Sunday, April 13, 2014

Uchaguzi Guinea Bissau



Raia wa Guinea Bissau kuchagua rais mpya

Bissau, Guinea-Bissau
Ni uchaguzi wa Kwanza tangu kufanyika kwa mapinduzi miaka miwili iliopita -ikiwa ni hatua ya hivi karibuni ya kijeshi ambayo imesaidia kuhakikisha kwamba hakuna raisi aliyechaguliwa ambaye amefanikiwa kuiongoza Guinea Bissau kwa kipindi chote alichochaguliwa tangu taifa hilo lijipatie Uhuru wake kutoka kwa Ureno mnamo mwaka 1974.
Kiongozi wa mapinduzi hayo Antonio Indjai aliikabidhi mamlaka serikali ya raia mnamo mwaka 2012 iliopewa wajibu wa kuandaa Uchaguzi huo.
Indjai alifunguliwa mashtaka nchini marekani kwa madai ya kufanya biashara ya mihadarati pamoja na kuwauzia silaha waasi wa Colombia.Wagombea 13 wanawania wadhfa wa urais.
Iwapo mmoja wao hatashinda kwa wingi wa kura basi uchaguzi huo utaenda kwa awamu ya pili mnamo mwezi May.


Marekani yaionya Urusi kuhusu Ukraine.

Kiev, Ukraine

Marekani imeonyesha wasiwasi wake kuhusu kile ilichokitaja kama harakati za kundi fulani linalotaka kujitenga ambalo limekuwa likisaidiwa na Urusi kuchochea ghasia mashariki mwa Ukrain.
Kufuatia kutekwanyara kwa vituo vya polisi katika miji kadhaa ya mashariki mwa Ukrain ,waziri wa maswala ya kigeni nchini marekani John Kerry amesema kuwa mashambulizi hayo ya watu waliojihami na silaha za Urusi yalifanyika kwa mpangilio.
Katika mazungumzo yao ya simu na waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov,Kerry ameitaka Urusi kusitisha mashambulizi kama hayo la sivyo ikabiliwe na vikwazo zaidi.
Urusi imeonya kuwa utumiaji wowote wa nguvu nchini Ukrain utahujumu harakati za kidiplomasia kumaliza mgogoro huo.


Boko Haram ladaiwa kuwaua watu laki moja

Abuja, Nigeria
Sasa imebainika kuwa wanamgambo wa kiislamu kazkazini mwa Nigeria wamewaua zaidi ya watu laki moja na arubaini na tano katika misururu ya mashambulizi juma lililopita.
Sineta wa jimbo la kazkazini mashariki la Borno Ahmed Zannah ameiambia BBC kwamba mauaji hayo yalifanyika katika maeneo matatu tofauti yaliopo mashambani.
Amesema kuwa taassi moja ya kutoa mafunzo ya elimu ndio iliokuwa ya kwanza kulengwa ambapo wanamgambo hao waliwaua walimu watano kabla ya kuwatekanyara wake zao kadhaa.
Wapiganaji hao wanaoshukiwa kutoka katika kundi la wanamgambo wa Boko haram baadaye walivamia vijiji viwili katika eneo la mashambani karibu na mpaka na Cameroon.

Chanzo: BBC Swahili

No comments:

Post a Comment