Monday, July 30, 2012

Wanawake waliohasiwa bila ridhaa washinda kesi namibia...


Mahakama nchini Namibia imetoa uamuzi wake kuwa wanawake watatu wanaoishi na virusi vya HIV haki zao za kibinadamu zilikiukwa walipofungiwa uzazi bila ridhaa yao.
Wanawake hao wanasema waliambiwa wafanyiwe utaratibu huo kama walikuwa wanataka kujifungua kwa upasuaji kupunguza uwezekano wa watoto wao kuambukizwa virusi vya HIV.
Mahakama hiyo iaangalia ni kwa namna gani watapata fidia ya athari walioipata. Mwandishi wa BBC Kusini mwa Afrika anasema uamuzi huo wa mahakama kuwapa haki wanawake hao unaweza kuwa na athari chanya kwa nchini nyingine katika ukanda huo.
Kesi hiyo ilifunguliwa na wanawake wajawazito watatu walioamua kujifungua kwa upasuaji ili kupunguza uwezekano wa watoto wao kuambukizwa virusi vya HIV.
Maafisa wa afya wamekana kuwa wanawake hao walifungwa uzazi kwa nguvu bila ridhaa yao.
Mawakili wa wanawake hao wanasema kesi nyingine kama hizo zimeripotiwa katika nchi nyingine katika ukanda huo.
Awali mawakili wa wanawake hao walisema wateja wao waliambiwa na madaktari nchini Namibia kuwa wangeweza tu kufanyiwa upasuaji iwapo wangekubali kufungiwa uzazi kwa wati huo.
Mawakili hao wanasema kulazimishwa kukubaliana ni tofauti na kupatiwa taarifa muhimu ili kukubalina na jambo hilo na kwa hiyo mamlaka za Namibia zilikiuka haki za binadamu kwa wanawake hao.
Wizara ya afya inakanusha kuwa ilitoa maelekezo kwa wanawake wanaoishi na virusi vya HIV wafungiwe uzazi na kuongeza kuwa haikuwa inafahamu kuwa kuna mtu yeyote amefungiwa uzazi bila ridhaa yao.
Nicole Fritz, kutoka kituo cha Sheria cha Kusini mwa Afrika na hivyo kufungua kesi, ameiambia BBC kuwa wanawake hao wamekuwa kwenye maumivu na hawajui nini kitatokea.
"Mmoja wa wanawake hao amekuwa kwenye uchungu kwa siku nne, uchungu ambao hauelezeki. Wengine kati hao hawakujua hasa kile walichokuwa wakikubaliana nacho. Walidhani ilikuwa ni sehemu ya utaratibu wa kufanyiwa upasuaji,"Alisema
"Hivyo taarifa kuwa walikubaliana, hawakuelewa kilichokuwa kinaendelea, hawakujua utaratibu ulivyokuwa na walikuwa wanakubaliana na nini, hawakuwa na taarifa za kutosha kukubaliana. "
Mawakili wanasema wana ushahidi kuwa wanawake wanalazimishwa kufungiwa uzazi nchini Swaziland na baadhi ya maeneo ya Afrika Kusini, ambapo wanasema inawanyima wanawake hao haki zao za kikatiba.
Kiasi cha 13% ya watu wazima nchini Nambia wanaishi na virusi vya HIV kwa mujibu wa UNAIDS.
Chanzo: BBC Swahili.

No comments:

Post a Comment