Saturday, December 15, 2012

Nelson Mandela afanyiwa upasuaji wa kifuko cha nyongo kutolewa mawe...


Ikulu ya rais wa Afrika Kusini inasema kuwa Nelson Mandela amefanyiwa uperesheni mjini Pretoria, kutolewa mawe ndani ya kibofu nyongo na anasemekana anaendelea vizuri.

Rais huyo wa zamani wa Afrika Kusini mwenye umri wa miaka 94, alilazwa hospitali juma moja lilopita kutibiwa mapafu, na ukaguzi ukaonesha mawe hayo kwenye kibofu.
Katika taarifa iliyotolewa na serikali, imearifiwa kuwa madaktari waliamua kushughulika na mapafu yake Bwana Mandela kwanza, kabla ya kufanyiwa upersheni wa Jumamosi.
Wakuu wa Afrika Kusini wamelaumiwa kuwa hawakuwa wakieleza hali ya Bwana Mandela, ambayo imechochea wasi-wasi zaidi kuhusu afya yake.

wakati huohuo huko nchini Misri inaripotiwa kuwa.......Wananchi wengi wa Misri wamejitokeza kushiriki kwenye kura ya maoni kuhusu katiba iliyogawa nchi, huku kukiwa na ulinzi mkubwa katika duru ya kwanza ya kura hiyo.
Upigaji kura uliongezwa muda wa saa mbili katika majimbo kumi pamoja na Cairo na Alexandria, ambako kura inafanywa Jumamosi.
Mkuu wa jeshi aliiambia BBC kwamba ameridhika na hali ndani na nje ya vituo vya kupigia kura.
Lakini upinzani wa ushirikiano wa National Salvation Front umekilaumu chama cha Muslim Brotherhood kuwa kimefanya udanganyifu kwenye kura.
Upinzani unasema katiba iliyopendekezwa inaelemea sana upande wa Uislamu na hailindi haki za raia.
Duru ya pili ya kura ya maoni itafannywa baada ya juma moja.
Chanzo: BBC Swahili.

No comments:

Post a Comment