Wednesday, May 15, 2013

Wenye ulemavu wanena...



MWENYEKITI wa Umoja wa Wafanyabishara Walemavu Dares Salaam (UWAWADA), Mohamed Kidumke amesema kama serikali haitawasaidia mikopo walemvu  basi kuna hatari baadhi ya watu hao wakaendelea kuwa ombaomba barabarani milele.
 Wakizungumza na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam juzi, Kidumke alisema badhi ya walemavu hao hawapendi kukaa barabarani na kuomba bali wamekuwa wakifanya hivyo kutokana na kukosa njia za kujiingizia kipato.

 Alisema Umoja wao unania ya kuwaondoa walemavu wote wanaomba barabarani kwa kuwaanzishia biashara ndogondogo lakini bado jitihada zao hizo zinahitaji uungwaji mkono na serikali kwa kuwapatia mikopo nafuu walemavu hao ili waweze kujikwamua.

 “Wapatiwe mikopo pia watengewe maeneo ambayo yatawezesha kukutana na wateja kwa wingi kwa mfano maeneo wanayolenga ni kama vile kwenye vituo vya daladala”alisema Kidumke.

 Kidumke alisema ni muda mrefu umoja huo uliuomba uongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Ilala kuwatengea maeneo ya kufanyia biashara lakini hadi sasa uongozi huo haujatoa jibu.

 Alisema wakati mwingine viongozi hao wamekuwa wakichukuliwa na umoja huo kama chanzo kimojawapo kinachokwamisha juhudi za maendeleo yao kwa kutozipatia ufumbuzi changamoto zinazowakabili. 
Chanzo:www.fullshangweblog.com

No comments:

Post a Comment