Tuesday, September 25, 2012

Leo wakati nafungua ukurasa wa facebook wa timu kongwe katika ligi ya Tanzania Bara Coastal Union 'wagosi wa kaya' nilikutana na habari za kujiuzulu kocha mkuu wa timu hiyo Juma Mgunda 'kipande cha baba'

 Hapa Juma Mgunda akisindikizwa na polisi baada ya kukoswakoswa kupigwa na washabiki wa Coastal wenye hasira. Ambao walikuwa wakitalka ajiuzulu, ni baada ya mechi ya kirafiki dhidi ya Bandari ya Mombasa nchini Kenya ambapo Coastal walifungwa 2-0... Kabla ya kuanza msimu mpya wa ligi mwaka huu.

 Uwanja wa nyumbani huu Mkwakwani mjini Tanga Kocha mkuu wa Wagosi wa kaya Juma Mgunda akiwajibika.

Hii ilikuwa ni mechi ya kirafiki Coastal na Yanga iliyochezwa katika uwanja mpya wa Taifa. Ambapo Coastal ililala 2-1...... Siku ya pili Coastal ilicheza mechi nyingine ya kirafiki dhidi ya Azam FC katika uwanja wa Chamanzi ambapo Coastal ililala 2-0.


''kwa mapenzi makubwa niliyo nayo juu ya timu yangu ya Coastal Union nimeamua kujiuzulu kufundisha Coastal union ili itimize malengo yake iliyojipangia ikiwa na amani na utulivu.......Mungu ibariki Coastal Union''................Maneno ya Juma Mgunda baada ya kuchukua maamuzi magumu ya kujiuzulu leo asubuhi.

Hii ndiyo habari yenyewe niliyoipata, lakini baada ya kuwapigia simu wadau na mashabiki waliopo Tanga walisema habari hizo zipo lakini bado Juma Mgunda hajazungumza rasmi na vyombo vya habari.

Lakini imeshathibitishwa kuwa katika mechi ya kesho ya ligi kuu katika uwanja wa nyumbani ambapo Coastal itakutana na Kagera sugar inayonolewa na mkongwe wa siku nyingi wa Simba King Abdalaah Kibaden, Juma Mgunda hatokuwepo katika benchi la ufundi badala yake benchi litaongozwa na kocha wa makipa mkongwe Juma Pondamali Mensah.

Mpaka sasa Coastal Union imeshacheza mechi tatu moja ugeninii na mbili nyumbani. Imeshinda mechi moja ya nyumbani dhidi ya Mgambo FC ya mjini Tanga iliyopanda daraja msimu huu, mechi nyingine ilikuwa ni dhidi ya Toto Africa na ya tatu ilikuwa ya ugenini dhidi ya Prison mjini Mbeya ambapo ilitoa suluhu mechi zote mbili.

Fuatilia kidojembe kesho ili kama kuna taarifa zozote mpya kuhusiana na hatma ya Juma Mgunda ambae ni mchezaji wa zamani wa Coastal Union katika safu ya ushambuliaji......

HAFIDH KIDO
DAR ES SALAAM, TANZANIA
kidojembe@gmail.com
0713 593894/ 0752 593894
25/09/2012

No comments:

Post a Comment