Monday, November 26, 2012

Makao makuu ya polisi nigeria yashambuliwa....




Wanajeshi wakishika doria katika makao makuu ya polisi, ambapo mshambuliaji wa kujitoa mhanga alishambulia mwaka jana
Polisi nchini Nigeri wanasema kuwa watu wenye silaha wameshambulia kambi ya polisi wa usalama iliyoko katika eneo lenye ulinzi mkali katika mji mkuu wa nchi hiyo Abuja.
Kituo hicho kina jengo la askari wa kikosi maalum cha kudhibiti wizi - ambapo pia wanashikiliwa wafuasi wa kundi la kiislamu lenye itikadi kali la , Boko Haram.
Boko haramu linalotaka kuondoa madarakani serikali ya Nigeria na kuweka sheria kali za kiislamu , limekuwa likifanya mashambulio kadhaa katika miezi ya hivi karibuni.
Shambulio la hivi karibuni lilikuwa ni la mabomu mawili ya kujitolea mhanga yaliyolipuliwa jana karibu na kituo cha kijeshi katika mji wa kaskazini wa Kaduna.
Shambulio hili linakuja siku moja baada ya mashambulio mawili ya kujitoa mhanga ambapo watu kumi na moja waliuawa ika kanisa iliyoko ndani ya kambi ya jeshi katika jimbo la Kaduna.
Raia mmoja mjini Abuja anasema alisikia milio ya risasi kwa takriban nusu saa mapema Jumatatu.
Hata hivyo msemaji wa polisi hakutoa maelzo ya ziada kuhusu shambulio hilo.
Hata hivyo kwa kuwa jengo hilo lina ulinzi mkali, hakuna dalili za uharibifu wowote kwa jengo hilo.
Washukiwa wa uhafu pia huziliwa katika jengo hilo mara kwa mara.
Mwaka jana mshambuliaji wa kujitoa mhanga wa kundi hilo alishambulia makao makuu ya polisi katika mji mkuu na kuwaua watu sita.
Chanzo:BBC Swahili


No comments:

Post a Comment