Monday, July 30, 2012

Kweli haki haina umri...


Leo waalimu wa shule za serikali wameanzamgomo wao uliotangazwa miezi kadha iliyopita. Ambapo mgomo huo umeitwa ni batili na Serikali ya Tanzania kwa madai kuwa shauri lao lipo mahakamani kwa kupatiwa ufumbuzi.

Serikali iliamua kukipeleka chama cha waalimu mahakamani baada ya kushindwa kupata muafaka katika baraza la usuluhishi nchini CMA.

Hata hivyo wanafunzi nao wameamua kuandamana kudai haki yao ya kufundishwa wakidai wapo karibu na kuanza mitihani ya muhula inakuwa vipi waalimu wanagoma?

No comments:

Post a Comment