Friday, August 31, 2012

Tanzania is the first country in East Africa to use GSS... read more...


By Veronica Kazimoto – MAELEZO
Dar es Salaam
31/08/2012.
 
THE GOVERNOR of Bank of Tanzania Prof. Benno Ndullu has launched the enhanced Government Securities System (GSS) embedded with a book entry system so as to increase efficiency in the Government Securities auctions and Central Depository Operations.Prof. Ndullu has said that this Government Securities System will help to facilitate management of various risks, promote secondary market trading and liquidity optimization in the Real Time Gross Settlement System.“In quest of further development of the financial markets infrastructure, the bank found it imperative to enhance the GSS so that it conforms to international best practice and keeps pace with technological advancement.” the Governor said.
The system includes features such as on line bidding for government securities, electronic provision of standby facilities (Intraday and Lombard), unique identification of auction participants and electronic platform for repurchase agreements among others.
  Before this system, bidding and settlement of Government securities was done manually until in 1994 where a semi automated system known as Treasury Bills Information System (TBIS) was introduced and settlement was done using both cash and bankers drafts and physical certificates were being issued as evidence of ownership.
In 1999 the Bank introduced the Government Securities System embedded with a book entry system wherein securities were issued in paperless form with connectivity to the Real Time Gross Settlement System.
Reactions::

Bara la Afrika lanyemelewa na njaa...


Bei ya vyakula duniani ilipanda kwa asilimia kumi mwezi Julai na kusababisha hofu ya bei ghali ya vyakula barani Afrika.
Taarifa hii ni kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na benki ya dunia.
Ripoti hiyo imesema kuwa wimbi la joto lililokumba Marekani pamoja na ukame katika baadhi ya maeneo ya Mashariki mwa Ulaya ndio chanzo kikubwa cha kupanda kwa bei hizo.
Bei ya nafaka kama vile mahindi ,ngano na maharagwe ndio ilipanda pakubwa kulingana na ripoti hiyo.
Benki hiyo sasa imeonya kuwa nchi ambazo hununua nafaka kutoka nje ndizo zitaathirika pakubwa.
Kuanzia mwezi Juni hadi Julai mwaka huu, bei ya mahindi ilipanda kwa asilimia 25 wakati bei ya maharagwe aina ya soybean ikipanda kwa asilimia 17. Ni bei ya mchele pekee ilishuka kwa asilimia nne.
Nchini Marekani, ukame ulioripotiwa na kutajwa kuwa mbaya zaidi kuwahi kushuhudiwa katika miaka ya karibuni, ulisababisha uharibifu wa mahindi na maharagwe wakati nchini Urusi, Ukraine na Kazakhstan, ngano iliharibika sana.
Benki ya dunia pia imesema kuwa hatua ya kutumia mahindi kuzalisha mafuta inawezekana ni mojawapo ya sababu ya kupanda kwa bei ya mahindi nchini Marekani.
Nchi hiyo hutumia aslimia arobaini ya zao lake la mahindi kutengeza mafuta yanayotokana na mimea.
Kwa jumla, ripoti ya benki ya dunia kuhusu bei ya vyakula ambayo hufanyia utafiti bei ya vyakula duniani, iligundua kuwa bei ilipanda kwa asilimia sita zaidi mwaka huu ikilinganishwa na mwaka jana.
Chanzo: BBC Swahili.

Dr Slaa ajibu mapigo ya Sitta....


Na Said Ng'amilo Wa Mjengwablog,Iringa

Mh Samweli Sitta kwa maneno yake aliyotamka hivi karibuni kama ilivyo ripotiwa na vyombo vya Habari nchini. Dr alieleza hayoleo mbele ya waandishi wa habari mjini Iringa katika ukumbi wa M.R HOTEL Majira ya asubuhi alianza kwakukanusha uongo aliousema Mh Sitta kuwa katika Chama cha Demokrasia na Maendeleo hamna viongozi tishio ila ni Dr Slaa.Amemshangaa nakusema, ajuavyo yeye Hawezi kuwasemea akikanusha hayo pamoja na kumuita Mh mwenyekiti wa Chadema ni mchezesha disco katika nchi hii niuwongo ulio wazi. Tunavyojua MH Mbowe nimmiliki wa klabu ya burudani ambamo wapenzi wa mziki katika nchihii wanajua hivyo natena kunabaadhi ya Mawaziri ni wateja katika ukumbihuo.


