Saturday, July 14, 2012

Mwaka mmoja tangu dada Charity Tunda aage dunia. Shughuli hii ilifanyika leo maeneo ya Kiluvya kwa Komba nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.



 Hapa nikiwa na jembe langu Danny, pembeni ni mama yake marehem Charity nyumbani kwao Kiluvya leo.

 Hapa nikiwa na dada wa majembe Editha, rafiki karibu wa marehem jembe la mass comm hili KIU. Maskini amemaliza chuo akiwa mpweke 'classmate' wake Mungu amempenda zaidi. Akijifariji na mama Tunda.

Hawa ni mama wa marafiki wawili vipenzi. Kushoto ni mama yake Editha na kulia ni mama yake Charity.

Na Hafidh Kido


Mwaka mmoja sasa umefika tangu uondoke dada yetu Charity Tunda, najua inatosha sasa kuhuzunika ila moyo wangu ulifanya simanzi niliposimama mbele ya kaburi lako na akili ikanambia ndani ya nyumba ile ya milele kumelala mifupa baridi ya mtu niliemthamini na kumpenda sana.

Hata sasa siwezi kusahau tabasamu lako na kicheko cha kutia matumaini, pia siwezi kusahau huruma yako kila nilipokuja katika chumba chako tukiwa chuoni Kampala, vinywaji vya maji ya matunda, chakula na kutazama Ze Comedy kwenye kin’gamuzi chako. Pia sitosahau namna ulivyokuwa ukinilazimisha kuja kukutembelea kila nilipokutupa. Bado natamani kusafiri basi moja ukiwa pembeni ya kiti tukielekea chuoni.

Yataonekana ni mambo ya kijinga kuyakumbuka lakini kwangu yalikuwa na maana sana kwa umri tuliokuwa pamoja. Sitosahau namna ulivyokuwa ukiipenda picha ya mwanangu Hafidh jr, kila nilipoingia chumbani kwako nilifarijika namna ulivyokuwa ukiitandaza kwenye meza picha ile.

Hatuna cha kufanya zaidi ya kumuomba Mungu akupokee vema na akusamehe kila baya ulilofanya ukiwa duniani.

HAFIDH KIDO
0713 593894/ 0752 593894
DAR ES SALAAM, TANZANIA
www.Kidojembe.blogspot.com

No comments:

Post a Comment