Tuesday, July 9, 2013

UINGEREZA INAONGOZA KWA UWEKEZAJI TANZANIA.

 Bi Zamaradi, Naibu Mkurugenzi wa idara ya habari MAELEZO akimtazama Pendo Gondwe, Meneja uhusiano wa TIC wakati akizungumza na wanahabari leo.

Meneja huduma kwa wawekezaji Revocatus Abegas akijibu maswali ya wanahabari leo asubuhi.


Kituo cha uwekezaji Tanzania (TIC) kimetaja nchi kumi zinazoongoza kwa uwekezaji nchini Tanzania ambapo nchi iliyoongoza ni Uingereza yenye miradi 934 nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa idara ya habari MAELEZO jijini leo katika utaratibu wa wasemaji wa asasi za serikali kukutana na wanahabari, meneja uhusiano wa TIC Pendo Gondwe amesema wawekezaji wa kigeni wanaiingizia serikali fedha nyingi za kigeni na ajira kwa wazawa.
Akitaja nchi hizo kumi zenye miradi mingi nchini idadi yake kwenye mabano, Pendo alisema, “Nchi inayoongoza kwa uwekezaji nchini ni Uingereza yenye miradi (934), China (455), India (365), Kenya inashika nafasi ya tano ikiwa na miradi (455) lakini faida yake si kubwa kama India.
Aidha nafasi ya tano inashikiliwa na USA (218), Uholanzi (162), Afrika Kusini (208), wakati Canada inashika nafasi ya nane ikiwa na miradi (195), Ujerumani (146) na Italy inashika nafasi ya kumi ikiwa na miradi (86).
Kwa mujibu wa Pendo mwaka jana 2012 TIC869 kutoka mataifa mbalimbali iliyotoa ajira 174,000, iliyokuwa na faida ya dola za kimarekani milioni 11 elf.
Katika hatua nyingine ripoti ya kituo hicho inaweka wazi kuwa miradi iliyoongoza kwa kusajiliwa ni Kilimo, utalii, usafirishaji, majengo ya biashara na viwanda.
“Hiyo ndiyo miradi mitano iliyoongoza kwa mwaka jana, lakini idadi ya wawekezaji 869 mchanganuo wake ni kama ifuatavyo watanzania wamesajili miradi 450, wageni kwa ujumla wamesajili miradi 219 na miradi iliyosajiliwa kwa ushirikiano wa wenyeji na wageni ‘joint venture’ ni 192.
“Miradi yote hiyo imezalisha ajira 93,000 na miradi hiyo imeleta faida ya dola za kimarekani mil 8505,” alisema Pendo Gondwe meneja uhusiano wa TIC.
HAFIDH KIDO
9 Julai, 2013
DAR ES SALAAM, TANZANIA

No comments:

Post a Comment