Friday, October 19, 2012

Umasikini wetu ni wa kujitakia....


Na Daniel Mbega 

CHINI ya miti ya mikaratusi, kando ya Mto Mlowa, vijana wanaonekana wakijaza nyanya kwenye matenga ya mbao huku pembeni yao kukiwa na malundo makubwa ya zao hilo

“Hii ni hasara kubwa, nimekuja na matenga hamsini, lakini inaonekana yametoka thelathini tu, haya malundo yote ni nyanya zilizolainika (masalo) ambazo haziwezi kwenda mahali popote,” anasema Jacob Kamota, mkulima wa nyanya kutoka Kijiji cha Iyayi, Kata ya Image wilayani Kilolo. 

Jacob analalamika kwamba, huko shambani pia ameacha malundo ya nyanya zisizofaa kusafirishwa, ingawa zinafaa kwa matumizi ya nyumbani au hata kwa kusindikwa, hali ambayo inazidi kumtia umaskini badala ya kujikwamua kiuchumi. 

“Sina mahali pa kuzipeleka, laiti kungekuwepo na kiwanda ningeweza kuuza nyanya zote na kupata faida, lakini sasa hata gharama zangu sidhani kama zinaweza kurudi,” anasema.
Chanzo: Mjengwa Blog

No comments:

Post a Comment