Thursday, July 12, 2012

Safari ya Rais Jakaya Kikwete nchini Uingereza aka kwa Bibi.

 Rais Jakaya Mrisho kikwete, Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda na mkewe Mama Janet Museveni, Waziri Mdogo wa Uingereza wa Maendeleo ya Kimataifa Bw. Stephen O'Brien (kulia) na Mama Melinda Gates wakibadilishana mawazo kabla ya kuhutubia.

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake katika mazungumzo na Afisa Mtendaji Mkuu wa British Gas (BG Group), Sir Frank Chapman (wa pili kulia) na maafisa waandamizi wa kampuni hiyo.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri Mdogo wa Maendeleo ya Kimataifa wa Uingereza Bw. Stephen O'Brien jijini London, ambapo Uingereza iliahidi kuendelea kuisaidia Tanzania katika mambo mbalimbali ya maendeleo ikiwa ni pamoja na kusaidia kuendeleza sekta ya nishati hususan utafutaji wa gesi asilia.




Kikwete amehutubia mkutano wa kwanza wa aina yake duniani ulioanzisha Mchakato wa Dunia wa kuwawezesha wanawake katikanchi maskini kuweza kupata taarifa sahihi juu ya kupanga uzazi bora.

Mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa Queen Elizabeth II jijini London July 11, 2012 utalenga kuwawezesha wanawake wapatao milioni 120 katika nchi masikini zaidi duniani kupata habari, huduma na mahitaji ya kupanga uzazi bora zaidi na kuokoa maisha yao ifikapo mwaka 2020.

Mbali na mkutano huo Rais Kikwete alifanya mazungumzo na kampuni ya gesi asilia ya British Gas (BG Group)  kampuni hiyo imewekeza kiasi cha Pauni 80 za Uingereza (Shilingi Trilioni 125) katika mradi wa kuchimba gesi asilia nchini Tanzania, na tayari visima vitano vya nishati hiyo vimeshatema gesi nyingi katika bahari kuu kusini mwa Tanzania maeneo ya Mtwara.

Hii ilikuwa ni ziara fupi katika makao makuu ya BG Group mjini Reading, Uingereza ambako Rais Kikwete na ujumbe wake walitembelea Julai 11 kujionea namna kazi za uvumbuzi wa gesi asilia unavyofanywa na kampuni hiyo yenye kufanya shughuli zake katika nchi 21 katika mabara matano, ikiwa na jumla ya wafanyakazi 6,000.

NB: Habari hii imehaririwa na Kido Jembe lakini habari kamili imetolewa kwa hisani ya mjengwa blog.

No comments:

Post a Comment