Monday, July 16, 2012

Malalamiko yaanza vitambulisho vya Taifa.

 Karani wa NIDA akichukua maelezo ya mwananchi ili kupata kitambulisho cha Taifa, Alimaua 'B' leo.

 Wananchi wakiwa katika sura za mshangao baada ya kusubiri kwa muda mrefu bila matumaini.

                                 Nenda ukasajiliwe upate kitambulisho chako kabla ya wikimbili kuisha.

                                    Mzee Mneka huyu, Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa, Alimaua B.



Malalamiko yameanza katika mchakato wa kupata vitambulisho vya Taifa. Leo nikiwa katika kituo cha kijitonyama alimaua B, nilikutana na changamoto hizo za malalamiko ya utaratibu mbaya wa kupata vitambulisho hivyo.

Sikutaka kufanya mahojiano na wadau hao maana sikutaka wajue mimi ni mwanahabari, lakini kwa ujumla malalamiko makubwa ni makarani kuwa taratibu katika kuchukua maelezo na wengi wao wakilalamika elimu ndogo ya makarani hao.

Kadhalika wafanyakazi wa serikali na binafsi walitoa ushauri ni kwanini wafanyakazi hao wa NIDA wasitoe fomu hizo katika ofisi ili kutoa urahisi na kuokoa muda. Maana kwa utaratibu wa sasa siku ya kwanza unajaza fomu halafu unarudi tena kuambiwa kuwa maelezo yako yamekubaliwa kwa ajili ya kupewa kitambulisho maana mpaka kikatengenezwe.

Hivyo kama ni mfanyakazi ambae unatoka asubuhi na kurudi jioni itakuwa vigumu kusubiri foleni ambayo kwa hakika ni ndefu. Nadhani ipo haja NIDA wakasikiliza matatizo ya wadau kuliko kujitia uziwi wasiokuwa nao.

HAFIDH KIDO
0713 593894/ 0752 593894
DAR ES SALAAM, TANZANIA
hafidhkido@yahoo.com

1 comment:

  1. KUTOKANA NA UNYETI WA KAZI HII WANANCHI TANATAKIWA KUWA NA SUBRA....!!!!!!
    VYENGINEVYO VITAMBULISHO VINAWEZA KUANGUKIA KWA WASIO WALENGWA....!

    ReplyDelete