vya ndani (own source). 


Imetolewa tarehe 20 Februari 2013 na: 

Aziz Himbuka 

Katibu Msaidizi 

Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Ubungo

Afrika kwanza....

 Katibu mkuu umoja wa mataifa Ban Kin Moon akiwa na viongozi wa nchi za ukanda wa maziwa makuu wakati wa utiliaji saini mpango wa umoja wa mataifa wa amani, usalama na ushirikiano katika nchi ya kongo (DRC) mjini Addis Ababa, Ethiopia jana.

Rais Kikwete akipongezana na waziri mkuu mpya wa Ethiopia ambae ndie mwenyeji wa mkutano huo ndugu Hailemariam Desalegn baada ya utiliaji saini mpango huo kwenye jumba la umoja wa Afrika mjini Addis Ababa, Ethiopia jana Feb 24, 2013. Anaeshuhudia furaha hiyo katikati ni mwenyekiti wa kamisheni ya umoja wa mataifa Dk Nkosazana Clarice Dlamini-Zuma.


 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete  leo Februari 24, 2013 ameungana na Wakuu wenzake wa Nchi za  Ukanda wa Maziwa Makuu  kutia  saini Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Amani, Usalama na Ushirikiano katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) mjini Addis Ababa, Ethiopia.
Mhe. Rais Kikwete alisema mara baada ya utiwaji saini wa Mpango huo kwamba: “Hii ni siku kubwa na ya kihistoria kwa watu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, jirani zake na Ukanda wote wa Maziwa Makuu. Ni siku ya kukumbukwa kwa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC), Afrika, Umoja wa Afrika, Umoja wa Mataifa na Jumuiya yote ya Kimataifa. “Watu wa Kongo wameteseka kwa muda mrefu sana. Wanastahili kupumua sasa. Wanastahili kuishi maisha
bora; maisha ambayo usalama wao umehakikishiwa na kuthibitishwa; maisha ambayo yatawafanya waendeshe maisha yao kwa kufanya mambo ya maana zaidi katika kuboresha  maisha yao ya kila siku.
“Saini tulizotia kwa Mpango huo leo ni kielelezo cha  dhati na ahadi ya utekelezwaji wa  yale yanayotarajiwa na watu wa Kongo na Ukanda wa Maziwa Makuu kwa ajili ya Amani, Usalama na Ushirikiano.
“Kwa niaba ya Serikali na Watu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania naahidi kwamba sisi tutatekeleza kwa dhati yale yote yanayotarajiwa kwa upande wetu”, alisema.
Mpango huo umetiwa saini na viongozi kutoka   Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Jamhuri ya Uganda, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Jamhuri ya Angola, Jamhuri ya Burundi, Jamhuri ya Kongo (Brazaville), Jamhuri ya Zambia, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Jamhuri ya Afrika Kusini.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Mhe. Ban Ki-moon, Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa, Dkt. Nkosazana Dlamini-Zuma, pamoja na wenyeviti wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) na Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR) wametia  saini Mpango huo kama mashahidi na wadhamini.
Mpango huo una nia ya kuchangia juhudi ambazo zimefanywa na ICGLR na SADC katika kutafuta amani Mashariki ya Kongo na ukanda wote wa Maziwa Makuu kwa ujumla.
Mpango huo pia umetilia maanani mapendekezo muhimu yaliyokubalika baada ya mashauriano kati ya wakuu wa nchi za ICGLR  na SADCna Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.
Mapendekezo ya mpango huo ni pamoja na kuboresha sekta ya Ulinzi na usalama, hususan jeshi la polisi, Kuimarisha mamlaka ya nchi hasa mashariki ya Kongo; na kuendeleza ajenda kuhusu maelewano, kuvumiliana na kudumisha demokrasia nchini humo.
Vile vile, nchi za Kanda zimetakiwa kutoingilia mambo ya ndani ya nchi jirani, kututoa msaada wowote wa vikundi vya waasi, kuheshimu utawala na maeneo ya nchi jirani na kuimarisha mahusiano ya Kanda.
Hali kadhalika, Jumuiya ya Kimataifa imetakiwa kuisaidia DRC na Kanda yote ya Maziwa Makuu kwa ujumla katika utekelezaji wa miradi muhimu pamoja na mkataba wa Amani, Usalama na Maendeleo katika Ukanda wa Maziwa Makuu.
Aidha, Mpango huo unapendekeza kuwepo kwa chombo cha usimamizi (Oversight Mechanism) ambacho kitaundwa na viongozi wote wa nchi 11 pamoja na Umoja wa Mataifa, SADC na ICGLR.
 Imetolewa na:
Muhidin Issa Michuzi,
Mwandishi wa Habari wa Rais, Msaidizi,
Addis Ababa,
ETHIOPIA.
24 Februari, 2013


Sunday, February 24, 2013

Huu ndiwo urafiki wa kweli kwenye shida na raha. Jakaya Kikwete ashiriki mazishi ya baba yake M7 Uganda.

 Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete akimpa pole mke wa Rais wa Uganda Yoweri Museven mama Janet Museven katika mazishi ya baba mkwe wake nchini Uganda.

Rias Kikwete akiwa na Rais Museven jana katika mazishi ya baba wa Rais huyo wa Uganda.

 Rais Kikwete akitoa heshima za mwisho katika jeneza la mzee Amos Kaguta (97) baba yake Rais Yoweri Kaguta Museven aliefariki wiki iliyopita nchini Uganda.

Rais Kikwete akiweka mchanga katika kaburi la mzee Amos Kaguta wakati wa mazishi yake kwenye kijiji cha Rwakitura magharibi mwa Uganda jana.

Picha zote kwa hisani ya mpiga picha wa Ikulu Fred Maro.

Rais Jakaya Kikwete alishiriki mazishi hayo alipopita Uganda akiwa njiani kurudi nyumbani akitokea nchini Ethiopia, ambapo wakuu wa nchi za Afrika ukanda wa maziwa makuu walikuwa wakitia saini mpango wa umoja wa mataifa wa amani, usalama na ushirikiano katika nchi ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo,mjini Addis Ababa.

Friday, February 22, 2013

Coastal Union na Yanga tofauti yao ni point 6 tu.

Pos. Logo Club P W D L GF GA GD Pts
1 Young Africans FCYoung Africans SC 16 11 3 2 32 12 20 36
2 Azam FCAzam FC 17 11 3 3 31 14 17 36
3 Simba SCSimba SC 17 8 7 2 26 14 12 31
4 Coastal Union SC 18 8 6 4 21 16 5 30
5 Kagera Sugar FCKagera Sugar FC 17 7 6 4 18 15 3 27
6 Ruvu Shooting StarsRuvu Shooting Stars JKT 16 7 4 5 20 17 3 25
7 Mtibwa Sugar FCMtibwa Sugar FC 17 6 6 5 20 18 2 24
8 JKT Mgambo 17 6 3 8 13 16 -3 21
9 JKT Oljoro FC 18 5 6 7 19 22 -3 21
10 Tanzania Prisons 16 4 6 6 10 13 -3 18
11 JKT Ruvu StarsJKT Ruvu Stars 16 4 4 8 14 26 -12 16
12 Toto African Toto African 19 2 8 9 15 28 -13 14
13 African Lyon FCAfrican Lyon FC 18 3 3 12 12 30 -18 12
14 Polisi Moro 16 2 5 9 8 18 -10 11