Wednesday, October 3, 2012

CUF iwache siasa za maji taka....



mjane,Asia Ismail ambaye ni mke wa marehemu Ismail Omary aliyeuwawa katika maandamano ya Chadema mnamo januari 5 mwaka jana jijini Arusha akiwa amembeba mtoto wake wa kike,Amina Ismail juzi katika mkutano wa hadhara wa Cuf uliofanyika uwanja wa Levolosi ambapo alikishutumu Chadema kwamba kimetafuna fedha za rambirambi za marehemu mme wake na kisha kumtekeleza pamoja na kuhaidi kumpatia.(picha na mahmoud ahmad)  

.
 Mahmoud Ahmad,Arusha 
MJANE,Asia Ismail ambaye ni mme wake,Ismail Omary aliuwawa katika maandamano ya januari 5 mwaka jana amekishutumu Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema) mkoani Arusha kwamba kimetafuna fedha za rambirambi za marehemu mume wake lakini mbali na hilo pia wamemtelekeza. Akizungumza katika mkutano wa hadhara wa Chama Cha Wananchi(Cuf) uliofanyika juzi katika uwanja wa Levolosi,mjane huyo alisema kwamba Chadema walihaidi kumpatia fedha za rambirambi zilizochangwa katika uwanja wa NMC wakati wa kuaga mwili wa mme wake lakini hadi leo hajazipata. Huku akiangua kilio katika mkutano huo alisema kwamba alipewa taarifa kwamba Chadema kinachangisha fedha za rambirambi na mara watakapokamilisha mchango hiyo watampatia lakini hadi leo hajawahi kuona fedha yoyote. Mjane,huyo aliyekuwa amembeba mtoto wake wa kike jukwaani aitwaye Amina Ismail alitoa machungu hayo na kwamba fedha aliyoambulia hadi sasa ni ile iliyotolewa na kada ya CCM,Mustafa Sabodo kiasi cha sh,5 milioni . Hatahivyo,alisema kwamba mara kwa mara alikuwa akifunga safari kufika katika ofisi za Chadema wilayani hapa kwa lengo la kufuatilia fedha za rambirambi za mumewe lakini badala yake alikuwa akipigwa danadana. “Nimekuja hapa leo mkutanoni kuelezea machungu yangu ninasikitika sana kwamba Chadema ,mbali na kuchangisha fedha za rambirambi za marehemu mume wangu lakini hadi leo sijawahi kuona hata senti tano”alisema huku akinagua kilio 
Hatahivyo,mjane huyo alisema kwamba pamoja na chama hicho kutangaza kuijali familia yake mara alipofariki mme wake lakini hadi leo hakuna kiongozi yoyote anayejua maendeleo ya familia hiyo. Alisema kwamba marehemu mme wake alimwachia watoto wawili ambapo kwa sasa anahangaika kuwahudumia kuwapatia mahitaji mbalimbali kama elimu,malazi na chakula hatahivyo mara nyngine anashindwa kuyatimiza kutokana na kukosa ajira ya kudumu. Mara baada ya kutoa kilioo hicho ndipo uongozi wa Cuf uliamua kuitisha harambee jukwaani hapo ambapo wafuasi mbalimbali wa chama hicho walimchangia mjane huyo kwa kumkabidhi fedha hizo mikononi kiasi cha zaidi ya sh,500,000 huku wakilaani kitendo kilichofanywa na uongozi wa chama hicho. Alipatafutwa katibu wa Chadema mkoani Arusha ili ajibu madai hayo kwanza alikanusha madai hayo na kusema kwamba wao walimpa rambirambi zote zilizochangwa na wafuasi wao ambazo hawajui ni kiasi gani pamoja na hundi ya kiasi cha sh,5 milioni zilizotolewa na Sabodo. Alisema kwamba hata kwenye kumbukumbu ya mauaji ya januari 5 mwaka huu walimpatia kiasi cha sh,200,000 mjane huyo na kudai anaendeshwa na upepo wa kisiasa na kuvitaka baadhi ya vyama vya siasa kumwogopa Mungu. Kuhusu madai ya kutekelezwa Gorugwa alisema kwamba hawawezi kuweka utaratibu wa kumpigia simu kila siku kwa kuwa kila mmoja ana maisha yake na hata mjane huyo ana maisha yake huko mkoani Tanga. “Jamani tumwogope Mungu huyu mama anapelekwa na upepo wa kisiasa tu lakini tumwonee huruma kwa kuwa ni mjane, sisi tulimpa hela yote na alisaini hundi ofisini kwetu na hata nyie waandishi mlikuja kupiga picha”alisema Gorugwa.

No comments:

Post a Comment