Wednesday, May 22, 2013

Ripoti ya kamati ya kuchunguza tuhuma za Rais wa Kenya yatoka..



Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta na naibu wake wametajwa katika ripoti inayowahusisha na ghasia za baada ya uchaguzi katika ripoti iliyosubiriwa kwa muda mrefu kuhusu ukiukwaji wa haki za bindamau nchini humo.

Ripoti hiyo hata hivyo haikutoa mapendekezo ya hatua inazotaka kuchukuliwa dhidi ya Rais Kenyatta na naibu wake William Ruto.

Mwenyekiti wa tume hiyo, aliambia BBC kuwa ni kwa sababu wawili hao wanakabiliwa na kesi ya uhalifu dhidi ya binadamu katika mahakama ya kimataifa ya ICC.

Rais Kenyatta na bwana Ruto wanakana tuhuma hizo.

Tume ya maridhiano na haki ilikabidhiwa jukumu la kuchunguza visa vya ukiukwaji wa haki za binadamu vilivyofanywa tangu mwaka 1963 nchi hiyo ilipojipatia uhuru wake.

Iliundwa baada ya ghasia za baada ya uchaguzi wa mwaka 2007/08 uliozua ghasia miaka mitano iliyopita kama njia ya kuleta maridhiano miongoni mwa wakenya.

Baada ya uchaguzi huo, watu 1,500 waliuawa na wengine zaidi ya 600,000 kulazimika kutoroka makwao.

Kenyatta na Ruto, waliokuwa mahasimu katika uchaguzi wa mwaka 2007, walishinda uchaguzi mkuu uliofanyika mwezi Machi baada ua kuungana chini ya muungano wa Jubilee.

Licha ya kuwa hakuna mapendekezo yaliyotolewa na tume hiyo dhidi ya Rais na naibu wake, inapendekeza uchunguzi zaidi dhidi ya maafisa wakuu waliotajwa kuhusika na ghasia za baada ya uchaguzi mwaka 2007 na hata kufunguliwa mashtaka

Baadhi ya waliotajwa ni pamoja na waziri mpya wa madini Najib Balala na maseneta wawili.

Hata hivyo yume hiyo ilimtaka rais Kenyatta kuwaomba radhi wakenya kwa makosa waliyotendewa chini ya seri9kali zilizopita katika kipindi cha miezi sita tangu kukabidhiwa ripoti hiyo hapo jana.

Rais mstaafu Daniel Moi pia alitajwa katika ripoti hiyo akihusishwa na mauaji ya waliokuwa wanasiasa mashuhuri wakati wa utawala wake
BBC SWAHILI

No comments:

Post a Comment