Thursday, May 30, 2013

Rais Tenga kuzindua kozi ya Makocha Jumatatu


RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodger Tenga anatarajia kuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa kozi ya makocha wa ngazi ya pili (Intermediate) itakayofanyika Jumatatu (Juni 3, 2013) kwenye Ukumbi wa Hobours Club, uliopo Kurasini jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Ufundi Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), Joseph Kanakamfumu, alisema Rais Tenga atakuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa kozi hiyo itakayohusisha amakocha 26.

Alisema kozi hiyo itakayomalizika Juni 28 itakuwa imewezesha kupatikana makocha watakaosaidia maendeleo ya mchezo huo katika Mkoa wa Dar es Salaam na Taifa kwa ujumla.

Aliwataja makocha wa kozi hiyo kuwa ni Shadrack Nsajigwa, Benard Mwalala, Steven Nyenge, Jemedari Said Kazumari, Zubeiri Katwila, Ibrahim Masoud ‘Maestro’, David William Ngaga, Idd Abushir Mwinchumu, Rajab Mohamed Nakuchema, Lubigisa Madata, Bakari Mahad, Greyson Swai, Chiwanga  A. Chiwanga, Sizza Mapunda na  Muhibu Kanu.

Wengine ni Omari Mbarouk, Omari Mohamed, Samuel Galafawo, Abdallah Mbogolo, Hassan Msonzo, Akida Said, Emanuel Gabriel, Barton Msengi, Edgar Method Katembo, Elly Kaiza na Renatus Benard.  



Kozi hiyo ni ya kwanza kuendeshwa na DRFA tangu kuingia kwa uongozi mpya wa chama hicho Desemba 12, chini ya Mwenyekiti Almas Kassongo.

Wengine walioingia madarakani katika uchaguzi huo uliofanyika kwenye Ukumbi wa Hoteli ya Mbezi Garden ni Meba Ramadhan (Makamu Mwenyekiti), Msanifu Kondo (Katibu), Muhsin Said (Mwakilishi wa Mkutano Mkuu wa TFF), Benny Kisaka (Mwakilishi wa Klabu), Ally Hobe (Mhazini) na Wajumbe wa Kamati ya Utendaji Mohamed Shabani, Sunday Mwanahewa na Bakari Mapande.

HAFIDH KIDO
kidojembe@gmail.com

No comments:

Post a Comment