Friday, September 5, 2014

Ajali Mbaya Musoma.....



                                         Miili ya marehemu ikisubiri kutambuliwa.



                                                  Mabasi yaliyogongana leo
Basi la Jumanne lililokuwa linatoka Sirari kwenda Mwanza limegongana uso kwa uso na basi la Mwanza coach lililokuwa linatoka Mwanza kwenda Musoma. Ajali imetokea katika eneo la daraja la sabasaba, Musoma. 

Mpaka sasa inadaiwa zaidi ya watu 40 wamepoteza maisha huku wengine wameumia vibaya.
endelea kufuatilia zaidi... 

Ajali hiyo imehusisha basi la Mwanza coach lenye namba za usajili T 736 AWJ lililokuwa likitokea Musoma kwenda Mwanza na basi la J4 lenye namba za usajili  T 677 CYC likitokea Mwanza kwenda Sirari na gari dogo aina ya Land Cruiser ambayo namba zake  hazikuweza kufahamika mara moja kugongana uso kwa uso majira ya saa 5 asabuhi.
Akizungumza na Waandishi wa Habari kwa niaba ya Mganga Mkuu,Dakatari wa hospitali hiyo Martini Khani alisema kuna idadi kubwa ya maiti zilizopokelewa pamoja na majeruhi na idadi kamili ya vifo na majeruhi itfahamika baadaye.
Wakizungumzia tukio hilo mashuhuda wa ajali hiyo walisema mabasi hayo ambayo yote yalikuwa kwenye mwendo kasi yalikutana kwenye daraja dogo katika eneo hilo huku pia gari dogo aina ya Land Cruiser lililokuwa likitokea Musoma likitaka kulipita basi la Mwanza Coach hali iliyosababisha  kutokea kwa ajali hiyo.

No comments:

Post a Comment