Thursday, July 5, 2012

Tukuyu Stars Wanataka kufufuliwa upya....





Timu ya mpira wa miguu ya mkoani Mbeya Tukuyu Stars imeamua kurudi upya ili kuwapa burudani wapenzi wa soka wa mkoa huo.

Akizungumza na wanahabari katika ukumbi wa idara ya habari MAELEZO leo asubuhi msemaji wa timu hiyo Kennedy Mwaisabula, amesema imefika wakati wameamua kuunda kamati maalum itakayoirudisha timu hiyo katika ligi kuu ya Tanzania bara ili kurudisha ile burudani iliyokosekana kwa kipindi kirefu.

Itakumbukwa Tukuyu Stars ni miongoni mwa timu chache zisizozidi saba za Tanzania bara kuweza kunyakua ushindi wa ligi kuu hapa nchini.

Timu hiyo ilipanda daraja mwaka 1985 na kufanikiwa kuchukua ubingwa mwaka 1986, ni timu iliyoweka rekodi ambayo haijawahi kuvunjwa mpaka sasa kwa kupanda daraja ndani ya mwaka mmoja na kufanikiwa kuchukua ubingwa mwaka uliofuata.

Baadhi ya wachezaji waliowahi kungara na timu hiyo ni Justin Nicodemus Mtekele (marehem), Aston Pardon, Sekilojo Chambua, Hussein Zito, Stephen Mussa (Marehem), Jabir Mohamed (Marehem), Peter Mwakibibi, Godwin Aswile (Scania), Salum Kabunda (Ninja), na wengine wengi.

HAFIDH KIDO
 0713 593894/ 0752 593894
DAR ES SALAAM, TANZANIA
<








                        Wadau wanaotaka kuifufua Tukuyu Stars wakizungumza na wanahabari leo.

               Kushoto kabisa alievaa shati la mistari ni mchezaji wa zamani wa Tukuyu Stars Godwin Aswile.

                Jembe lililowahi kuchezea Tukuyu Stars, Simba na Timu ya Taifa Mosses Mkandawile (Golikipa)

No comments:

Post a Comment