Thursday, May 30, 2013

Sababu za kifo cha msanii wa Tanzania nchini afrika Kusini, ni hizi.

Mangwea (katikati) akiwa katika moja ya harakati zake za muziki enzi za uhai wake.
Wadau mbalimbali wa sanaa ya muziki Tanzania wakiwa katika viwanja vya Leaders Club jana kujadili na kuunda kamati itakayoshughulikia kuusafirisha mwili wa msanii huyo. Mpaka jana taarifa zilizopatikana na kuwa mwili unahitaji Sh mil 30, ili kuweza kuusafirisha kutoka Afrika Kusini. 
Mtangazaji wa kituo cha Clouds FM, Millard Ayo akifanya mahojiano na mmoja wa watu walio Afrika Kusini kuhusiana na msiba huo wakati aliposafiri mpaka Hospitali aliyofariki Mangwea.



Dar es Salaam. Wakati mazishi ya mwanamuziki marehemu Albert Mangwea(28) maarufu kama `Ngwair’ yakitarajiwa kufanyika mjini Morogoro, maeneo ya Kihonda baada ya mwili kuwasili nchini, hospitali iliyomfanyia vipimo imethibitisha kuwa pombe na dawa za kulevya kupita kiasi ndivyo vilivyomuua.

Mwili wa mwanamuziki huyo, ambaye alitamba kwenye miaka ya 2000 na wimbo wa `Mikasi’, unatazamiwa kuletwa kesho nchini na kuagwa Jumamosi kabla ya kusafirishwa kwenda kwao Kihonda, Morogoro kwa mazishi.

Kwa mujibu wa taarifa Mangwea alifariki dunia juzi kwenye Hospitali ya St Hellen, iliyopo Johannesburg, Afrika Kusini alikokuwa amekwenda kwa shughuli za muziki.

Kifo chake

Ripoti iliyochapwa na mitandao mbalimbali ya ndani na nje ya nchi inasema marehemu alifikwa na umauti baada ya kulewa kupindukia, kibaya zaidi alikuwa hajala.

Siku ya kifo chake, Mangwea alianguka nyumbani kwa rafiki zake akiwa katika hali hiyo ya kulewa sana.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, baada ya kufikishwa hospitalini, Mangwea aligundulika kulewa mara tano ya kipimo cha kilevi kilichopitishwa na serikali ya Afrika ya Kusini, ambacho ni 416mg za pombe kwenye kila milimita 100(kwa mlevi anayeendesha chombo cha moto).

Pia marehemu alikutwa na upungufu wa hewa ya oksijeni kwenye seli na tishu za mwili wake.

Ripoti hiyo ilibainisha kuwa Mangwea, maarufu Ngwair, alikuwa na tatizo la kutokula chakula vizuri kabla ya kifo chake na pia kukosa muda wa kupumzika.

Sampuli zilizopatikana mwilini mwake zinaonyesha mkusanyiko wa dawa za kulevya mbalimbali zikiwemo heroine, cocaine chafu na bangi ya gramu 0.08 ambavyo vilikutwa kwenye damu yake.

Kifo chake kilitokana na mshtuko wa moyo na kushindwa kupumua, hali iliyosababisha mapigo ya moyo wake kusimama kwa sekunde chache, na kusababisha kifo chake.

Mwili wa Ngwair ulionekana kana kwamba alitokwa na damu nyingi puani baada ya kuonyeshwa kwa Watanzania wengi jana jioni Johannesburg, Afrika Kusini.

Taarifa za awali zilizotolewa na rafiki wa karibu aliyepo nchini Afrika Kusini, aliyejitambulisha kwa jina moja tu la Jonathan zilidai kuwa marehemu hakuamka tangu alipopumzika usiku wa kuamkia juzi.



M2 The P naye mahututi

Rafiki wa Ngwair aliyekuwa naye siku ya tukio, ambaye pia ni msanii, Mgaza Pembe maarufu kwa jina la `M2 To The P’ naye alifikishwa katika Hospitali ya St Hellen baada ya kukutwa amepoteza fahamu akiwa na Ngwair. Msanii huyo, ambaye makazi yake yako Kibaha mkoani Pwani, aliwahi kutamba na wimbo wa ‘M2 To the P’ na ule wa hivi karibuni wa `Nyumbani’.

Historia ya Ngwair

Ngwair alizaliwa Novemba 16, 1982 jijini Mbeya, ni mtoto wa mwisho kuzaliwa kwa baba akiwa mtoto wa 10 na kwa mama akiwa mtoto wa sita. Ngwair asili yake ni Ruvuma kabila la Wangoni. Akiwa na miaka mitano walihamia Morogoro akasoma Shule ya Msingi Bungo alipofika darasa la tano, baba yake akapata uhamisho kwenda Dodoma. Baadaye alisoma Shule ya Sekondari ya Mazengo kabla ya kujiunga na Chuo cha Ufundi Mazengo.

