Na Hafidh Kido
Katibu mkuu wa chama cha demokrasia na maendeleo
CHADEMA ameendelea kushikilia msimamo wake wa kutokutoa taarifa zozote kwa
jeshi la Polisi kuhusiana na suala lao la kutafutwa na watu anaodai ni wana
usalama akidai hiyo ni kazi yao kufuatilia ukweli.
Akizungumza na wanahabari nje ya jengo la makao makuu
ya jeshi hilo leo mchana alipokwenda
kujisalimisha yeye na Gdbelss Lema, Dk slaa amesema hawezi kutoa taarifa zozote
kwani hana imani na jeshi hilo
juu ya masuala yanayomfika.
"Siwezi kusema chochote na wala sijabadili
msimamo wangu wa kutotoa taarifa zozote kwa jeshi hili. Maana zipo taarifa
nyingi tumeshawahi kuwapatia lakini kwa dharau tu hawajatekeleza hata moja,
sasa inakuwaje wanataka wanihoji," aliuliza.
Hata hivyo wanahabari walikuwa na wakati mgumu katika
jengo hilo
baada ya kusubiri kwa muda mrefu tangu saa nne kamili muda ambao Dk Slaa na Lema
waliingia kufanya mahojiano na polisi mpaka saa sita na dadkika 28 mchana
walipotoka.
Askari waliwazuia wanahabari kupiga picha na kuwataka
watoke nje ya eneo hilo
kwa madai wao hawajaita wanahabari.
Akizungumza na wanahabari mnadhimu wa polisi H.R.
Mbezi, alisema hakuna ruhusa mwanahabari yeyote kupiga picha wala
kuzungukazunguka kwani kufanya hivyo ni kinyume cha sheria.
"Nani amewapa ruhusa kupiga picha, hamjui ni
kinyume cha sheria na tunao uwezo wa kuchukua kamera zenu na kufuta picha zote
mlizopiga," alihoji Mbezi na kuendelea "Tunawaomba muende kwa afande
Kova kituo kikuu cha Polisi atawapa taarifa zaidi," alisema lakini
wanahabari waliendelea kuwepo mpaka walipoitwa katika ukumbi wa mkutano na
msemaji wa jeshi hilo afande Advera Senso.
Hata hivyo afande Senso hakuwa na la ziada zaidi ya
kurudia yaleyale ambayo wanahabari walikuwa wakiyajua na ndiyo maana walikuwa
hapo.
"Sisi tumewaita viongozi hawa wa CHADEMA ili
kuwahoji na ikiwezekana watupe ushirikiano kutokana na taarifa zao walizozitoa
wiki iliyopita kuwa wanatishiwa maisha na baadhi ya watu wa jeshi la
polisi," alisema Senso.
wiki iliyopita viongozi wa chama hicho wakiongozwa na
mwenyekiti wao Freeman Mbowe waliita wanahabari makao makuu ya chama hicho mtaa
wa Ufipa Kinondoni wakidai kuna wana usalama wanafuatilia nyendo za Katibu mkuu
wao Wilbrod Slaa, mbunge wa Ubungu John Mnyika na aliekuwa mbunge wa Arusha
mjini Godbless Lema.
Lakini baada ya jeshi la polisi kupewa agizo na waziri
wa mambo ya ndani Dk Emmanuel Nchimbi, kuwa wachukue maelezo za viongozi hao,
chadema waligoma kutoa ushirikiano wowote kwa jeshi hilo kwa madai hawana imani nalo.
NB: Samahani wadau nilipiga picha nyingi lakini kamera
ya jembe imeleta hitilafu sikuweza kuziweka kwenye mtandao. Ila nawaahidi
ikikaa sawa nitawawekea nanyi mfaudu..
HAFIDH KIDO
0713 593894/ 0752 593894
DAR ES SALAAM ,
TANZANIA
hafidhkido@yahoo.com

No comments:
Post a Comment