Akimuelezea Mh Samweli Sita ni Muhaini wa kwanza katika nchi hii akiwa Spika wa Bunge la Jamuhuri la muungano wa Tanzania alizuia muswada uliopelekwa Bungeni na Mh Zito kabwe unaohusu Ufisadi katika makampuni yauma. Yakiwemo Meremeta nk.kinyume chake wakamfukuza Mh zito Bungeni kwa miezi sita na wakamrudisha kimyakimya.


Pia Mh sita nimwanzilishi wa chama cha CCJ katika nchi hii wakiwa na Mh Mwakyembe  kwa  lengo lakuhama CCM waliandika katiba kama ya CHADEMA wakiwa nadhamira ya kujaribu upinzani huku wakisema wakishindwa watajiunga na CHADEMA. Wakatihuo Sitta akifanya mawasiliano ya faragha maranyingi na Dr.Slaa  huku akijigamba kuwa ana  wa bunge wengi zaidi ya Hamsini atahama nao iwapo atakuja Chadema.


 kipindi cha uchaguzi wa Spika wa Bunge la Jamuhuri la Muungano CCM walipo badili utaratibu na kumtaka mgombea Mwanamke yeye alichukizwa nahilo. Nandio ulikuwa mwanzo wakutapatapa akijua muda wake wakudhani yeye ni Spika wakudumu. Kwani mfano tunao akiwa spika alijenga nyumba ya Spika Jimboni kwake kwa pesa ya Serikali yenye gharama kubwa zaidi ya mara kumi yakiwango kilicho pangwa cha kujengewa ofisi za wa Bunge katika kila jimbo. Nasiyo kama alivyofanya yeye. Dr Saa alisema tunayajua mengi yafanywayo na viongozi serikalini wanao toka CCM kwaleo nasema machache mengine ni akiba. kwakua natumia silaha sawa na wanyotumia maadui zetu.


Pamoja na hayo Chadema wamewashukuru Jeshi la Polisi na CCM Kwakuwa wamekuwa kama  makada wao kwani wamewafanya wawafikie wananchi wegi katika mkoa wa Iringa baada ya kusitisha Maandamano na Mkutano mpaka Sensa ipite wao wakaamua kwenda mtaa kwa mtaa kijiji kwa kijiji. kata kwa kata hivyo toka waanze wamefika vijiji Mia na  hamsini katika Wilaya ya Mufindi,(W)Iringa,Wilaya ya Kilolo pamoja na Iringa Manispaa ambapo watafanya Mkutano tar 9.9.2012 viwanja vya Mwembetogwa.


Picha na habari- Said Ng'amilo wa Mjengwablog, Iringa 

Wangapi mnakumbuka songombingo za kaboka mchizi?







Sensa ya mwaka huu imeleta mambo jamani khaaaa... hebu someni hii...





Jamani eeennhh leo jembe ijumaa nimesalia msikiti wa harakati...

Nimefurahishwa sana na hutba ya leo iliyotolewa na sheikh Hasheem Rusaganya, ilihusu husuda. Kumuonea mwenzio kijicho. Ilikuwa katika msikiti wa Mtambani Kinondoni B...

Jamani kweli uongozi mtamu, leo hii Amos Makala anakagua gwaride la heshima?

Huyu ni Amos Makala naibu waziri wa Habari na mbunge wa Kilombero akikagua gwaride la heshima kutoka kwa polisi jamii alipotembea jimbo lake mwnzoni mwa wiki hii...

Have you voted for your Country to get a place in Seven wonders of the World?ven Natural


Lets talk a deal, vote for Mount Kilimanjaro, the Ngorongoro Crater, and the Serengeti National Park so that they become among the New seven Natural Wonders of the World. Wake Up Tanzanians and make our country proud wherever we are. It is easy, submit your entries via e-mail: vote@sevennaturalwonders.org bearing the subject title "Tanzania" listing the names of the three entries, and not more than four other tourist attractions.



Mount Kilimanjaro


Mount Kilimanjaro is one of the largest stratovolcanoes in the world reaching 19,340 feet (5,895 m) into the air. As the tallest mountain in Africa, Mount Kilimanjaro is also the tallest free standing mountain in the world. Kilimanjaro is a composite volcano that includes layers of lava, tephra, and volcanic ash. The volcano is currently inactive with no known history of eruptions.
Mount Kilimanjaro has seven distinctive peaks with Uhuru Peak accounting for the mountains highest elevation at 19,341 feet (5,895 m). A 1.5 mile wide crater is featured as part of the Kibo portion of the mountain.
The high elevation and proximity to the equator allows visitors to experience a variety of climate types. Kilimanjaro also features a year round snow-topped peak. Although the volcano is isolated, it is part of the line of volcanoes that reach across northern Tanzania.


