Thursday, March 7, 2013

Kenya wahamia Analojia katika kuhesabu kura.



Shughuli ya kuhesabu kura katika uchaguzi wa Kenya ingali inaendelea kwa kujikokota, baada ya mashine za elektroniki kugoma na kisha kutupiliwa mbali.
Makarani waliokuwa wanahesabu kura katika vituo vya kupigia kura wamelazimika kupeleka karatasai zao katika kitovu cha kutangazia matokeo ya kura ya urais katika ukumbi wa Bomas viungani mwa mji wa Nairobi.
Kura sasa zinahesabiwa kwa njia ya kawaida.
Mgombea wa urais Uhuru Kenyatta, ameweza kusalia mbele ya mpinzani wake Raila Odinga kwa zaidi ya kura laki tano, lakini maafisa wa uchaguzi wanasema shughuli hiyo huenda ikachukua muda.
Mkuu wa tume ya uchaguzi ameonya kuwa huenda shughuli hiyo ikakamilika Ijumaa au hata Jumatatu kabla ya mshindi kujulikana.
Wakati huo huo Chama cha mgombea wa urais nchini Kenya , Uhuru Kenyatta, kimekosoa uamzi wa tume ya uchaguzi , kwamba kura zilizoharibika zinapaswa kuongezwa katika idadi ya kura zilizohesabiwa.
Hii itapunguza kwa kiwango kikubwa uwezekano wa bwana Kenyatta , ambaye sasa anaongoza kwa kura zilizohesabiwa.
Katiba ya kenya inasena kuwa ili kufanya hivyo , kura zilizoharibiwa zinapaswa kuwa zaidi ya nusu ya jumla ya kura zilizopigwa, lakini kwa sababu ya matatizo ya mfumo wa kielektroniki , kura zilizoharibika tayari zimefikia zaidi ya laki tatu .
Matatizo ya kielektoniki yanaendelea , na maafisa wa Kenya wanasema matokeo rasmi huenda yasitangazwe hadi mwishoni mwa juma.
Chanzo: BBC Swahili.

No comments:

Post a Comment