Saturday, August 25, 2012

haya sasa tazameni picha hizo za shughuli nzima ya leo kuhusu semina ya namna gani utazalisha pesa kupitia mtandao wa internet...


Kitu nilichojifunza leo ni kuwa watanzania wengi wanatumia mitandao ya kijamii kujifurahisha tu bila kujua fursa ambazo zinaweza kuwafanya wakawa matajiri bila ya kuajiriwa.

Mwanaadamu huna budi kutengeneza bomba ama mrija wa kuzalisha pesa ‘pipe line’ kwani si kila siku utakuwa na afya ama utakuwa na nguvu za kufanya kazi za sulba. Inahitajika pesa zako zikutumikie na si wewe kuzitumikia pesa.

Kwa mfano unapogundua unatumia mitandao ya kijamii bure basi wewe unatumika kama bidhaa ama njia za wengine kuzalisha pesa kupitia uwepo wako.

Tazama, watu wengi wanaweka pesa katika kanzi ‘bank’ lakini pesa hizo zinakaa miaka miwili mpaka mitatu bila ya kuzitumia. Lakini cha ajabu watu wenye shida wanakwenda kukopa na kuanza kuzitumia. Hivyo huna sababu ya kshindwa kuzizalisha pesa zako.

Umeshawahi kuona kurasa za kampuni kubwa mfano tigo, vodacom ama Serengeti katika facebook? Basi wapo watu kazi yao ni kuziendesha kurasa hizo na wanalipwa mamilioni ya pesa kwa mwezi. Vipi wewe umesha ‘like’ kurasa ngapi za kampuni, unajua kama unawaingizia pesa watu kupitia uwepo wako?

Mpaka sasa umeshachukua hatua gani kuhakikisha furaha yako ya kushiriki mitandao ya jamii haiishii katika kukutana na marafiki wako ulioachana nao siku nyingi badala yake inakuwa ni ajira?

Duniani kuna mabilioni ya blongs na website zinazokaribia 600, wewe upo wapi?
Anza sasa uhakikisha mitandao ya kijamii kwako ni ajira na si furaha tu.

Tanzania bado tupo nyuma, masikitiko makubwa haya mpaka sasa inakisiwa ni watanzania milioni moja tu wanaoingia katika mitandao kwa siku. Sasa jiulize katika watanzania wanaokaribia milioni hamsini ni milioni moja tu wanaoingia katika internet kwa siku.

Tafakari… chukua hatua.

HAFIDH KIDO
DAR ES SALAAM, TANZANIA
0713 593894/ 0752 593894
kidojembe@gmail.com




 kijana aliehudhuria semina ya leo akizungumza kitu wakati mkutano ukiendelea.

 Huyu ni mzee Charles Nazi mwandishi wa vitabu juu ya ujasiriamali na pia anamiliki blogu inayohusu namna ya kuwa tajiri.


 Semina ikiendelea huku wadau wakisikiliza kwa makini bila kukosa hata kitu kimoja.

                                              Jembe nsmi nikiwa makini wakati wa semina.

                                       Bwana Mlaseko huyu akiendelea kuwapasha watu habari.



                                               Washiriki hawa wakisikiliza kwa makini.

                                    Jembe na laptop yake akiuza sura, kuchoka nako kubaya.

No comments:

Post a Comment