Sunday, August 19, 2012

Habari zenu ndugu zangu, poleni kwa kuwatupa sikukuu imetufanya kuenda mbio. Sasa imeisha turudi ofisini. picha hii na habari yake nilivipata katika ukurasa wa facebook wa ndugu Chesi Mpilipili. Nimevutiwa sana na hii habari nikaona si vibaya tukigawana taarifa.


‎...Huyu alikuwa ni Nguli wa muziki ambaye tunaweza kusema ni kama 'alinunua' kifo chake mwenyewe kwa maana halisi.
Alizaliwa Washington D.C tar 2 April 1939 kwa baba Marvin GAY Sr aliyekuwa mchungaji na mama Alberta Cooper-GAY aliyekuwa mwalimu na mtumishi wa ndani.
Alibatizwa Marvin Pentz GAY na kama ilivyo kwa wasanii wengi wa zamani wa Marekani alianza kwa kuimba kwaya kwenye kanisa alilokuwa akihubiri baba yake.
Alipoanza rasmi safari ya kuwa mwanamuziki akaongeza herufi e kwenye jina lake la mwisho na kuanza kufahamika rasmi kama MARVIN GAYE Jr.
Alipata kujifanya kichaa ili kutimuliwa kwenye jeshi la anga la marekani USAF ili kutimuliwa baada ya kuwa mkaidi wa kufuata amri za jeshi. Akarudi uraiani na kuingia rasmi kwenye shughuli za Muziki.

Alisumbua sana na nyimbo zake za mapenzi kama 'How sweet it is(to be loved by you), Aint no Mountain high enough, Heard it over the Grapevine, Aint that peculiar, what is going' nk.
Hata hivyo, kilele cha mafanikio ilikuwa pale September 1982 alipotoa wimbo uliokuja kuwa 'Wimbo wa Taifa wa Masuala ya Mapenzi' wa SEXUAL HEALINGS' uliotingisha Ulimwengu mzima.
Matumizi ya madawa ya kulevya yakamfanya nguli huyu mtu asiyejiamini na kila saa kuhisi kuwa kuna wabaya walikuwa wanamvizia ili kumdhuru na kwenye sikukuu ya Krisimasi ya 1983 akamnunulia baba yake mzee Marvin Gay bastola ili aitumie katika kumlinda. Ole Wake!
Miezi mitatu tu baadaye kwenye siku ya Wajinga tar 1 April 1984 baba mtu huyu ambaye tayari aliishakuwa mtu wa kibywaji kwa sana akatumia bastola hiyo hiyo kumuua mwanaye Marvin Gaye ambaye alikuwa anajaribu kusuluhisha mzozo kati ya Wazazi wake hao.
MARVIN GAYE akatangulia mbele za haki siku moja kabla hajatimiza miaka 45 kamili huku kibao chake cha SEXUAL HEALINGS kikiwa kwenye kilele cha mafanikio kama ilivyo hadi leo unapokisikia. MARVIN GAYE, tunakukumbuka:

No comments:

Post a Comment