Thursday, July 12, 2012

blogu ya kido jembe imefikisha wadau 2380. Usingoje kusimuliwa jiunge sasa.


Ndugu zangu

Namshukuru Mungu mambo yanazidi kuniendea vizuri katika shughuli yangu hii ya blogu. Ni ndoto yangu ya muda mrefu kumiliki blogu yenye habari mchanganyiko. Kawaida sipendi kilema cha habari (kuegemea mrengo mmoja).

Nilianza kama utani tu mwezi uliopita, kwa sasa nina mwezi mmoja na siku chache tangu nianze kutuma habari yangu ya kwanza katika blogu hii ya kijamii.

Nilianza na wastani wa watu 15 kwa siku, lakini mpaka ninavyozungumza leo tarehe 12 july, 2012 Alhamisi saa nne na nusu asubuhi (10:30am) nilikuwa na watu 104. zingatia si watembeleaji wa wakati wote, bali tangu siku ya leo ianze asubuhi mpaka saa nne blogu yangu imetembelewa na wadau 104  'wakati awali nilikuwa na watembeleaji 15 kwa siku nzima'.

Hivi ninavyoandika tangu asubuhi mpaka saa sita na nusu mchana nimeshatembelewa na wadau ‘157  ‘ ambapo ni ongezeko la wastani wa wadau ‘53‘ ambayo ni ongezeko la asilimia takriban ‘40‘ ndani ya saa mbili. Ni hatua kubwa sana kwa wanaojua takwimu.

Watu wote waliowahi kuembelea blogu yangu tangu ianzishwe wamefikia ‘2380‘ mpaka hivi ninavyoandika. Hivyo usingoje kusimuliwa mafanikio haya yanasababishwa na nini, nadhani wadau wangu wanapenda vitu mchanganyiko.

Huwa ninajaribu kuandika kila ninachokiona na kupiga picha kila kinachojipitisha katika kamera yangu, sitaki mchezo.

Napokea marekebisho na ushauri wa aina yoyote juu ya kuifanya blogu hii kuwa imara na ya kihabari zaidi, kila unapohisi kuna habari unataka itolewe usisite kuwasiliana na mimi kwa namba za hapo chini na barua pepe.

Nawashukuru sana kuwa pamoja nami kupambana na umaskini, kipo kitu nitaongea kesho juu ya ahadi niliyompa rafiki yangu Evans Musoka, vipi nitapambana na umaskini nilipokuwa mgeni wake nchini Kenya.

HAFIDH KIDO
DAR ES SALAAM, TANZANIA
0713 593894/ 0752 593894
hafidhkido@yahoo.com

No comments:

Post a Comment