Thursday, June 20, 2013

Unawajua hawa? Miguu yao ilipeleka ubingwa wa soka Mkoani Tanga mwaka 1988.

                                                                   Aggrey Chambo.



Aggrey Chambo, miongoni mwa vifaa vilivyosaidia kupeleka heshima ya soka mkoani Tanga alikuwa mzuri katika kuchungulia nyavu.

Itakumbukwa goli lake la kusawazisha dhidi ya Miembeni kombe la muungano msimu wa 1988/89 ndilo lililotupa nafasi ya pili nyuma ya African Sports na kutupatia ticket ya kushiriki kombe la washindi barani Africa na kutolewa na Ferraviaro ya msumbiji.

Hussein Mwakuluzo anaeleza kuwa "Hiyo mechi na miembeni naikumbuka vizuri sana, nilicheza mechi nikiwa na malaria, zikiwa zimesalia dakika tano mpira kwisha nikawa siwezi kuendelea na mechi, ndiyo nikatoka akaingia Aggrey! Mpira wa kwanza alioupata akampiga kanzu Riffat Said akafunga goli."

Mwakuluzo anaongeza kuwa "Nakumbuka mechi hiyo ilikuwa na ushindani sana nakumbuka nilibaki na Riffat Said, mara kadhaa na zote aliokoa, mwaka uliofuata Riffat akasajiliwa na Coastal Union."

Jina jingine la Aggrey aliitwa Mkombozi, kwasababu alikuwa akiingia lazima abadili matokeo, Ally Kiraka anasema "Nakumbuka mechi na Simba uwanja wa Mkwakwani Mohammed Mwameja ndiyo amesajiliwa Simba, mechi hii Aggrey alibishana sana na Mwameja na hiyo mechi ilikua na vurugu sana nje ya uwanja mpaka ndani ya uwanja.

"Tulipata penati Kassa Mussa kwa presha akakosa ndipo 'Mkombozi' Aggrey Chambo akasawazisha tukatoka suluhu na Simba ya 1-1 tukawatibulia ubingwa wao ndipo vurugu kubwa watu wa 'sweat corner' wakapigana na wachezaji wa simba pamoja na washabiki wao. Buma, alipigana na watu kama 10 ila alikua na nguvu ndiyo siku tuliyovunja undugu na Simba."

Kudhihirisha ukombozi wake Aggrey Chambo katika mechi dhidi ya African Sports, Mombasa Stadium alikomboa goli halafu Juma Mgunda akafunga goli la kuongoza mpaka mpira unaisha Coastal Union 2 African Sports 1, ilikua ni kwenye sherehe za Uhuru wa Kenya mwaka 1990 timu zote zilialikwa.

Kwa sasa legend huyu Aggrey Chambo anasumbuliwa na maradhi, mwili wake ni dhaifu sana, kwa sasa mtu pekee anayemsaidia ni golikipa wa zamani wa Coastal Union, Simba na timu ya Taifa Mohammed Mwameja ambaye ametoa pesa katika hoteli mojawapo eneo la karibu analoishi Chambo jijini Dar es Salaam ambapo anapata chakula kila siku.

Ukijisikia kumsaidia kwa hali na mali piga namba hizi 0714392601 ukipiga atapokea kijana mmoja anaitwa Uledi ndiye anayekaa na Aggrey, useme nataka kuongea na Aggrey ataitwa maana hana simu.

                                                                Yassin Abuu Napili



Abuu Yassin Napili, mchezaji wa zamani wa Coastal Union ambaye alijulikana kwa jina maarufu Valmet au kumbakumba kutokana na kujaaliwa mwili mkubwa wenye nguvu. Alikuwa beki mzuri enzi za kucheza kwake soka.

Kutokana na nguvu alizojaaliwa kuna mechi katika uwanja wa Mkwakwani dhidi ya watani wa jadi kutoka barabara ya 12 African Sports, Napili aliupiga mpira mpaka ukapasuka. Wengi wanaamini kilikuwa ni kitendo cha bahati nasibu, wengine wanaamini ilikuwa uchawi na wapo wanaoamini ni uwezo na nguvu za miguu.

Hussein Mwakuluzo anasema wakiwa kambini walikuwa wakimuita Napili kwa jina la utani la Garagaregwa kwa namna alivyokuwa na uchungu na mpira hataki utani mpaka mazoezini mipira yote ya adhabu ndogo anataka kupiga yeye. Na kitu cha kuchekesha Ally maumba naye alikuwa anapenda kupiga mipira iliyokufa 'adhabu' ikawa ugomvi baina ya Maumba na Napili.

Mchezaji huyu anahitaji heshima ya hali ya juu, maana Coastal Union baada ya kupata ubingwa mwaka 1988 wachezaji wazuri wote walipata soko nchi za Kiarabu, kipindi hicho Arabuni kulikwenda wachezaji wengi kutoka Afrika Mashariki. Lakini aliporejea miaka ya tisini yeye akiwa na Hilal Hemed, Juma Mgunda waliamua kujiunga tena na kikosi kijabahatika kupanda ligi kuu lakini baada ya msimu mmoja timu ikashuka.

Mwaka 2007 ikapanda tena lakini msimu huo huo ikashuka tena mpaka ilipopanda mwaka 2010 ambapo ilirudi kwa kishindo ikashiriki ligi kuu msimu wa 2011/12 na kushika nafasi ya tano, halafu msimu ulioisha wa 2012/13 imeshika nafasi ya sita.

Chanzo: COASTAL UNION Blog



No comments:

Post a Comment