Ngorongoro Crater


Ngorongoro Crater is the world's largest unbroken caldera. Often referred to as "Africa's Garden of Eden," the crater is home to over 30,000 animals including elephants, lions, cheetahs, wildebeests, buffaloes, and the rare black rhinos. View Wildlife of Ngorongoro Crater to learn more about the wildlife and View Birds of Ngorongoro Crater to discover some of the many species that are found in the area.
Ngorongoro Crater was created from a volcano that exploded creating the caldera wilderness haven. The crater is 12 miles (19 km) across and consumes 102 square miles (264 sq km) of wilderness. The rim of the crater rises just over 2,000 feet (610 m) above the caldera floor reaching an elevation of 7,500 feet (2,286 m).



Serengeti Migration


The Serengeti migration is the longest and largest over land migration in the world. The Serengeti plains account for over 18,641 square miles and the migration itself travels 500 miles on the path from Tanzania to the Masai Mara Reserve in Kenya. Approximately 80% of the Seregeti plains are protected by the Tanzanian and Kenyan governments.
The Serengeti is home to over 70 larger mammals and approximately 500 different types of birds. Probably the most impressive part of the migration is the herds of wildebeests that blanket the plains. The migration will kill off around 250,000 wildebeests each year.
 Learn about about this on www.sevennaturalwonders.com

CCM wanaanza kukubali kiaina....


Color in the desert


MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya CCM, Samuel Sitta amekiponda Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), akidai kuwa muda wake wa kutawala nchi bado, kwa kuwa hakina viongozi wa kutosha wa kufanya kazi za Serikali ukimwondoa Katibu Mkuu wake, Dk Willibrod Slaa.

Sitta ambaye pia ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, alisema hayo jana alipokuwa akizungumza na baadhi ya viongozi wa CCM wa Wilaya ya Karagwe, Kagera, alikokuwa katika ziara ya kutembelea ofisi za CCM.


Alisema kuna upungufu mwingi katika safu ya uongozi wa chama hicho, kutokana na kutokuwa na watu wenye uzoefu wa kufanya kazi za Serikali, badala yake akidai kuwa kina baadhi ya viongozi wenye uzoefu wa kuongoza kumbi za muziki... “Wote hapa mnasikia kwamba Mwenyekiti wao, Freeman Mbowe ni mjuzi wa disko za usiku, sasa huwezi kulinganisha na CCM hata akitoka mtu mmoja chama chetu hakiwezi kuyumba.”


Dk Slaa na Mbowe hawakupatikana jana kuzungumzia kauli hiyo ya Sitta baada ya taarifa kueleza kuwa Mbowe yuko nje ya nchi na alikuwa hapatikani kupitia simu yake ya mkononi kama ilivyokuwa kwa Dk Slaa.


Hata hivyo, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe alipinga kauli hiyo akimtaka Sitta aachane na chama hicho kikuu cha upinzani na atumie muda wake kukijenga chama chake ambacho alidai kuwa kina makundi zaidi ya sita.

“Mwaka 2005 tuliweka mgombea Mbowe, mwaka 2010 tukamweka Dk Slaa, mwaka 2015 anaweza akarudi Mbowe, Dk Slaa au mwanachama yeyote wa Chadema,” alisema Zitto.

Alisema Chadema ni taasisi na si chama cha makundi kama ilivyo kwa CCM hivyo hakiwezi kumtegemea mtu mmoja... “Sitta asigombane na Chadema, ajenge chama chake ili tukutane mwaka 2015.”


Akizungumza na viongozi hao wa CCM Karagwe, Sitta alisema hakuna kiongozi mwingine anayeweza kufanya kazi ya kukiongoza Chadema na kukifanya chama kikubalike kwa umma.


“Hawa jamaa hawana hazina ya viongozi kama tulionayo CCM, ambapo tunaweza kusimamisha wagombea 20 wa urais wenye sifa zinazofanana tofauti na wao wanaye Dk Slaa tu ambaye inasemekana aliukimbia upadri.”


Kuhusu CCM

Akizungumzia chama chake, Sitta aliwataka viongozi wa CCM Mkoa wa Kagera kutokaa kimya na badala yake wajitoe na kujibu hoja za upinzani wanazozitoa kuikosoa Serikali iliyopo madarakani ili ionekane haijafanya mambo ya maendeleo tangu kupatikana kwa uhuru.

“Serikali ya CCM imefanikiwa katika maeneo mengi ya huduma za jamii kama elimu, barabara, afya na mawasiliano, sasa inashangaza kuona viongozi wa chama mnashindwa kufanya mikutano ya kuwaeleza wananchi mafanikio yanayotokana na utekelezaji wa sera na ilani ya chama chetu.”


