Tuesday, July 10, 2012

Chadema wanena....... leo mchana.

                                      Dk Slaa akimwaga cheche....

                     Hapa akifafanua jambo juu ya matamshi ya dharau ya Serikali.

                                  Akizungumza na makamanda wake baada ya kumalizana na wanahabari..

wanahabari wakifuatilia kwa makini maneno ya katibu mkuu wa chadema makao makuu ya chama hicho leo mchana.


Na Hafidh Kido

Chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA), kimetoa tamko la kulaani kitendo cha Serikali kupitia waziri wa mambo ya ndani na Katibu mkuu mtendaji Ikulu, kusema taarifa za viongozi wa chama hicho kutishiwa maisha yao ni kujitafutia umaarufu.

Akizungumza na waandishi wa habri katika ofisi za makao makuu ya chama hicho katibu mkuu wa CHADEMA Dk Wilbrod Slaa, amesema chama chao ni chama makini na hakitafuti umaarufu wa kisiasa kwani ikiwa wanataka umaarufu wataupata kupitia shughuli zao wanazozifanya katika kulitetea taifa.

“Wapo watu kama Ombeni Sefue na Dk Emmanuel Nchimbi, wanasema tunajitafutia umaarufu kwa lipi….” Alihoji na kuenedelea “Kazi ya serikali baada ya kupata taarifa ni kuchunguza na si kuhoji. Kitengo cha usalama wa taifa kinapata mamilioni ya pesa wakati wa bajeti kazi yake ni nini?,” alihoji Dk Slaa.

Mbali ya kutoa dukuduku hilo pia CHADEMA kimetoa mambo manne waliyozungumza jana katika kikao cha dharura cha kamati kuu kilichokutana jana eneo la Mbezi Garden kuwa ni kufanya awamu nyingine ya ziara za mikoani baada ya kumalizika kwa operesheni sangara.

“Sisi si chama cha msimu, tunahakikisha tunatembelea kila eneo ili kutetea maslahi ya mtanzania wa kawaida, awamu ya pili ya operesheni sangara tulimaliza robo tatu ya nchi nzima na sasa tumepanga kufika katika mikoa mitano Singida, Dodoma, Morogoro, Iringa na Manyara,” alisema.

Aidha katika kuhakikisha wananchi wa hali ya chini wanafikiwa Dk Slaa amesema watatumia siku 44 kutembelea majimbo 44, kata 806 na vijiji 4000 vya mikoa hiyo mitano.

“Katika maeneo yote hayo tutapiga kelele na kupinga upotoshwaji wa kiharakati kama unaofanywa na Waziri mkuu Mizengo Pinda ambae akili zake zimeganda. CHADEMA siyo chama cha msimu kama vilivyo vyama vingine vinavyosubiri uchaguzi tu.

“Sisi tunadai ‘change’ yetu ya Rada, Meremeta, Tan Gold, Deep Green na miradi mingine ya kifisadi. Kamwe hatutanyamaza bali tutaendelea kupiga kelele mpaka kieleweke. Na kauli mbiu mpya ya operesheni hii ni hakuna kula, kunywa wala kulala mpaka kieleweke,” Dk slaa.

Mambo mengine ambayo yaliazimiwa jana katika kikao maalum cha kamati kuu ni kuanzisha anuni ya kupinga rushwa ndani na nje ya chama, kupima uwajibikaji wa wabunge wa chama hicho mpaka madiwani na wenyeviti wa vijiji na serikali za mitaa. Kadhalika wataliangalia kwa undani sualala kukusanya maoni ya mabadiliko ya katiba ili kuhakikisha hakuna upotoshwaji kama ilivyokuwa katika kamati ya wali ya jaji Kisanga.

Siku ya juzi viongozi wa CHADEMA wakiongozwa na mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe, waliitisha mkutano na waandishi wa habari makao makuu ya chama hicho kuzungumzia tatizo la viongozi wa chama hicho John Mnyika, mbunge wa Ubungo na Dk Slaa katibu mkuu wa chama hicho.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa juzi ni kuwa wapo watu ambao walitumwa mjini Dodoma kuchunguza nyendo za Mnyika ili kujua anapolala, anapokula na anapotembea.

Lakini cha kushangaza viongozi wa serikali wakiongozwa na Waziri wa mambo ya ndani Dk Nchimbi kuwa viongozi hao wa CHADEMA si kweli kuwa wanafuatiliwa maisha yao badala yake wanatafuta umaarufu wa kisiasa.

HAFIDH KIDO
0713 593894/ 0752 593894
DAR ES SALAAM, TANZANIA.



No comments:

Post a Comment