Sunday, December 15, 2013

Tunisia yapata Waziri Mkuu



           Mehdi Jomaa alikuwa waziri wa viwanda hadi alipoteuliwa kama waziri mkuu.

Wanasiasa nchini Tunisia wamefikia makubaliano kuhusu waziri mkuu mpya baada ya mazungumzo kati ya chama tawala cha Ennahda na upinzani.
Mehdi Jomaa, waziri wa viwanda, ataongoza serikali ya mpito hadi uchaguzi utakapofanyika mwaka ujao.
Jina la Bwana Mehdi lilikuwa moja kati ya majina ya watu sita walioteuliwa kushikilia wadhifa huo katika mazungumzo yaliyofanyika siku ya Jumamosi.
Mgogoro wa kisiasa Tunisia umekuwa ukitokota tangu kuuawa kwa wanasiasa wawili wakuu mapema mwaka huu.
Uteuzi huo ni sehemu ya makubaliano yaliofikiwa Alhamsi ambapo wanasiasa waisilamu wenye msimamo wa kadri watakabidhi mamlaka ili kumaliza mgogoro huo wa kisiasa.
Mauaji ya mwanasiasa Chokri Belaid mnamo mwezi Februri na mwenzake wa upinzani Mohammed Brahmimwezi Julai yalicochea maandamano dhidi ya serikali.
Chama cha Ennahda kililaani mauaji hayo. Lakini upinzani umekituhumu kwa kukosa kuwachukulia hatua wanasiasa waisilamu wenye itikadi kali ambao huenda walihusika na mauaji hayo.
Mgogoro wa kisiasa uliofuata mauaji hayo, umetishia kusambaratisha kipindi cha mpito ambacho kilianza baada ya maandamano ya kiraia yaliyopindua serikali ya aliyekuwa Rais Zine al Abidine Ben Ali mwanzoni mwaka 2011.
Chanzo: BBC Swahili
 

No comments:

Post a Comment