Sitta aliwataka viongozi chama hicho nchini kuepuka mapambano na chuki miongoni mwao lakini akasisitiza kwamba kinaendelea na mkakati wake wa kuwaondoa viongozi wanaodaiwa kuwa ni mafisadi maarufu kwa jina la “magamba”.

Alisema chuki na mapambano yanayoendelea ndani ya chama hicho ndiyo yanayochangia kukidhoofisha na kuwapa la kusema wapinzani na hata kusababisha baadhi ya wanachama kukihama.

“Mapambano ndani ya CCM ndiyo chanzo cha migogoro na mitafaruku inayosababisha viongozi na wanachama wetu kuombeana mambo mabaya na kutoa mwanya kwa watu wetu kuhamia upinzani.”

Sitta yupo katika ziara ya siku tano ya kiserikali mkoani Kagera kukagua miradi mbalimbali inayohusiana na mwingiliano wa uchumi na kijamii kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).
Chanzo: http://www.mwananchi.co.tz

Mwanamitindo Mustafa Hassanali kukwea pipa... Kuenda Botswana.


Mwanamitindo mkongwe ndani ya Afrika anayetokea Tanzania Mustafa Hassanali amealikwa katika maonesho ya mitindo ya color in the desert yanayofanyika kuanzia tarehe 31 agost hadi tarehe 1 septemba ikiwa ni mara ya pili kufanyika nchini Botswana katika mji mkuu wa Gaborone. Akiwa ni mtanzania pekee aliyealikwa katika maonesho hayo ya mavazi yanayosifika Botswana  na Afrika kwa ujumla Hassanali anasema “ Nimefurahi sana na anajisikia fahari na heshima kuzindua toleo langu jipya la mtindo ikiwa ni la nne ndani ya mwaka huu na nategemea kutumia fursa hii kuutangaza utamaduni wetu na kuboresha urafiki uliopo kati ya Botswana na Tanzania”.

Toleo hili linaloitwa Pink Desert collection lina magauni yenye alama ya Mustafa Hassanali ikiwa ni pamoja na nguo za kiume ambazo ziko tayari kwa kuvaliwa na kuonesha umaridadi wa mbunifu huyo.


Toleo hili linatoka na kuzinduliwa ikiwa ni kipindi tunachoelekea mwezi oktoba ambao unajulikana duniani kote kuwa ni mwezi wa kuhamasishana dhidi ya ugonjwa wa kansa ya matiti.


‘”Nitatumia toleo hili la mitindo pia katika kuhamasisha na kuelimisha jamii kuhusiana na tatizo la ugonjwa wa kansa ya matiti ili kila mwanamke aweze kuwa na uelewa wa kujichunguza mwenyewe juu ya afya yake, sambamba na kupenda kuvaa nguo zenye rangi ya pinki kama kiashiria cha uelewa juu ya kansa ya matiti ugonjwa ambao unaathiri wanawake wengi.” Alimalizia Mustafa Hassanali.


Kwa mwaka 2012 Mustafa Hassanali ameshazindua matoleo matatu ya mavazi ambayo ni, Afrikalos aliyoonesha Nchini Nigeria (Lagos), Toleo la Harusi aliloonesha Tanzania (Dar es salaam) na toleo maalumu la mwezi wa Ramadhani liliooneshwa Dakar Senegal.


KUHUSU MUSTAFA HASSANALI 

Licha ya kuwa mbunifu pekee anayeongoza katika ubunifu wa mavazi ya jioni na harusi, Mbunifu nguli wa mavazi Afrika mashariki na kati Mustafa Hassanali anaichukulia fani yake ya ubunifu wa mavazi kama dini hata kufikia kuitwa mkongwe wa ubunifu wa mavazi barani Afrika.

Mustafa Hassanali amekwisha onesha ubunifu wake katika nchi 16 ulimwenguni na miji mikubwa 25 na pia ametajwa katika orodha ya wabunifu bora wa kiume kutoka Afrika ndani ya jarida la new African Woman la nchini uingereza, na pia alichaguliwa na waziri wa habari ,Vijana utamaduni na michezo kuwa katika kamati maalumu ya kutafuta vazi la taifa nchini Tanzania.


Ama kwa hakika Mustafa Hassanali ni mwenye kipaji maalum na asili cha ubunifu wa mavazi.

