Monday, November 26, 2012

Wanataka Bangi ihalalishwe....


Mwezi huu, Majimbo mawili nchini marekani yamepiga kura kuhalalisha , kudhibiti na kutoza kodi bangi.
Kutokana na matangazo ya kibiashara na sheria za kudhibiti ulevi wa bangi wakati madereva wakiwa njiani , basi tunahoji nini cha mno kinachosubiriwa?
Kura iliyopigwa tarehe sita mwezi Novemba katika majimbo ya Colorado na Washington, bila shaka iliwatia furaha watumiaji wa Bangi lakini polisi wengi walilala wakiwa na wasiwasi si haba.
Na hatua hiyo ikaleta karibu malumbano kati ya majimbo hayo mawili na serikali ya kitaifa, kwani bangi ingali imeharamishwa chini ya sheria za kitaifa. Lakini kama ilivyo ada, kila jimbo nchini Marekani liko huru kutunga sheria zake.
Marijuana kama inavyojulikana na wengi, ni dawa ya kulevya inayotumiwa sana nchini Marekani. Lakini sasa wataalamu wanasema huu ni mwanzo tu wa kuhalalisha dawa hiyo ya kulevya ambayo bado imepigwa marufuku.
“Hiki ni kionjo tu, bado mengi yatakuja’’ alisema Sanho Tree mkuregenzi mkuu wa mradi kuhusu sera ya mihadarati.
"Ikiwa majimbo haya mawili yataendelea na harakati zao za kuhalalisha dawa hiyo ya kulevya, bila mawingu kuanguka, basi utakuwa mwanzo mpya kwa uhuru wa kisiasa." Alisema Sanho
Lakini watawala wako macho
"Wakuu wa polisi mjini Colorado wana wasiwasi kuhusu usalama wa watu kwa ujumla" anasema afisaa mmoja wa polisi John Jackson
Takriban miaka 80 baada ya Marekani kufutilia mbali sheria iliyoharamisha pombe, tunajaribu kujibu baadhi ya maswali ya watu walioelezea hisia mbali mbali kuhusu bangi kuhalalishwa.
Je wauzaji na wakulima wa Bangi wataendesha vipi matangazo ya kibiashara ya bangi?
Ni haramu kwa watu walio chini ya umri wa mia 21 kupatikana na bangi huku jimbo la Washington likiharamisha matangazo a kibiashara ya bangi katika maeneo ya watoto kuchezea .
Kwa watu ambao hawajahi kutumia bangi , harufu na aina zote za bangi ni sawa tu, wakati inapovutwa athari zake ni sawa tu, yaani hakuna tofauti kubwa.
Wakati itakapohalalishwa, je wauzaji/makampuni katika maeneo ya Washington na Colorado yataendesha vipi biashara zao ili kupata wateja wengi?
“Iwe ni soksi au bangi, kitu cha kwanza mteja atataka kufanya ni kuangalia muuzaji wa bidhaa ile.’’ Hii ni kulingana na mtaalamu mmoja wa matangazo ya kibiashara mjini New York.
Anasema kuwa soko la bangi lipo lakini kama ni kwa vijana wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, ambao tayari wanaitumia , hakuna ugumu hapo, kwani hawatahitaji matangazo ya kuwashawishi ili kununua.
Kibarua ni kwa wahafidhina ambao labda kwa sababu ya maadili, hawavuti bangi. Lakini soko linaweza kuwepo kwa wataalamu wanaosongwa na mawazo au wapambe wa kiafya na kadhalika.
Muuzaji wa bangi anaweza kubuni mbinu ya kipekee ya kuuza bangi na kuweza kuifunga kwenye pakiti za kuvutia kwa rangi na ambazo zina mvuto wa kuwa ghali , labda ndio kitu kitakachoweza kuwavutia wanunuaji.
Je mwajiri anaweza kukulazimisha kufanyiwa uchunguzi wa madawa ya kulevya?
Katika jimbo la Colorado, utumiaji wa Bangi bado unaweza kukuweka mashakani, kwani, sheria hiyo mpya, inawaruhusu waajiri kuharamisha utumiaji wa bangi miongoni mwa wafanyakazi.
"Hii haishurutishi mageuzi yoyote,’’ anasema Mason Tvert, mmoja wa wanaharakati wanaotaka matumizi ya Bangi kudhibitiwa kama ilivyo pombe katika jimbo la Colorado.
Sheria ya taifa nayo haina msimamo halisi kuhusu swala hili
Lakini uchunguzi uliokuwa unafanyiwa wafanyafakazi kwenye maofisi umendelea kudidimia. Inahofiwa waajiri katika majimbo ya Colorado na Washington, sasa watatupilia mbali jukumu la kuhakikisha wafanyakazi maofisini hawaji kazini wakiwa walevi wa bangi
Uchunguzi mwingi unaofanyiwa watu kubaini ikiwa wanatumia mihadarati, ni kutokana na dhana kuwa wafanyakazi wengi wanaotumia madawa hayo, huathiri biashara.
Wafanyakazi wengi wanaopatikana wakiwa na chembechembe za mihadarati mwilini, wanajulikana kama 'wavutaji wa bangi wa Jumamosi,' yaani waliovuta bangi mwishoni mwa wiki. Na hivyo hawawezi kufanya kazi.
Sheria za marekani wakati mmoja ziliharamisha pombe. Je sheria hizi zinaashiria kuwa nchi hiyo iko tayari kuhalalisha bangi?
Majimbo mawili nayo tayari yamegusia uwezekano wa kuwasilisha mswaada wa kuhalalisha Bangi.
Baadhi ya watu hutumia Bangi kama njia ya kujiliwaza, kujiburudisha au wakiwa waraibu. Wengine wanasisitiza kuwa Bangi inafaida za kimatibabu.
Nini maoni yako kuhusu swala hili tete?
Chanzo: BBC Swahili

No comments:

Post a Comment