Monday, April 22, 2013

Suarez apewa saa 12 kukubali au kukataa kitendo cha kum-Tyson beki wa Chelsea Branislav Ivanovic.



Chama cha soka nchini Uingereza, FA kimenuia kumpa adhabu kali mshambuliaji wa Liverpool Luis Suarez kwa kitendo chake cha kumng'ata beki wa Chelsea Branislav Ivanovic katika mchezo wa jumapili baina ya Liverpool na Chelsea,mchezo uliomalizika kwa sare ya 2-2.
FA imesema mwamuzi wa mchezo huo hakukiona kitendo hicho uwanjani lakini marejeo ya picha za mchezo huo zilionyesha Suarez alimng'ata Ivanovic,kitendo ambacho kinachukuliwa kama vurugu mchezoni na adhabu yake ni kufungiwa mechi tatu lakini adhabu hiyo haitoshi kwa tukio alilolifanya Suarez.
Suarez amepewa muda wa mpaka saa 12 jioni jumanne ya April 23, awe amekubali au kukataa kosa hilo kabla ya tume ya kudhibiti maadili haijakutana hapo siku ya jumatano kutoa hukumu stahili kwa kosa hilo.
Mwenyewe Suarez aliisha kiri kufanya kosa hilo na kumuomba Ivanovic msamaha kwa njia ya simu na kuwaomba mashabiki wa soka wamsamehe kwa kosa hilo.
Klabu yake ya Liverpool imempa adhabu ya kumpiga faini mchezaji huyo wa kimataifa wa Uruguay.
Mwaka 2010, Suarez wakati akiichezea Ajax ya Uholanzi alimng'ata begani kiungo wa PSV Eindhoven, Otman Bakkal na kufungiwa mechi saba na chama cha soka nchini Uholanzi kwa kosa hilo.
Itakumbukwa Suarez tayari amekwishawahi kufungiwa kutocheza mechi nane za mashindano nchini Uingereza na faini ya paundi elfu 40 kwa kosa la kumtolea lugha ya kibaguzi beki wa Manchester United Patrice Evra mwaka 2011.
BBC SWAHILI

No comments:

Post a Comment