Monday, July 15, 2013

Fabregas kutua Man U...


Klabu ya Manchester United imewasilisha ombi la kutaka kumsajili mcheza kiungo wa klabu ya Barcelona Cesc Fabregas.
Ripoti zinasema kuwa Manchester United inataka kumsajili mchezaji huyo wa zamani wa Arsenal kwa kitita cha pauni milioni ishirini na tano.
Wasimamizi wa Barcelona kwa sasa wanajadili pendekezo hilo, lakini inaaminika kuwa kiasi walichopendekeza ni kidogo.
Licha ya kuwa Fabregas hajaomba kuruhusiwa kuondoka, lakini kuna fununu kuwa huenda akashawishika kurejea tena nchini England.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26, huenda akakubali kujiunga na Manchester United ikiwa wasimizi wa Barcelona watakubali kiasi kilichopendekezwa na Manchester United.
BBC SWAHILI

No comments:

Post a Comment