Sunday, July 29, 2012

Kutoka BBC Swahili...


Polisi wa Kenya wanasema kuwa wanaendelea na uchunguzi, juu ya mauaji ya balozi mpya wa Venezuela nchini humo, ambaye aliuwawa Ijumaa.

Olga Fonseca, aliyeanza kazi Kenya kati ya mwezi Julai, alikutiakana ameuwawa nyumbani kwake, na watu sita wamekamatwa hadi sasa.
Watu hao sita wamekamatwa siku mbili tu baada ya balozi huyo kupatikana amefariki nyumbani kwake.
Siku ya Ijumaa, polisi walisema kuwa maiti ya Bi Olga Fonseca ilipatikana kitandani mwake lakini sababu za kuuwawa kwake hadi sasa hazijulikani.
Bila ya kutoa maelezo zaidi, polisi wamesema kuwa wanawashikilia watu sita kuhusiana na kifo cha balozi huyo.
Taarifa kutoka wizara ya maswala ya njee ya Kenya imesema kuwa wafanyikazi katika makaazi ya balozi huyo waliwasilisha malalamiko yao kwa polisi baada ya kufutwa kazi hivi majuzi.
Inadaiwa kuwa bi Fonseca aliwafuta kazi baada ya wao kukataa kuondoa malalamiko kuhusu madai ya kunyanyaswa kijinisia na mtangulizi wa balozi huo.
Hata hivyo polisi wamesema wanachunguza madai hyao.


Wakati huohuo

Mashirika yasiyokuwa ya serikali katika Jamhuri ya Demokrasi ya Congo, yanasema kuwa wanajeshi wa Uganda wameingia Jamhuri ya Demokrasi ya Congo, kupigana pamoja na jeshi la huko dhidi ya wapiganaji waitwao M23.

Mashirika hayo yanasema magari ya deraya sita, yaliyojaa wanajeshi yamevuka mpaka kutoka Uganda, na kuingia jimbo la Kivu Kaskazini.
Jeshi la Uganda limekanusha tuhuma hizo.
Mataifa kadha ya magharibi yamesimamisha msaada kwa Rwanda, baada ya ripoti ya Umoja wa Mataifa kusema kuwa Rwanda inalisaidia kundi la wapiganaji la M23 -- tuhuma ambazo zinakanushwa na Rwanda.
Chanzo: BBC Swahili

No comments:

Post a Comment