Tuesday, March 5, 2013

Christian Ronaldo amtengua udhu Ryan Giggs katika mechi yake ya 1,000.





Christiano Ronaldo leo amekuwa mwiba kwa timu yake ya zamani Man United baada ya kufunga goli moja katika mawili yaliyozamisha jahazi la mashetani wekundu kuendelea na klabu Bingwa barani Ulaya.

Ronaldo alifunga goli la pili dakika ya 68 baada ya Modric kusawazisha bao la kujifunga ndani ya dakika ya 48 lililowekwa kimiani na mchezaji wa Madrid Sergio Ramos.

Wapenzi wa soka duniani, leo macho yao yalikuwa kwa mchezaji mkongwe wa Manchester United, Ryan Giggs aliecheza mechi yake ya 1,000 tangu aanze kuichezea timu hiyo mwaka 1990.

Manchester United ya Uingereza leo ilikuwa na kibarua kigumu dhidi ya Real Madrid ya Hispania, katika mchezo wa kihistoria wa marudiano wa Klabu Bingwa Ulaya, uliopigwa kwenye uwanja wa Old Trafford, jijini Manchester.

Mara ya mwisho timu hizo kukutana katika uwanja huo ni miaka kumi iliyopita katika mchezo wa marudiano Klabu Bingwa Ulaya, ambapo Manchester United ilishinda 4-3.

Hata hivyo, Manchester United waliaga michuano hiyo kwa tofauti ya magoli 6-5, kwani katika mchezo wa awali katika uwanja wa Bernabeu, jijini Madrid, Real Madrid ilishinda 3-1.

Wakati Giggs na mashabiki wake wakisherehekea mechi ya 1,000, mchezaji Cristiano Ronaldo kutoka Ureno wa Real Madrid amekuwa gumzo la mashabiki hao kama ilivyokuwa kwa Ronaldo De Lima wakati timu hizo zilipokutana kwa mara ya mwisho katika kombe kama hilo, April 23, 2003.

Aidha, Ronaldo De Lima kwa miaka hiyo, alikuwa akishutumiwa kushuka kiwango kama ambavyo Cristiano anavyoshutumiwa kwa sasa, hasa wapinzani wake wakipima kiwango chake na Lionel Messi wa Barcelona.

Hata hivyo, Ronaldo De Lima, alifunga midomo ya mashabiki wa Uingereza kwa kutumbukiza mabao yote matatu, katika ushindi wa Manchester United wa mabao 4-3, mabao matatu hayo ya Real Madrid yote yakiwekwa kimiani na Ronaldo.

Steve McManaman, kiungo wa Real Madrid wakati huo alisema: “Kila mmoja alikuwa na hamu ya kumuona Ronaldo. Alituhumiwa sana kuhusiana na kiwango chake, lakini kwa mabao matatu aliyofunga alidhihirisha alikuwa na uwezo mkubwa katika mechi muhimu kama ile.”

Manchester imekutana na Real Madrid wakiwa na matokeo ya nguvu sawa ya suluhu ya 1-1 wiki mbili zilizopita katika uwanja wa Santiago Bernabeu, hivyo Real Madrid walikuwa na kazi kubwa sana ya kutinga robo fainali ya michuano hiyo inayoheshimika barani Ulaya kwani wapinzani wao walikuwa na faida ya goli la ugenini.

Nadhani usiku wa leo historia ya Ronaldo wawili imejirudia kwani mbali ya bao moja alilopata Crostiano lakini yapo mabao mengi zaidi ambayo laiti yote yangeikia wavuni basi nae angetoka na magoli matatu kama mtangulizi wake Ronaldo De Lima.

HAFIDH KIDO
6 March, 2013
Dar es Salaam, Tanzania









No comments:

Post a Comment