Thursday, February 28, 2013

Warsha ya wadau wa kilimo katika picha...

 Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bw Sazi Salula akifungua Warsha ya Wadau ya Kupitia na Kujidili Muongozo wa Kitaifa wa Mabadiliko ya Tabianchi juu ya Wakulima na Wafugaji Nchini Kulia Mkurugenzi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais Dk Julias Nihgu Warsha imefanyika kwenye Hotel ya Palmtree Village Bagamoyo.
 
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bw Sazi Salula akimsikiliza jambo Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Mazingira Ofisi ya Makamu wa Raisi Bw Richad Muyungi mara Baada ya Ufunguzi wa Warsha hiyo jana.y



 Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bw Sazi Salula akiwa katika Picha ya Pamoja na Washiriki wa Warsha ya Kupitia na Kujadili Muongozo wa Kitaifa wa Mabadiliko ya tabianchi juu ya Wakulima na Wafugaji Nchini.



Mkurugenzi Msaidizi Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais Bw Richad Muyungi akimwambia jambo Afisa Mazingira Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bw Daniel Nkondola Mara baada ya Ufunguzi wa Warsha hiyo jana.



 [Picha zote na Ali Meja Ofisi ya makamu wa Rais]


Monica Sapanjo- Ofisi ya Makamu wa Rais

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bwana Sazi Salula amewataka wadau wa sekta ya kilimo  nchini hasa wakulima wadogo wadogo  kujitahidi  kufahamu athari  na  changamoto mbalilmbali zinazoikabili sekta hii kutokana na athari za  mabadiliko ya tabianchi. Alitoa rai hiyo wakati akifungua warsha ya siku mbili  ya kitaifa ikihusisha wadau mbalimbali kuandaa  mwongozo wa taarifa za kuhimili mabadiliko ya tabianchi kwa  jamii za wakulima na wafugaji nchini.

Aliwaomba wajumbe wa warsha hiyo kutoa maoni yao ya kitaalamu ili kuhakikisha   mwongozo unakuwa tayari kwa matumizi ya jamii za wakulima na wafugaji nchini mapema iwezekanavyo hasa ikinzingatiwa kuwa athari sasa zimeanza kuwa kubwa sana. Alisema  mwongozo huu  ni muendelezo wa juhudi za serikali katika kushughulikia masuala ya mabadiliko ya tabianchi. "Juhudi hizi zitaiwezesha nchi kuhimili atahari za mabadiliko haya na kuchangia juhudi za kimataifa za kupunguza gesijoto" alisema Bwana Salula.

Warsha hiyo ya siku mbili imeandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais kwa ufadhili wa Serikali ya Japana kupitia UNDP,  kwa ajili ya kujadili mwomgozo huu wa kusaidia wakulima na wafugaji wadogo wadogo kuhimili  mabadiliko ya tabianchi. Washirki wa warsha hiyo  ni kutoka kwenye taasisi  mbalimbali  ikiwa ni pamoja na  Ofisi ya Waziri mkuu, Wizara ya maji, Wizara ya habari na michezo, Wizara ya kilimo na baraza la Mazingira la Taifa(NEMC, Jumuia ya Wakulima Tanzanaia na asasi mbalimbali zisizo za kiserikali.

Madhumuni ya mwongozo huu ni kuwasaidia wakulima na wafugaji  kuendeleza shughuli zao za ufugaji na ukulima katika maeneora ambayo yamebadilika kutokana na mabadiliko ya tabianchi.



No comments:

Post a Comment