Kwa taarifa zaidi tembelea www.mustafahassanali.net
WASILIANA NA: DAVIS MWIJAGE.
SIMU: +255712847881
BARUA PEPE: davis@361tanzania.comi

Mikoani kuna mambo, hebu soma habari hii...


Kufuatia habari iliyochapishwa katika Gazeti la Majira la tarehe
29-08-2012, na mwandishi, Yusuph Mussa, Korogwe, DC wa Korogwe
aliyetamka maneno hayo
.

Mkuu wa Wilaya ya Korogwe mkoani Tanga, Bwana Mrisho Gumbo,
 
anatarajiwa kufikishwa kizimbani wakati wowote kwa madai ya
kumdhalilisha Mwanasheria wa Halmashauri hiyo Bi Najum Tekka.

Bi Tekka alifikia uamuzi huo baada ya Bwana Gambo kumwambia Shahada
 
yake ni ya nguo za ndani pamoja na kumuweka chini ya ulinzi wa polisi
ili ahojiwe bila kujua kosa lake.

Akizungumza na gazeti la MAJIRA jana, Bi Tekka alisema kutokana na
 
udhalilishaji huo, anatarajia kufungua kesi katika Mahakama Kuu Kanda
ya Tanga na kudaia fidia ya Sh 90 milioni.

Alisema Juni 14 mwaka huu Bwana Gambo alimwita kwenye kikao cha kamati
 
ya Ulinzi na Usalama cha Wilaya, ambacho kilifanyika ofisini kwake
ambapo kikao hicho, pia kilihudhuriwa na baadhi ya Madiwani pamoja na
viongozi wa soko la Manundu Mjini Korogwe.

Sababu ya kuitisha kikao hicho ilikuwa ni kutafuta muafaka kwa njia ya
 
mazungumzo ili kama tutakukubaliana na wafanyabiashara wa soko la hili
ambao wanapinga ongezeko la kodi ya vibanda kutoka 2,000/= kwa mwezi
hadi 20,000/= kwa mwezi ifutwe.

"Majibu yangu katika kikao hiki ndiyo yalimfanya Bwana Gambo
 
kunidhalilisha kwani mimi kama mwanasheria sina uwezo wa kuzungumza
kesi ambayo ipo mahakamani," alisema Bi Tekka.

Alisema baada ya kuzungumza maneno hayo Bwana Gambo alianza kusema,
 
"Huyu Mwanasheria Digrii yake ni ya Chupi, sina imani naye kabisa,
kesi zote za halmashauri anazisababisha yeye, hana msaada wowote
kwetu."

"Kimsingi amenidhalilisha mimi mwenyewe pamoja na taaluma yangu kwa
 
maneno aliyoyatumia, pia amenidhalilisha kwa kuniweka chini ya ulinzi
wa polisi ili nihojiwe wakati kosa langu mimi silijui hata mahakamani
sijapelekwa" alisema Bi. Tekka.

Bi Tekka alisema pamoja na kumpa bwana Gambo siku 14 awe amefuta kauli
 
yake kwa kuitisha kikao kama alichokiitisha awali bado alipuuza, mbali
na kushauriwa na wakuu wenzake wa wilaya.

"Nafungua kesi Kesho (jana) Mahakama Kuu kanda ya Tanga, ili aweze
 
kunilipa Milioni 90 kwa kunidhalilisha" alisema

Bwana Gambo alipofuatwa na MAJIRA alikiri kumualika Bi. Tekka kwenye
 
kikao hicho ili aweze kutoa ufafanuzi kwanini wameshindwa kufikia
muafaka na wafanyabiashara.

"Kabla ya hapo mimi niliwaita wafanyabiashara wakakubali kwenda kufuta
 
kesi, lakini huyu mwanasheria sijui ana maslahi gani na kesi hii,
tulishafikia mwafaka na waende mahakamani kuifuta lakini walipofika
akawakimbia. Hadi sasa kesi haijafutwa lakini wafanyabiashara
wamekubali kulipa sh. 10,000/= badala ya sh.20,000/=, kweli aliandika
notice ya kuomba radhi kwa kumdhalilisha lakini nilimwambia aende
mahakamani hata leo, tutakwenda kupambana " alisema Gambo.

Bwana Gambo alipongeza kuwa, kama Bi.Tekka anadai alidhalilishwa,
 
mbona hakuandika madai hayo polisi badala yake anakaa na watu wake na
kudai amedhalilishwa?

Mwandishi: Prosper R Mushi

Hapo jee... siasa yetu umekua ama?


Thursday, August 30, 2012

Je Dunia imepuuza hali ya Mali, watu wanavyouwawa?


