Wednesday, March 13, 2013

Kura za Papa hazijatosha....


Moshi mweusi umetokea kwenye dari la hekalu ya Sistine mjini Roma, kumaanisha kuwa makadinali walioko ndani ya hekalu wameshindwa kuafikiana juu ya Papa mpya anayetarajiwa kuchaguliwa.
Moshi mweupe utaashiria kupatikana kiongozi mpya wa kanisa Katoliki la Roma.
Makadinali hao wanatarajiwa kupiga kura mara nne kwa siku hadi pale thuluthi mbili ya makadinali wote watakapoafikiana juu ya Papa mpya.
Walipiga kura yao ya kwanza ambayo haikuleta maafikiano hapo usiku wa Jumanne. Yeyote atakayeteuliwa kuliongoza kanisa hilo katoliki anakabiliwa na wakati mgumu, ambapo kanisa limezongwa na kashfa mbali mbali pamoja na migawanyiko ya ndani.
Papa aliyeondoka Benedikt wa Kumi na sita aliwashangaza wengi alipotangaza kujiuzulu wadhifa huo miaka minane tu tangu kuchaguliwa. Yeye ndiye Papa wa kwanza kujiuzulu katika miaka 600 ya historia ya kanisa hilo.
Alitoa sababu kuwa amezeeka na afya yake imedhoofika kwa hivyo haoni kuwa anaweza kutekeleza wajibu wake kikamilifu kama Papa wa kanisa.

No comments:

Post a Comment