Friday, July 13, 2012

Jamaa ataka kupigwa na wanachama wa Yanga kwa kutaka kuvuruga uchaguzi.

Huyu ndie jamaa mwenyewe alietaka alietaka kufuturiwa na wanazi wa Yanga leo asubuhi.


Jamaa mmoja mida hii chupuchupu agombewe na wanachama wa Yanga, baada ya kufika makao makuu ya klabu, Jangwani akiwa na barua ya wakili  inayoshauri uchaguzi wa klabu hiyo uliopangwa kufanyika Jumapili wiki hii uahirishwe.

Kilichomponza ni kwamba, alipofika mlango wa kuingia klabuni, akasema anataka kumuona Katibu Mkuu, ana barua ya Mahakama ya kuzuia uchaguzi.

Watu kusikia hivyo wakamvaa, kwanza wakampora begi lake wakachukua barua wakaisoma. Wakagundua ni ya wakili tu na haina nguvu, ndipo wakamrudishia barua yake na kumfukuza, tena wakimuonya asionekane kabisa katika viunga hivyo. Soma barua yenyewe….

Chanzo: www.bongostaz.blogspot.com

No comments:

Post a Comment