Ligi kuu ya Tanzania bara, maarufu
kama Ligi Kuu ya Vodacom inaanza rasmi mzunguko wa pili leo, Ijumaa
baada ya kusitishwa tangu Novemba 7, 2014.
Hadi ligi hiyo
ilipositisha mzunguko wa kwanza, tayari timu 14 zinazoshiriki ligi hiyo
zilikuwa zimecheza michezo saba kila moja. Kwa mujibu wa ratiba
iliyotolewa na Shirikisho la Kandanda nchini Tanzania, TFF, Simba ambayo
ni miongoni mwa timu kongwe za ligi hiyo na ambayo katika mzunguko wa
kwanza haikuwa na matokeo mazuri baada ya kwenda sare mara sita na
kushinda mchezo mmoja na kujikusanyia pointi tisa ikishika nafasi ya
saba katika msimamo wa ligi hiyo, leo inaikaribisha Kagera Sugar
inayoshikilia nafasi ya tano katika pambano litakalofanyika Uwanja wa
Taifa jijini Dar es Salaam.
Michezo mingine itafanyika katika viwanja mbalimbali kuanzia Ijumaa, Jumamosi na Jumapili wiki hii. Mpaka sasa Mtibwa Sugar ndiyo
inayoongoza ligi hiyo ya Vodacom baada ya kujikusanyia pointi 15,
ikifuatiwa na Young Africans(Yanga) kwa kuwa na pointi 13 sawa na Azam
mabingwa watetezi.
Mbeya City iliyotikisa msimu uliopita na kupata
mashabiki wengi nchini Tanzania, imejikuta ikizibeba timu zote baada ya
michezo saba ikiwa na pointi tano tu ikitanguliwa na timu za Ndanda na
Tanzania Prisons zenye pointi sita kila moja. Hata hivyo mzunguko huu wa pili
utakuwa na kivutio cha aina yake baada ya timu hizo kuruhusiwa kusajili
katika dirisha dogo, ambapo Simba imeweza kusajili wachezaji wapya
ndugu mahiri kutoka Uganda kina Sserunkuma.Nao wapinzani wao wa
jadi Yanga, imemtimua aliyekuwa kocha wake kutoka Brazil Marcio Maximo
baada ya kufungwa mabao 2-0 na Simba katika mchezo wa Nani Mtani Jembe.
Pia Yanga imesajili wachezaji mahiri akiwemo Amisi Tambwe ambaye katika
mzunguko wa kwanza alichezea timu ya Simba lakini akaenguliwa katika
usajili wa dirisha dogo.
Kinachosubiriwa na wapenzi na mashabiki wa timu hizo ni kwa kila timu kupata ushindi, kufikia ubingwa.
No comments:
Post a Comment