Wednesday, March 27, 2013

Mahakama ya rufaa nchini Misri, imeamuru kiongozi mkuu wa mashtaka aliyefutwa kazi na rais Mohammed Morsi kurejeshwa kazini mwezi Novemba.



 27 Machi, 2013 - Saa 14:08 GMT
·                              

Mahakama hiyo imefutilia mbali uamuzi wa rais Mosri kumteua mwendesha mkuu wa mashtaka mwingine Talat Ibrahim.
Hatua ya Bwana Morsi kumfuta kazi Abdel Maguid Mahmoud, iliwaudhi sana majaji wakuu walioina kama hatua ya kuhujumu mamlaka yao.
Hii ilikuwa hatua ya kwanza kama hii kutokea baada ya rais Mosri kujiongeza mamlaka makubwa.
Hatua ya rais Morsi iliindolea idara ya mahakama mamlaka yake ya kuweza kubatilisha uamuzi wowote tatanishi alioutoa . Lakini rais Morsi baadaye alibatilisha uamuzi wake baada ya maandamano makubwa kumpinga.
Kiongozi wa mashtaka wa sasa bwana Mahmoud, aliteuliwa na rais wa zamani Hosni Mubarak.
Aidha Talaat Ibrahim naye alitakiwa kudurusu uchunguzi kuhusu vifo vya waandamanaji waliopinga serikali ya Mubarak.
Afisaa mkuu wa serikali aliambia BBC kuwa serikali itakata rufaa dhidi ya uamuzi wa mahakama ya juu zaidi nchini Misri.
Bwana Morsi amekabiliwa na matatizo chungu nzima tangu kuchukua mamlaka mwezi Juni mwaka 2012 baada ya uchaguzi wa kwanza kufanyika tangu kuondolewa mamlakani kwa Mubarak.
 Chanzo: BBC Swahili.

No comments:

Post a Comment