Aliondoka lini?

Ngwair aliondoka nchini mwaka huu mwezi Machi, tarehe 26 kwa mwaliko wa kisanii ambapo tangu kipindi hicho, amekuwa akifanya onyesho moja kila mwezi na mara ya mwisho, onyesho lake lilikuwa wiki mbili zilizopita.

P Funk: Ngwair Ana nyimbo 50 ambazo hazijatoka!

Paul Mathyesse, a.k.a P Funk ambaye ni mtayarishaji aliyefanya idadi kubwa ya muziki wa Ngwair, ameiambia Mwananchi kuwa hadi sasa haelewi nini kimetokea lakini anachofahamu kuwa Albert Mangwea ni zaidi ya msanii kwake na ni kati ya wasanii aliofanya nao kazi nyingi.

Alisema kila ambacho amekuwa akimfundisha na kumwelekeza ndicho alichokifanya kwa kuwa alikuwa na uwezo wa kuimba aina zote za muziki Hip Hop, Free style na ragga.

“Nilikuwa na Ngwair kwa zaidi ya miaka 13, ninamfahamu vizuri na ninaujua uwezo wake, alikuwa ni zaidi ya rafiki yaani sina neno zuri la kusema kumhusu zaidi ya kumtakia safari njema,”alisema.

P- Funk pia ni Mkurugenzi wa Bongo Records ambayo marehemu alikuwa akifanyia kazi zake hadi anafikwa na umauti.

P –Funk anafafanua kuwa hata albamu zote mbili za Ngwair yeye ndio amefanya ukiachilia mbali nyimbo ambazo alikuwa akifanya moja, moja ambazo hadi sasa wanazo nyimbo 50 ambazo hawajazitumia.

Anasema alikutana na Ngwair mwaka 2000 ambapo alikwenda studio na rafiki yake ambaye hamkumbuki jina ilipofika wakati wa kuimba ndio alipokigundua kipaji chake na kumsainisha mkataba na wimbo wao kwanza ulikuwa ni ‘Gheto langu’.

Anaendelea kusema kuwa hata kumtambulisha kwa mashabiki mikoani kwa mara ya kwanza walifanya wao ambapo aliunganishwa kwenye ziara ya ‘wimbo wa nini cH chanzo’ wa Juma Nature,mwaka 2001.

Maneno ya mwisho aliyoandika kwenye ukurasa wake wa Twitter.

Ilikuwa ni Mei 26 Ngwair aliweka ujumbe huu kwenye ukurasa wake wa Twitter,”Namuhitaji Mungu kwa kila dakika kila saa,” akitumia lugha ya Kiingereza.



Maneno ya mwisho kuzungumza na mama yake

Ilikuwa ni wiki mbili zilizopita Ngwair aliwasiliana na mama yake na kumtaka aendelee kumwombea au waombeane na kumwahidi angerudi Ijumaa iliyopita na hakuwasiliana naye tena hadi anafikwa na umauti.



Baadhi ya watu aliowahi kufanya nao kazi wazungumzia kifo chake

Mchezaji Adam Nditi aliandika kupitia ukurasa wake wa Twitter R.I.P Albert Ngwair You will be missed by many Tanzanians.

Mtangazaji wa Clouds Loveness aliandika kwenye ukurasa wake kuwa “Yani siamini Ngwair amefariki dunia nini ilichomkuta #RIP # Ngwair r #akaCowobama

Jamani Ngwair , am in tears now ….. Jamani!. I can’t believe this. I can’t tweet The RIP….

Whyyyyy?

Mr II a.k.a Sugu

R.I.P ALBERT MANGWEA a.k.a NGWAIR...U R GONE TOO SOON MY NIGGA...



Lady Jay Dee

Ngwair ndio aliniandikia verse ya Rap, kwenye wimbo wa Jaffarai. Unaoitwa “Sio Kweli”

ASALAAM ALAYKUM, TANZANIA. IT’S JIDE ONCE AGAIN HEAR ME LOUD N CLEAR.........na maneno mengine yote yalioendelea.

I Wish i could turn back the hands of time.

Profesa Jay

PUMZIKA KWA AMANI KAMANDA Wangu Wanadamu tulikupenda sana ila MOLA amekupenda zaidi, Jina lake LIHIMIDIWE.. Tutakukumbuka daima #COWIIZZ”.

Diamond

DAH! bado nashindwa kuamini nnachokiskia na kukiona kwenye Media.

 Wasanii na watu mbalimbali wamekuwa wakiandika kwenye kurasa za kijamii kuhusiana na kifo hicho cha ghafla cha msanii huyo.

 Imeandaliwa na Harrieth Makwetta, Kalunde Jamal na Vicky Kimaro
MWANANCHI

No comments:

Post a Comment