Tuesday, April 2, 2013

Madonna azua utata mpya Malawi.


Msanii wa kimataifa Mmarekani, Madonna anafanya mkutano na rais wa Malawi, Joyce Banda kujaribu kusuluhisha mzozo kuhusu kazi ya misaada ya msanii huyo nchini humo.
Mwezi Disemba,shirika la misaada linalomilikiwa na Madonna lilitangaza kuwa limejenga shule kumi nchini Malawi.
Hata hivyo waziri wa elimu Eunice Kazembe, alisema kuwa Madonna ameweza tu kujenga madarasa kumi katika shule zilizopo.
Madonna ameasili watoto wawili, kutoka Malawi, na aliahidi kuwarejesha nyumbani kwao baada ya miaka michache.
Chanzo: BBC Swahili.

No comments:

Post a Comment