Mjumbe maalum wa umoja wa mataifa wa haki za binadamu Valerie Amos amesema kuwa dunia imeshindwa kuwajibikia hali ya hatari kwa usalama wa raia wa Mali, ambako zaidi ya watu nusu milioni wametoroka makwao kutokana na vita.
Bi Valerie Amos, ambaye amekuwa akizuru kambi za wakimbizi ametoa wito wa msaada zaidi na ufadhili kuongezwa baada ya jamii ya kimtaifa kukusanya tu nusu ya pesa zinazohitajika kukabiliana na hali nchini humo.Tangu hapo, wapiganaji wa kiisilamu wa kabila la Tuareg wameteka maeneo ya kaskazini mwa Mali.Bi Amos yuko katika ziara ya siku tatu nchini Mali kujionea hali na athari za mzozo baada ya mapinduzi ya kijeshi mwezi Machi.
Mwandishi wa BBC David Loyn, ambaye yuko katika msafara wa Amos, anasema kuwa mzozo huo umeathiri pakubwa nchi hiyo na kufanya rasilimali kuwa dunia kabisa.
Juhudi za kutoa msaada katika eneo la kaskazini zimeathirika kutokana na mapigano.
Bei ya juu ya vyakula pamoja na kipato cha chini zimesababisha hali ngumu kwa wananchi wa Mali.
Serikali mpya ya muungano, iliundwa katika mji mkuu Bamako,mwishoni mwa wiki ikiahidi kuleta mageuzi na utahibiti katika maeneo ya kaskazini mwa nchi.
Wapatanishi kutoka muungano wa nchi za magharibi ECOWAS, wamefanya mazungumzo na wapiganaji hao, na hata kupeleka wanajeshi elfu tatu nchini Mali ikiwa ni sehemu juhudi za amani hazitazaa matunda.
Wapiganaji wa Tuareg waliteka eneo la kaskazini baada ya rais Amadou Toumani Toure kupinduliwa mwezi Machi.

Haya sasa kama una ndugu yako anasoma Uingereza jiandae kuenda kumpokea...



Zaidi ya wanafunzi 2,000 nchini Uingereza huenda wakarudishwa nchi zao za asili, baada ya leseni ya chuo kikuu cha London Metropolitan kudhamini na kutoa mafunzo kwa wanafunzi nje ya mataifa ya muungano wa Ulaya wa EU kufutiliwa mbali.
Idara ya serikali inayohusika na kuwazuia wageni wasio halali kuingia Uingereza, UK Border Agency (UKBA), imeelezea kwamba chuo kikuu cha London Metropolitan, kimeshindwa kufuatia suala la ikiwa wanafunzi kweli huwa wanafika darasani au la, na wengi wao hawana hata vibali vya kuwa nchini Uingereza.
Kutokana na hayo, chuo hicho kikuu hakitakuwa tena na mamlaka ya kuidhinisha visa kuwaruhusu wanafunzi kuingia Uingereza.
Chuo hicho kimekanusha madai ya UKBA, na kimeelezea kwamba kisheria kitachukua hatua.
Kamati maalum imeanzishwa ili kuwasaidia wanafunzi ambao wataathiriwa na hatua hiyo, ambayo huenda ikawalazimisha zaidi ya wanafunzi 2,000 kutoka mataifa mbalimbali, kufanya juhudi zaidi katika kutafuta wadhamini wapya, na vile vile vyuo vingine, la sivyo, warudishwe nyumbani.
Serikali imeelezea kwamba ingelipenda kukadiria idadi kamili ya wanafunzi ambao watajiunga na vyuo vingine, kabla ya kuwaamrisha watakaosalia, kuondoka nchini Uingereza chini ya muda wa siku 60.
Hata hivyo, wizara ya mashauri ya ndani ya Uingereza kwa sasa imeelezea kwamba haiwezi kuthibitisha ni lini itatoa tangazo la kuwataka baadhi ya wanafunzi hao kuondoka nchini.
UKBA imeelezea kwamba chuo kikuu cha London Metropolitan kimeshindwa "kuangazia mara kwa mara baadhi ya masharti muhimu" katika kipindi cha miezi sita iliyopita.
Waziri wa uhamiaji Damian Green alisema chuo hicho kimeshindwa kutimiza wajibu wake katika masuala matatu muhimu:
Zaidi ya robo ya wanafunzi 101 waliokaguliwa hawana vibali vya kuishi Uingereza.
Wanafunzi kati ya 20 hadi 50 ambao faili zao zilichunguzwa "hamna ushahidi thabiti" kwamba walikuwa na viwango vya kuridhisha kwa upande wa lugha ya Kiingereza.
Na wanafunzi 142 kati ya 250 (asilimia 57), haikuwezekana kuthibitisha kama walikuwa wakifika darasani au la, na kwa hiyo chuo kikuu hakina utaratibu thabiti wa kutambua kama kweli wanafunzi hao walikuwa wakiendelea vyema na masomo.
Chanzo: BBC Swahili.

