Tuesday, December 2, 2014

Jela miaka 50 kwa kuwaharibu watoto Kenya






NAIROBI, Kenya
Mahakama nchini Kenya imemhukumu kifungo cha miaka 50 jela raia mmarekani kwa kutengeza na kusambaza picha chafu za video za watoto wakifanya vitendo vya ngono.
Terry Ray Krieger alikiri makosa yake mbele ya mahakama mwezi jana. Pia alipatikana na kosa la kuwadhalilisha watoto wadogo huku akinasa vitendo hivyo kwa kanda ya video.
Alikamatwa na maafisa wa usalama Kenya baada ya kupata taarifa kutoka kwa shirika la kimataifa la polisi kwamba alikuwa anasambaza video hizo zilizokuwa zinaonyesha watoto wakifanyiwa vitendo vichafu kwenye mtandao.
Krieger amewahi kushtakiwa kwa makosa sawa na hayo na kufungwa jela nchini Marekani miaka 20 iliyopita.
Polisi wa Kenya walipokea taarifda kutoka kwa polisi nchini Marekanmi wakiwaamiwa kuwa kuna raia mmarekani nchini Kenya anayetengeza na kusambaza video chafu za watoto wadogo wakihishwa na vitendo vya ngono.
Aliomba mahakama kumuonea huruma kutokana na maradhi anayougua ya mifupa lakini mahakama ilisema kuwa maradhi yake sio haiwezi kuwa sababu ya kutowajibishwa kwa makosa yake.
Chanzo: BBC Swahili

No comments:

Post a Comment