Saturday, June 30, 2012

Madaktari bingwa watoa tamko


Mkutano wa Madaktari bingwa jana MNH, MUHAS NA ORCI  umeamua kuungana rasmi na madaktari wote nchini katika mgomo na kusitisha utoaji wa huduma zote zikiwemo za dharura Pia wanatoa wito kwa madaktari bingwa wengine kote nchini kuungana katika mgomo huu.

Pia wanalaani vikali vitisho na manyanyaso yanayofanywa na vyombo vya dola (serikali) dhidi ya madaktari na wameitaka serikali kutoa tamko la kuwahakikishia usalama madaktari kote nchini.

Pia kuna haja ya kuweka uwezekano wa kumsafirisha Dr. Ulimboka kwenda nje ya nchi kwa ajili ya uchunguzi na matibabu zaidi; hivyo zinahitajika $40,000(sawa na takribani tsh milioni sitini na nane 68000000),mpaka sasa madaktari wamechangisha Tsh mil 40..

Na njia nyingine zote za uchangiaji pesa zimesitishwa na kupendekeza zitumike namba za mawakala zifuatazo Voda 31915 na Tigo 054.

No comments:

Post a Comment