Have you heard about this?


Yet another African big shot is dead and gone to his grave. And it is the controversial and assertive Meles Zenawi, who was officially Ethiopia’s Prime Minister.
 
Zenawi, died aged 57 on Monday August 20, in a hospital abroad after months of illness, government officials have said. Details of what killed him are not yet known.
Hailemariam Desalegn, Deputy Prime Minister and who also acts as the country’s foreign minister, has been named as acting head of government.
 
The former PM’s death comes some eight months after going out of the public domain, amidst speculation and concerns over what could have possibly led to his sudden silence.
 
The speculations heightened when he was missing in action at the African Union summit held in the Ethiopian Capital of Addis Ababa last month.
 
“The premier had been receiving medical treatment abroad for the past two months and his health was improving, but due to a sudden infection which occurred on Sunday, he went back to hospital for emergency treatment, and even if a lot of medical attention was given by his doctors, he died yesterday Monday at around 23:40,” a statement from the Ethiopian government read.
 
Appreciated and detested in equal measure, and also called names including one which likened him to a “devil incarnate”, (by Commander Assefa Seifu) Meles, who took power in 1991 “as the leader of rebels that ousted communist leader Mengistu Haile Mariam in 1991 and led the country's economic transformation,” was to most Ethiopians, a Prime Minister who had the country at heart.
 
The West loved him as much as they liked his stance against Islamist extremism, having fought the Al Shabab Islamist groups in Somalia. On two occasions, he had reason to send troops to Somalia to fight the group, which is said to be connected to Al Qaeda.
 
In a tribute to Zenawi, the United Kingdom’s David Cameron says he was “an inspirational spokesman for Africa”.
 
Despite leading Ethiopia to unprecedented economic growth in the past half decade, it wasn’t all rosy for Zenawi as he had to account and explain reasons why his style of governance saw so much repression and disrespect for basic human rights.
 
A typical example is the 2005 post election incidents that saw a defiance of human rights; where about 200 people lost their lives. This is still fresh on the minds of his critics.
 
As tough as he was, Zenawi always found very subtle ways to explain his side of an issue, and be it as it may that he had the backing of the West in certain areas, he was in most instances hailed as the “King” and the man, who can’t go wrong.
 
The United States government for instance, liked him.  Under his rule, Ethiopia received hundreds of millions of dollars in aid. Some have said, the support from the U.S was also a way of showing appreciation to his (Zenawi) government for occasionally hosting the US military drones that patrolled parts of East Africa.
 
An intelligent peace broker who was very instrumental in the search for a lasting solution to the problems the newly independent South Sudan and Sudan had, Zenawi duly served his people well.
Often considered controversial, Zenawi is said to have at a point, referred to the Ethiopian flag as “just a piece of rag”.
Here are some of his all-time quotes.
“I am Yemeni. I know myself to be a Yemeni. We are Yemenis. Apart from the royal family, Ethiopians are Arabs”.
Ethiopia is only 100 years old. Those who claim otherwise are indulging themselves in fairy tales”.
“I have no problem talking to anybody so long as it helps the purpose of peace”.
 
“What we have is a pattern of prevarication, a pattern of trying to draw out the process and consolidate the hold on our territory, if that's the case –and it appears to be the case – then the opportunities for resolving this problem peacefully could be fast disappearing”.
 
“I don’t know what the prosecution will ask for but the death penalty is still legal in Ethiopia. On a personal note that is not the penalty I would like to see applied. It is for the prosecution and courts to decide, but if I have any say on it I would prefer prison sentences rather than death sentences”.
 
“What we have detained are people who have tried to overthrow the duly constituted government, and that in my view is treason under the laws of the country”.
 
“The violence has marred the image of Ethiopia. The worst is clearly behind us and we do not expect any such violence in the near future”.
 
“We have no intention of playing fast and loose with this document, with the OAU process. We only hope that this time around the other side really means what it says”.
 “What the implications of this will be in terms of relations between Ethiopia and the EU we will have to wait and see. But I don't think you will be surprised if Ethiopia were to insist that it should not be patronized”.

“The only forces we are pursuing are Eritreans who are hiding behind the skirts of Somali women”.


