Sunday, September 7, 2014

Mbowe awekewa pingamizi Uenyekiti Chadema.




Friday, September 5, 2014

China yaishawishi A.Kusini kumzuia Dalai Lama



                                                   Dalai Lama
 
Kiongozi wa kiroho wa Tibet, Dalai Lama, amesitisha ziara yake nchini Afrika Kusini ambako alitarajiwa kukutana na washindi wenzake wa tuzo ya Nobel,mjini Cape Town mwezi ujao.
Kiongozi huyo ambaye yuko uhamishoni, alisitisha ombi lake la Viza kuingia Afrika Kusini baada ya maafisa wake kusema kuwa huenda akanyimwa viza hiyo.
Serikali ya Afrika Kusini imekanusha madai ya kumnyima Dalai Lama Visa kutokana na shinikizo kutoka kwa China ambaye ni mshirika wake mkubwa wa kiuchumi.
China inamuona Dalai Lama ambaye hutetea haki za watu wa Tibet kama kiongozi hatari anayetaka kusambaratisha nchi hiyo.
Miaka miwili iliyopita mahakama ilisema kuwa Afrika Kusini ilikiuka sheria kwa kuchelewa bila sababu kumpa Dalai Lama Viza kuingia nchini humo.
kuchelewa huko kulimaanisha kwamba Dalai Lama asingeweza kuhudhuria sherehe za kuadhimisha miaka 80 ya rafiki yake mkubwa askofu mstaafu Desmond Tutu mjini Cape Town.
CHANZO: BBC SWAHILI

Ajali Mbaya Musoma.....



                                         Miili ya marehemu ikisubiri kutambuliwa.



                                                  Mabasi yaliyogongana leo
Basi la Jumanne lililokuwa linatoka Sirari kwenda Mwanza limegongana uso kwa uso na basi la Mwanza coach lililokuwa linatoka Mwanza kwenda Musoma. Ajali imetokea katika eneo la daraja la sabasaba, Musoma. 

Mpaka sasa inadaiwa zaidi ya watu 40 wamepoteza maisha huku wengine wameumia vibaya.
endelea kufuatilia zaidi... 

Ajali hiyo imehusisha basi la Mwanza coach lenye namba za usajili T 736 AWJ lililokuwa likitokea Musoma kwenda Mwanza na basi la J4 lenye namba za usajili  T 677 CYC likitokea Mwanza kwenda Sirari na gari dogo aina ya Land Cruiser ambayo namba zake  hazikuweza kufahamika mara moja kugongana uso kwa uso majira ya saa 5 asabuhi.
Akizungumza na Waandishi wa Habari kwa niaba ya Mganga Mkuu,Dakatari wa hospitali hiyo Martini Khani alisema kuna idadi kubwa ya maiti zilizopokelewa pamoja na majeruhi na idadi kamili ya vifo na majeruhi itfahamika baadaye.
Wakizungumzia tukio hilo mashuhuda wa ajali hiyo walisema mabasi hayo ambayo yote yalikuwa kwenye mwendo kasi yalikutana kwenye daraja dogo katika eneo hilo huku pia gari dogo aina ya Land Cruiser lililokuwa likitokea Musoma likitaka kulipita basi la Mwanza Coach hali iliyosababisha  kutokea kwa ajali hiyo.

ICC yaahirisha kesi ya Rais Kenyatta



                         Uhuru Kenyatta

Kiongozi wa mashitaka katika mahakama ya kimataifa ya ICC, Fatou Bensouda, ameiomba mahakama hiyo kuahirisha kesi ya Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta kwa muda usiojulikana.
Hii ni baada ya malalamiko kutoka kwake kuwa Kenya imekataa kushirikiana na mahakama hiyo katika kuikabidhi ushahidi unaohitajika kuendesha kesi kwa hiyo ina maana kuwa hana ushahidi wa kutosha dhidi ya Kenyatta.
Serikali ya Kenya ilitakiwa kuikabidhi mahakama taarifa za kifedha za Rais Kenyatta pamoja na maelezo kuhusu mali yote anayomiliki.
Katika uamuzi uliotolewa na mahakama hiyo Fatou Bensouda amesema kuwa hana ushahidi wa kutosha kumfungulia mashitaka Rais Kenyatta ambaye anadaiwa kuhusika na ghasia za baada ya uchaguzi mkuu nchini Kenya mwaka 2007.
Zaidi ya watu 1,000 walifariki katika ghasia hizo. Bensouda amenukuliwa akisema kuwa halitakuwa jambo la busara kufutulia mbali kesi hiyo hasa ikizingatiwa kuwa Kenya haitaki kutoa ushahidi unaohitajika na mahakama hiyo.
Badala yake aliomba mahakama kuiahirisha kesi hiyo hadi pale Kenya itakapokubali kutoa ushahidi unaohitajika.
Kesi dhidi ya Kenyatta ilipaswa kuanza mapema mwezi Oktoba.
CHANZO: BBC SWAHILI