Tuesday, July 31, 2012

Futari ya leo,

Asalam Alaykum,

Leo tutapika futari ya kipwani, Mihogo ya nazi, maharage ya sukari, chapati na mchuzi wa kukaanga, papa wa kuchoma na nyama ya kuchemsha iliyokaushwa na viungo kama pilipili manga, tangawizi, limao na vitunguu swaum.

Halafu unamalizia na matunda kama kawaida yetu, ukipata aina mbili za matunda itakuwa vema. Maji mengi ni muhimu usisahau.

No comments:

Post a Comment