Hatimae KomandooSalmin akumbukwa kutoka mafichoni...


Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) Profesa. Idris Ahmada Rai (kushoto) akimkabidhi Shahada ya uzamivu (PHD)  ya heshima ya Chuo Kikuu hichoc, Rais mstaafu wa awamu ya tano wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Dk. Salmin Amour Juma nyumbani kwake Migombani mjini Zanzibar. Kulia ni mjumbe wa Baraza, Mohammed Said Dimwa.

Picha kwa hisani ya amanitanzania.blogspot

Hili jembe langu Abdallah James aka Piero aka Kiduchu aka D salut aka jembeeeeee

Huyu ni rafiki yangu wa karibu sana hatujaonana kwa kipindi kirefu yapata miezi sita. Leo amenitembelea nyumbani jioni, tukazungumza mambo mengi sana ambayo nahitaji kuwaeleza hata nyinyi.

Abdallah ametoka Soni kijiji cha wasambaa mkoani Tanga, alikuwa mwalimu lakini katika maisha yake hajawahi hata kusomea japo kozi ya siku moja ya ualimu. Alikuwa anaganga njaa ama kwa maneno yake alikuwa anafukuza upepo.

Ni maisha fulani hivi magumu yasiyo na muelekeo, nilisoma nae kidato cha nne katika shule ya kiislam Masjid Qubah mwaka 1999 mpaka 2002. Sote tukahangaika mpaka tukamaliza shahada mojamoja za chuo kikuu, yeye alisomea shahada ya rasilimali watu mimi nilisomea shahada ya mawasiliano ya umma.

Lakini mpaka sasa hakuwa amepata kazi ya maana, nami kadhalika. Akaniambia sababu ni kuwa sisi hatuna mitandao (connection) ambayo itatuwezesha kujuana na watu ambao watatupa mawazo na fikra mbadala. Abdallah na rafiki yetu mwingine anaitwa Juma Mwiroma walianzisha kampuni ya kupokea tenda za kusambaza vifaa vya kompyuta, lakini waliamua kuifunga kampuni hiyo baada ya kukosa connection kutoka kwa watu.

Hili limekaaje wadau?

Lakini nashukuru leo Abdallah amekuja na habari njema,amenambia amekimbia kule kijijini na amepata kazi Bagamoyo katika hotel, anaweza kuenda kuripoti kazini muda wowote kuanzia leo.....

Mbuyu Twite amkebehi Mwenyekiti wa Simba Aden Rage kwa kuvaa jezi ya Yanga ikiwa na jina lake leo...


Na Mahmoud Zubeiry
BEKI mpya wa Yanga, Mbuyu Twite ametua Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere na kulakiwa na mamia ya wapenzi wa klabu hiyo, kabla ya kupakiwa kwenye gari kuelekea makao makuu ya klabu, makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani, Dar es Salaam.
Hakuna kiongozi yeyote wa Simba wala askari polisi aliyemsogelea kama ambavyo kulikuwa kuna tishio kwamba akitua tu beki huyo wa kimataifa wa Rwanda, mwenye asili ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) watamkamata kwa tuhuma za kuwatapeli dola za Kimarekani 30,000.
Inadaiwa, kabla ya kusaini Yanga, Twite aliyekuwa akichezea APR ya Rwanda alisaini Simba na kuchukua dola 30,000.
Hata hivyo, baadaye mchezaji huyo alighairi na kuamua kwenda Yanga na kurudisha fedha za Simba kupitia viongozi wa APR na St Eloi Lupopo ya DRC, ambazo zilikuwa zinammiliki kwa pamoja mchezaji huyo.
Lakini viongozi wa Simba waligoma kupokea fedha hizo ingawa viongozi wa APR na Lupopo walifika hadi ofisi za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kutaka kuzikabidhi fedha hizo, ili Simba wakazichukulie hapo.
Twite aliianza kuichezea Yanga wiki iliyopita ilipokuwa Kigali, Rwanda kwa ziara ya wiki moja lakini alishindwa kurejea na wenzake Jumatatu kwa kile kilichoelezwa anakamilisha kuhama kwake rasmi na kuja kuanza maisha mapya Dar es Salaam,
Lakini upande wa pili, Simba SC waliamini beki huyo amekwepa kukamatwa kufuatia kuvuja kwa habari za mpango wa kumtegea akitua nchini wamkamate.
Ametua na amekwenda Jangwani, maana yake jaribio la kumkamata akitua limefeli na sasa tusubiri kama Simba watamuwekea mtego mwingine.
 Picha zote na habari kwa hisani ya bongostaz.blogspot.com