Thursday, July 26, 2012

Mafunzo ya siku tatu kwa wapiga picha wanaotoka nchi za Afrika ya mashariki yamemalizika rasmi leo mjini Arusha ambapo malengo yake ni kuhakikisha kunakuwepo na wapiga picha imara ambao wanaweza kuripoti matukio katika jamii kwa njia ya picha kwani picha inaweza kutafsiriwa kwa urahisi na watu wa lugha zote duniani kuliko maneno...

 Washiriki wa warsha ya wapiga picha kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakiwa katika picha ya pamoja na Naibu Katibu Mkuu wa EAC anayeshughulikia Shirikisho la Kisiasa Dr Julius Rotich (aliyeketi wa pili kushoto) mjini Arusha jana. Kushoto kwake ni Kaimu mkuu wa mpango wa EAC-GIZ and kulia ni Mkuu wa Idara ya Habari EAC Owora Othieno. Kulia kabisa aliyesimama ni mratibu wa mafunzo wa EAC Sukhdev Chhatbar.


Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), anayeshughulikia Shirikisho la Kisiasa,Dkt. Julius Rotich(akifafanua jambo kwa waandishi juu ya Mafunzo ya Upigaji picha ‘EAC-GIZ Master Class Photographers Training’

 Mpiga picha mahiri kutoka Tanzania na mmiliki wa blogu ya 'father kidevu' Mroki Mroki, akizungumza na wanahabari wakati wa mafunzo ya siku tatu ya upigaji picha yajulikanayo kama ‘EAC-GIZ Master Class Photographers Training’ yaliyoanza Julai 23-26, 2012 mjini Arusha.


 Mkufunzi Mkuu wa Upigaji picha ambaye pia ni Mpigapicha kutoka Ujerumani ambaye anafanya shughuli zake nchini Kenya, Hartmut Fiebig akitoa maelekezo kwa wapigapicha.


Washiriki kutoka nchi wanachama za Afrika ya Mashariki wakiwa darasani ambapo kila nchi ilitoa washiriki wawili kuhakikisha mafunzo hayo yanaleta udugu na muingiliano mzuri kutoka nchi tano za jumuiya hiyo.

No comments:

Post a Comment