Friday, September 5, 2014

China yaishawishi A.Kusini kumzuia Dalai Lama



                                                   Dalai Lama
 
Kiongozi wa kiroho wa Tibet, Dalai Lama, amesitisha ziara yake nchini Afrika Kusini ambako alitarajiwa kukutana na washindi wenzake wa tuzo ya Nobel,mjini Cape Town mwezi ujao.
Kiongozi huyo ambaye yuko uhamishoni, alisitisha ombi lake la Viza kuingia Afrika Kusini baada ya maafisa wake kusema kuwa huenda akanyimwa viza hiyo.
Serikali ya Afrika Kusini imekanusha madai ya kumnyima Dalai Lama Visa kutokana na shinikizo kutoka kwa China ambaye ni mshirika wake mkubwa wa kiuchumi.
China inamuona Dalai Lama ambaye hutetea haki za watu wa Tibet kama kiongozi hatari anayetaka kusambaratisha nchi hiyo.
Miaka miwili iliyopita mahakama ilisema kuwa Afrika Kusini ilikiuka sheria kwa kuchelewa bila sababu kumpa Dalai Lama Viza kuingia nchini humo.
kuchelewa huko kulimaanisha kwamba Dalai Lama asingeweza kuhudhuria sherehe za kuadhimisha miaka 80 ya rafiki yake mkubwa askofu mstaafu Desmond Tutu mjini Cape Town.
CHANZO: BBC SWAHILI

No comments:

Post a Comment