Tuesday, May 21, 2013

Mourinho njia nyeupe kurudi Chelsea.

Klabu ya Real Madrid imethibitisha kuwa kocha wa timu hiyo Jose Mourinho ataondoka kwenye kibarua cha kuifundisha timu hiyo mwishoni mwa msimu.

Rais wa klabu ya Real Madrid,Florentino Perez amewaambia waandishi wa habari jumatatu jioni kuwa Mourinho hatofukuzwa bali wamekubaliana kumaliza mkataba wao na kocha huyo raia wa Ureno.

Aidha Madrid, imeongeza kuwa haijaanza mazungumzo na kocha yeyote kwaajili ya kuchukua nafasi ya Mourinho lakini vyanzo mbalimbali vya habari za michezo zinamtaja kocha wa PSG ya Ufaransa, Carlo Ancelloti kuchukua jukumu la kuifundisha Madrid msimu ujao.

Duru za kimichezo zinasema, Jose Mourinho huenda akarejea nchini Uingereza kuifundisha klabu yake ya zamani ya Chelsea baada ya kuwepo makubaliano baina yake na uongozi wa klabu hiyo.

Wakati Real Madrid ikitangaza kuwa inamtaka Kocha Carlo Ancelotti timu yake ya Paris St-Germain ya Ufaransa imesema haiwezekani yeye kuhama.

Wiki iliyopita maombi ya klabu hicho cha Uhispania yalikataliwa na mabingwa hao wapya wa Ufaransa.
Taarifa zinazohusiana.
                                                                         Carlo Ancelotti

Sasa Ancelotti mwenyewe ametangaza kuwa anataka kuondoa Ufaransa na kuijunga na Real Madrid

"nimewaomba kuondoka na hadi sasa bado nasubiri jubu lao," Ancelotti, wenye umri wa miaka 53 amesema.

Lakini Rais wa PSG Nasser al-Khelaifi mwenye makao yake Qatari amesema: " ameomba kuondoka na kujiunga na Real Madrid , hii haiwezekani kwa sababu kwa muujibu wakandarasi yake bado amesalia na mwaka mmoja, kwa hiyo huo ndio uamuzi wetu".

Akizungumza na kituo kimoja cha Televisheni cha Qatari rais huyo amesema : " hiyo ni shauri yake; sio tatizo letu . Mbali na mwaka mmoja uliosalia tumetangaza kumuongezea mwaka mmoja zaidi . Ukiwa na mkataba unapaswa kuuheshimu".

Hadi sasa Jose Mourinho ni Meneja wa Real Madrid inagawa imetangazwa kwamba anarudi Chelsea msimu ujao.

Wakati huohuo kocha mkuu wa Tottenham Andre Villas-Boas amesema ikiwa klabu hiyo inataka kufanya vyema msimu ujao basi lazima wamuhifadhi mchezaji Gareth Bale.

Spurs iliteleza kuingia katika michuano ya Klabu Bingwa bara Ulaya katika michuano ya siku ya mwisho wa Ligi kuu ya Uingereza baada ya Arsenal kuwafunga Newcastle 1-0 hivyo kumaliza ligi wakiwa alama moja juu ya Tottenham.

Kuna hofu kuwa mshambulizi huyo mwenye umri wa miaka 23 huenda akahama kutokana na Spurs kushindwa kufunzi katika mashindano hayo ya bara Ulaya.

Lakini Villas-Boas amesema: "ikiwa tunataka kufaunye vizuri zaidi msimu ujao nilazima tushikilie hazina yetu na hilo ndilo nimekuwa nikifahamishwa tangu awali".

Bale, ambaye anadaiwa kunyemelewa na timu kadhaa maarufu miongoni mwao Real Madrid aliifungua Spurs bao lao la ushindi dhidi ya Sunderland siku ya mwisho wa Ligi kuu ya Uingereza.

Licha ya ushindi huo bado Spurs ilimaliza katika nafasi ya tano, ikiuwa nyuma ya Arsenal.

Villas-Boas amesisitiza kuwa msimu ujao timu yake itafufuka na kuwa katika nafasi bora zaidi ya kufuzu katika michuano ya Klabu bingwa bara ulaya.
BBC SWAHILI

No comments:

Post a Comment