Friday, June 29, 2012

tigo imewakumbuka wateja wake coco beach kesho


Na Hafidh Kido

Tigo imejipanga kuwapa burudani wakaazi wa jiji la Dar es Salaam siku ya jumamosi na jumapili mwishoni mwa wiki hii katika fukwe za coco beach. Lengo likiwa ni kuwaandaa watumiaji wa tigo na sikukuu ya sabasaba.

Akizungumza na wanahabari katika hoteli ya serena leo asubuhi afisa habari wa kampuni hiyo ya mawasiliano bi Alice Maro, amesema kampuni yake imeamua kuwapa burudani nyingi watumiaji wa mtandao huo lengo likiwa ni kuwa nao karibu na kufahamiana zaidi.

“Mwaka huu tumeamua kuwaletea burudani nyingi za kutosha, hatutotaka wateja wetu waje tu kufurahi mwisho wa wiki hii ila tungependa pia wapate fursa ya kupata huduma zetu bora na nafuu zilizoandaliwa kwa ajili yao.”

Aidha tigo katika kunogesha shughuli hiyo waeamua kuonyesha fainali za mpira wa miguu za ulaya kati ya Italy na Hispania siku ya jumapili, sherehe hizo zitasindikizwa na wasanii maarufu watakaokonga nyoyo za wapenzi wa muziki wa kizazi kipya hasa pale wasanii mahasimu Izzo B pamoja na Roma Mkatoliki watakapopanda jukwaa moja siku hiyo.

“Kilele cha maadhimisho hayo kitakuwa ni siku ya jumapili na burudani kutoka kwa Juma nature, Roma mkatoliki, izzo B, Professor J, Mwasiti, Barnabas, Fid Q, Joe Makini na burudani maalum kutoka kundi la vichekesho la “Ze Comedy,” alisema Alice.

Tigo ni mtandao wa kwanza wa simu za mkononi Tanzania ulioanza biashara mwaka 1994, na ni mtandao wenye ubunifu wa hali ya juu na bei nafuu kupita zote nchini unaotoa huduma katika mokoa yote 26 Tanzania bara na visiwani. Ingawa katika siku za hivi karibuni kumekuwepo na malalamiko ya mitambo ya mtandao huo kutokuwa mizuri wakati wa mawasiliano.


No comments:

Post a Comment